Projects za Mchungaji Kimaro akiwa KKKT Kijitonyama

Hiz dini ni ujinga mtupu ni sehemu ya upigaji tu bora zipigwe marufuku mbona kuna nchi hazina huu ujinga wa makanisa na misikiti na maisha yanaenda tu na wana maendeleo kuliko huku kwenye unafiki wa dini
 
Amezifanya yeye kaka yeye au imefanyika akiwa mchungaji kiongozi wa Usharika!

Why tunatanguliza kusema projects za kimaro na sio kusema projects za Usharika wa Kijitonyama!??
Kwa haraka hapo ndio msingi wa kiburi cha Kimaro na Wafuasi wake wakasahau kuwa wafuasi wa Mungu na kazi ya Mungu wakageuka kuwa wafuasi wa mtu ambaye n Kimaro

Mkaanzishekanisa lenu ili mkamilishe lengo lenu
 
Ulitaka kujua kimaro ana kipawa..jiulize kkkt kkooo now days Iko wapi? Mbona haisikiki? Mimi binafsi nilikuwa nawahi morning glory daily kkoo kabla ya kuja job posta..baada ya kumwondoa kkoo imepoa kabisa imerudia enzi zake..kimaro kaenda knyama kaibadilisha kabisa naamini hata mapato yake yalikuwa maradufu. Ana karama ya kipekee
Ila kwa hili ingawa hatujui Nini chanzo ila naamini pande zote mbili walipaswa kutumia busara Ili kuilinda imani.kwani angetangaza kwamba ameomba likizo ya miezi miwili kwa ajili ya mapumziko kisha akaenda malizana na viongozi angepungukiwa Nini..yaelekea wamemshika pabaya anataka huruma ya raia
 
Si ndiyo zetu hizo...

Magufuli kanunua ndege sita mpya

Samia kachimba mashimo ya vyoo laki tisa

Utafikiri pesa zao...

Eti miradi ya Kimaro
 
Mapato alikua anatoa hela zake mfukoni?
 
U celebrity mpaka makanisani. Mitume karibu wote wa Yesu waliuawa na kazi ikaendelea sembuse Kimaro?

Watu wanaabudu watu siku hizi ndiyo maana wako tayari hata kuwa abused kisa tu eti ni mtumishi mwenye "upako" na miujiza haijalishi upako huo ni wa nuru au giza.

Kimaro atapita na kazi ya Mungu itaendelea!
 
Hapo Yesu hakuwasifia bali aliwaponda mafarisayo ,pia zaidi ya Mara moja aliwaponda sehemu zingine.

Mathayo 23:13

[13]Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnawafungia watu ufalme wa mbinguni; ninyi wenyewe hamwingii, wala wanaoingia hamwaachi waingie.
 
Vuongozi wengi sana siku hizi pamoja na waumini wao wanaangalia zaidi ya kimwili kama miradi na uwekezaji na kusahau kujijenga na kukua kiroho
Mkuu Mshana Jr Yale mambo yako ya matunguli uliacha ukawa mkristo? Nakuuliza sio kwa ubaya ila nakumbuka JF 2016 ulivyowasha moto Na habari za majini Na mortuary Na mapicha picha kibao
 
Mkuu Mshana Jr Yale mambo yako ya matunguli uliacha ukawa mkristo? Nakuuliza sio kwa ubaya ila nakumbuka JF 2016 ulivyowasha moto Na habari za majini Na mortuary Na mapicha picha kibao
Labda amenunua wokovu na miujiza kama Simoni mchawi wa enzi za akina Paulo🤣🤣🤣
 
Mkuu hapa unazungumzia Dayosisi ya Kaskazini Kati na hayo yote vinamilikiwa na Kaskazini Kati.
 
wewe kkoo morning glory mbona bado inabamba sana tena sadaka zimezidi kuliko hata alivyokua mch kimaro
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…