F16 Falcon
JF-Expert Member
- Dec 16, 2022
- 750
- 1,632
Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema anatazamia kuona Umoja wa Afrika (AU) unakuwa mwanachama kamili wa mataifa ya G20, akizungumza wakati wa kuanza kwa mkutano wa viongozi wa Afrika mjini St Petersburg.
"Tunatumai kuwa uamuzi huu utafikiwa mwanzoni mwa Septemba, wakati wa mkutano wa kilele wa G20 huko New Delhi," Bw Putin alisema.
"Kama hapo awali, Urusi iko tayari kufanya kila linalowezekana kukuza uimarishaji wa uhuru wa mataifa ya Afrika, kusaidia kuifanya Afrika kuwa moja ya washirika muhimu katika mfumo mpya wa mpangilio wa ulimwengu wa pande nyingi," aliongeza.
Akihutubia uamuzi wa Urusi kujiondoa kwenye mkataba ulioidhinishwa na Umoja wa Mataifa wa kuruhusu usafirishaji wa nafaka kutoka bandari za kusini mwa Ukraine, na hatimaye kuelekea Afrika, Bw Putin alisema kuwa Urusi inaweza kuziba pengo hilo.
Aliongeza kuwa Urusi itaweza kutoa nafaka bure kwa nchi sita za Afrika katika miezi michache ijayo.
Viongozi wachache wa Kiafrika wanashiriki katika mkutano huo ikilinganishwa na tukio la lililopita kama hilo, kufuatia uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.
"Tunatumai kuwa uamuzi huu utafikiwa mwanzoni mwa Septemba, wakati wa mkutano wa kilele wa G20 huko New Delhi," Bw Putin alisema.
"Kama hapo awali, Urusi iko tayari kufanya kila linalowezekana kukuza uimarishaji wa uhuru wa mataifa ya Afrika, kusaidia kuifanya Afrika kuwa moja ya washirika muhimu katika mfumo mpya wa mpangilio wa ulimwengu wa pande nyingi," aliongeza.
Akihutubia uamuzi wa Urusi kujiondoa kwenye mkataba ulioidhinishwa na Umoja wa Mataifa wa kuruhusu usafirishaji wa nafaka kutoka bandari za kusini mwa Ukraine, na hatimaye kuelekea Afrika, Bw Putin alisema kuwa Urusi inaweza kuziba pengo hilo.
Aliongeza kuwa Urusi itaweza kutoa nafaka bure kwa nchi sita za Afrika katika miezi michache ijayo.
Viongozi wachache wa Kiafrika wanashiriki katika mkutano huo ikilinganishwa na tukio la lililopita kama hilo, kufuatia uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.