wana JF tuondokane na mawazo ya kupandikizwa tena nashauri tuwe makini katika baadhi ya thread. Je Baregu si Profesa? Kahigi Je? Mbona hawa walipojiunga na CHADEMA watu hawakusema wanaandaliwa kugombea Urais mwaka 20!5? Tusisahau kuwa Profesa Safari amejiunga CHADEMA akitokea CUF hivyo nashauri tuwe makini na baadhi ya mada kwani zinaweza kuwa na nia ya kuleta migogoro na mfarakano. Hebu jiulize, je wafuasi wa ZK watajisikiaje ikiwa watasadiki hayo? Nadhani kwa chama kinachozingatia Demokrasia kila mwanachama ana haki kugombea nafasi yoyote ndani ya chama au kitaifa.