AZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya, amewaeleza Watanzania kuwa baada ya kuugua kwa muda mrefu hivi sasa afya yake imeimarika kwa kiasi kikubwa na anasonga mbele kuwatumikia wananchi kwa ujumla.
Mwandosya aliyasema hayo jana Mbeya wakati akitoa salamu kwa wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM katika Viwanja vya Bustani ya Jiji mkoani hapa, baada ya kumalizika kwa matembezi ya mshikamano ya kuadhimisha miaka 37 ya kuzaliwa chama hicho.
Maandamano hayo yaliongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete.
"Si mmeniona jamani afya yangu imeimarika hivyo kilichobaki ni kuchapa kazi na kusonga mbele katika kuwatumikia Watanzania," alisema Mwandosya ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rungwe Mashariki.
Kwa muda mrefu alikuwa anasumbuliwa na matatizo ya kiafya na sasa afya yake imerudi katika hali ya kawaida na kuwapa moyo wapigakura wake, ambao kwa muda walikuwa na wasiwasi kutokana na kuugua kwake.
Mbali na Mwandosya pia viongozi mbalimbali wa kitaifa akiwemo Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho, Taifa Philip Mangula, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Naibu Waziri wa Kilimo na Chakula, Godfrey Zambi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama hicho mkoani Mbeya, Waziri wa Uchukuzi, Dkt Harrison Mwakyembe na viongozi wengine walishiriki matembezi hayo.
Matembezi hayo yaliyoanzia Soweto saa 1.30 na kumalizika saa 2.15 asubuhi, wananchi walijitokeza kwa wingi na wengine wakisimama kandokando ya barabara huku wakionesha kushiriki pamoja na viongozi na wanachama, wakereketwa wa CCM.
Awali, wananchi waliopata fursa ya kuzungumza na gazeti hili kuhusiana na hali ya kisiasa mjini hapa walisema kuwa kwa mara ya kwaza haijawahi kutokea wananchi hao kujitokeza kwa wingi katika sherehe za Chama hicho, kutokana na upinzani wa kisiasa uliokuwepo.
Source: majira.co.tz
Mwandosya aliyasema hayo jana Mbeya wakati akitoa salamu kwa wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM katika Viwanja vya Bustani ya Jiji mkoani hapa, baada ya kumalizika kwa matembezi ya mshikamano ya kuadhimisha miaka 37 ya kuzaliwa chama hicho.
Maandamano hayo yaliongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete.
"Si mmeniona jamani afya yangu imeimarika hivyo kilichobaki ni kuchapa kazi na kusonga mbele katika kuwatumikia Watanzania," alisema Mwandosya ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rungwe Mashariki.
Kwa muda mrefu alikuwa anasumbuliwa na matatizo ya kiafya na sasa afya yake imerudi katika hali ya kawaida na kuwapa moyo wapigakura wake, ambao kwa muda walikuwa na wasiwasi kutokana na kuugua kwake.
Mbali na Mwandosya pia viongozi mbalimbali wa kitaifa akiwemo Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho, Taifa Philip Mangula, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Naibu Waziri wa Kilimo na Chakula, Godfrey Zambi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama hicho mkoani Mbeya, Waziri wa Uchukuzi, Dkt Harrison Mwakyembe na viongozi wengine walishiriki matembezi hayo.
Matembezi hayo yaliyoanzia Soweto saa 1.30 na kumalizika saa 2.15 asubuhi, wananchi walijitokeza kwa wingi na wengine wakisimama kandokando ya barabara huku wakionesha kushiriki pamoja na viongozi na wanachama, wakereketwa wa CCM.
Awali, wananchi waliopata fursa ya kuzungumza na gazeti hili kuhusiana na hali ya kisiasa mjini hapa walisema kuwa kwa mara ya kwaza haijawahi kutokea wananchi hao kujitokeza kwa wingi katika sherehe za Chama hicho, kutokana na upinzani wa kisiasa uliokuwepo.
Source: majira.co.tz