Profesa huyu anastahili pongezi za dhati

Profesa huyu anastahili pongezi za dhati

Manyerere Jackton

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
2,438
Reaction score
4,461
Wiki hii nimefika Mwanga mkoani Kilimanjaro. Nimedhuru vijiji kadhaa kama Mgagao, Ngulu, Lembeni na Kwakoa. Hapo kwakoa nimekuta kitu cha hamasa sana. Kuna jengo kubwa mno la kisasa linajengwa na Profesa Ngoma.

Ni hospitali, chuo na kwa shughuli nyingine. Kwakoa ndipo alipozaliwa Profesa huyu, hakika mradi huu ni wa mfano kwa wasomi kukumbuka kuwekeza kwao. Profesa ngoma si wa kujikweza, lakini nadhani anastahili pongezi nyingi akingali hai. Wasomi wakifanya mambo makubwa ya aina hii bila shaka vijana wengi watapenda kuishi vijijini.

Naomba wanahabari wazuru kwakoa wajionee fahari hii ya mtanzania huyu.
 

Attachments

  • 20140810_160208.jpg
    20140810_160208.jpg
    553.7 KB · Views: 814
  • 20140810_160323.jpg
    20140810_160323.jpg
    439.7 KB · Views: 684
Sio siri anatendea haki u profesa wake kwa kuwa na impact kubwa kwa jamii yake hata hospitali zake huduma nzuri
 
Vipi uhalali wa upAtikanaji wa Fedha hizi?!!
 
Je, hizo pesa ni zake au za wahisani?

Pesa kuwa yakwake au yawahisani haituhusu!! Kikubwa ni pongezi kwakufanya huo mradi kijijini kwake'

Hiyo ni alama ya ukumbusho na mchango wa elimu yake kwajamii alikozaliwa.

Pongezi kwako Prof..
 
Mkuu Manyerere, asante!. Kwanza nakuu mkono pongezi zako kwa Prof. Ngoma, na kuungana na wito watu, watu wenye uwezo, wakumbuke makwao, wawekeze makwao na kuinua makwao kama CRS ya kurudisha kile kidogo with appreciation!.

Bila kujali sources of fund, tunachoangalia hapa ni "The end justifies the means!", ila mimi naomba niende a bit deeper zaidi katika "the motive behind" ziara yako kuzuru kijiji hicho!. Kama ulikuwepo hapo kwa safari zako nyingine, na ikatokea tuu ukauona huo mjengo, ukahamasika na kuutumia ku inspire na wengine, then its very fine!.

Lakini kama ulifanya "facility visit", kwa lengo hilo tuu, whoever facilitated that "visit kutembelea maendeleo ya enero hilo", might have "motive behind" with a good intention "watu" waone maendeleo ya "see what this man is doing for us!", hive mbunge wa eneo hilo ni nani vile?!, ili na mimi nimlobby a sponsored tour, atutembeze atuonyeshe amefanya mini, vinginevyo 2015...

Hongera zake Prof. Ngoma!.
Asante.
Pasco
 
Hata kama ni ufadhili, ametumia akili na utu kwa kutambua kuwa vijijini nako wana haki ya kusogezewa huduma muhimu kama hizo. Lakini kubwa ni kwamba profesa amerejesha fadhila kwa ndugu na jamaa waliohangaika kumsokesha. Matunda ya usomi wake kayajeresha nyumbani. Hili ni jambo la kuigwa na wengi wetu.
 
Pasco, ziara yangu inahusu migogoro ya ardhi. Ilitokea tu nilipofika hapo nikaona hilo jengo. Nikajibiwa kuwa ni kazi ya huyo msomi. Hakika nikawa sina jingine, isipokuwa kumpongeza na kuwapa hamasa watanzania wasomi wengine kufanya mambo makubwa kama haya
Kwa hiyo hiku kitu nilikutana nacho tu kwa "bahati mbaya'.
 
Hapa tusiangalie uhalali, tunaangalia investiment ambayo ina tija kwa jamii tena vijijini,hata wale wezi wasingepeleka uswiz badala yake wangewekeza nchini ningewapa pongezi.
Nimekubali, kwahiyo tuhamasishe wezi waongeze juhudi za kuiba ili wawekeze ndani??!!
 
Pasco, ziara yangu inahusu migogoro ya ardhi. Ilitokea tu nilipofika hapo nikaona hilo jengo. Nikajibiwa kuwa ni kazi ya huyo msomi. Hakika nikawa sina jingine, isipokuwa kumpongeza na kuwapa hamasa watanzania wasomi wengine kufanya mambo makubwa kama haya
Kwa hiyo hiku kitu nilikutana nacho tu kwa "bahati mbaya'.
Hapo professor anastahili pongezi siyo hii mi-professor mingine she.nzy type inakimbilia siasa tu na huko inatuchosha tu wala hatuoni cha maana wanachokifanya. Muhongo, Maghembe, Kapuya the list goes on and on and on....................
 
Hapo professor anastahili pongezi siyo hii mi-professor mingine she.nzy type inakimbilia siasa tu na huko inatuchosha tu wala hatuoni cha maana wanachokifanya. Muhongo, Maghembe, Kapuya the list goes on and on and on....................

hao wote wameacha taaluma yao wamekimbiliaa kwenye siasa....
 
Hata zikiwa za wahisani, bado haimuondolei uzalendo huyu Profesa.

Ndio zenu nyie magamba kuhalalisha wizi kwa kigezo tu eti amejenga kijijini kwao!! Fanyeni forensic audit pale Ocean Road hospital ili mjue ukweli.
 
Hiki ni kielelezo kuwa serikali bado imelala na bado inategemea makabaila ndio wawekeze hadi kwenye huduma muhimu kama hizi...
 
Hongera Wachaga ,sasa kilichobaki ni kuchukua nchi basi kilimanjaro itakuwa kama "london
 
Wiki hii nimefika Mwanga mkoani Kilimanjaro.

Nimedhuru vijiji kadhaa kama Mgagao, Ngulu, Lembeni na Kwakoa.

Hapo kwakoa nimekuta kitu cha hamasa sana.

Kuna jengo kubwa mno la kisasa linajengwa na Profesa Ngoma.

Ni hospitali, chuo na kwa shughuli nyingine. Kwakoa ndipo alipozaliwa Profesa huyu, hakika mradi huu ni wa mfano kwa wasomi kukumbuka kuwekeza kwao.

Profesa ngoma si wa kujikweza, lakini nadhani anastahili pongezi nyingi akingali hai.

Wasomi wakifanya mambo makubwa ya aina hii bila shaka vijana wengi watapenda kuishi vijijini.

Naomba wanahabari wazuru kwakoa wajionee fahari hii ya mtanzania huyu.

Umedhuru, au umezuru? Angalia kiswahili chako bwana!!
 
Back
Top Bottom