Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 3,119
- 1,428
Mbunge wa Musoma Vijijini, Profesa Sospester Muhongo ametajwa kutekeleza vema aliyoyaahidi jimboni kwake.
Mbunge huyo ambaye pia ni mwanataaluma bobezi ameng'ara kwa namna alivyowatumikia wapiga Kura wake katika kipindi cha miaka mitano inayomalizika.
Utekelezwaji wa ilani ya CCM jimboni Musoma Vijijini umetajwa kuwa wa kitaalamu unaokipa haiba njema Chama cha Mapinduzi kwa Wananchi wa jimbo hilo.
Miradi ya Maji, shule zikijumuisha maabara za masomo ya sayansi, zimempa Mbunge huyo upendo mkubwa miongoni mwa wananchi
Muhongo ambaye Awamu ya Nne mwishoni na Awamu ya tano mwanzoni alikuwa Waziri wa nishati na madini aliyefanya mabadiliko makubwa katika sekta hizo ametajwa kuwa Mbunge aliyetumia wakati mwingine jimboni kwake akishiriki, kusimamia miradi pamoja na kusaidia wananchi wa jimbo hilo katika masuala ya kijamii.
Ili kuweka kumbukumbu, ofisi ya Mbunge huyo, imechapisha vitabu vyenye kuonesha utekelezaji wa ilani ya CCM jimboni humo kwa kipindi cha 20/25.
"Profesa Muhongo ametisha" , ameandika Mwananchi mmoja kwenye ujumbe mfupi akionesha kufurahia kwake kazi nzuri iliyofanywa na Mbunge huyo wa Musoma Vijijini.
Profesa Muhongo aliingia Bungeni mwaka 2015, akachaguliwa kwa kura za kishindo mwaka 2020, utekelezaji wake wa ilani jimboni Musoma Vijijini, umeliweka jimbo hilo kuwa moja ya ngome imara ya Chama hicho katika chaguzi zote.