Prof. Mukandala 'aifilisi' UDSM

Prof. Mukandala 'aifilisi' UDSM

HUYU baba ameharibu chuo hadi basi. Inafikia hatua ukiwa mhaya au mchaga unakuwa na advantage ya kujihakikishia ulaji na nafasi hapo chuoni. Hivi inakuwaje mtu mwenye elimu na akliyejichanganya maeneo mbali mbali anafanya mambo kama haya bila hata aibu??
 
Kuna ndugu mmoja aliniambia kuwa katika kipindi hiki cha uchaguzi kila mmoja anasema lake, kila mmoja anakuja na propaganda kwa yeyote na kwa namna yoyote. Nilipoona ujumbe wa vuta nkuvute nikafananisha na yale niliyoambiwa na yule ndugu. Kiukweli sijaelewa mleta mada anataka kutuambia nini. Kama kawaida yangu huwa sikurupuki kushabikia hoja kabla ya kufanya kautafiti. Ndugu oim2015 ameeleza vyema kuhusu maendeleo yanayoonekana UDSM na chuo kinavyojitegemea. Kuna ndugu amesemea ni majungu. Huko mi sitaongelea sana ila nitaongelea utafiti mdogo na wa haraka nilioufanya UDSM siku ya leo. Malengo yangu yakiwa ni kujibu maswali yafuatayo Prof Mukandala yupo safarini, kama ndiyo kwa shughuli ipi? chuo kimefilisika? Ipo miradi iliyosimama kwa kukosa pesa? Kama ndiyo tatizo liko wapi? Na mwisho swala la hati chafu na ukabila nimeliweka by the way maana ni shutuma zilizojileta (shutuma mjongeo). Matokeo ya kautafiti kangu ni kama ifuatavyo:--

kwanza ni kweli Prof. Mukandala yuko safarini kikazi na kwa mujibu wa ushahidi usio na shaka kuwa ni safari ya kikazi.-

Pili, chuo hakijafilisika, kwa kuwa ni chuo cha umma ambacho mapato yake yanatoka serikalini, utafiti na ushauri wa kitaalam, miradi ya kimaendeleo, ada toka kwa wanafunzi na kutoka kwa wafadhili ambao ni wahitimu na wadau wa elimu.-

Miradi imesimama ama la and why? Kwa mujibu wa chanzo toka kwa msarifu mkuu wa UD, ni kwamba kila mradi una chanzo chake cha mapato hivyo haiwezekani mtu akachukua fedha za miradi kwa matumizi tofauti na ilivyopangwa labda litokee janga. Amenipa mifano aliyoitoa oim2015 pamoja na extension ya jengo la utawala ambalo nilishuhudia mafundi wakiwa kazini.-

Kuhusu hati chafu nijikuta naulizwa swali maana ya hati chafu ni nini? Nami nikajiuliza hivi hati chafu mbona kama imekuwa personalized kwa Prof. Mukandala? Lakini mwisho nikakumbuka kaka yangu Prof. Kitila mkumbo aliwahi kuniambia nitofautishe Mukandala kama mtu na ka makam mkuu wa chuo. Nikachoka kabisa.-

Swala la ukabila kwa kweli sikulifuatilia sana si kwamba nimemdharau aliyelichomekea kwenye hoja kuu, au kwamba haijanigusa mzigua mie, bali naitafutia muda wa kuifanyia kazi ya ziada baada ya kumuuliza mtu mmoja aliyejinasibu kuwa moja ya waanzilishi wa THTU akaniuliza je manaibu wakuu wa chuo taaluma na utawala ni wachaga au wahaya? Je mhasibu Mkuu? Je mwanasheria? Nikamjibu sijui maana siwafaham vyema na ni muda toka nimalize shahada yangu ya pili ya uhandisi.

Akaniambia ndiyo maana umekuja bila kufanya utafiti wa angalao kukagua tovuti ya chuo maana list ya viongozi wote na majina yao kwa kirefu. Nikaona aibu nikasepa.

Maoni binafsi. Ndugu zangu nadhani ni vyema tuwe na mtazamo chanya dhidi ya viiongozi kabla ya kuhukumu. Sisemi tusikosoe na sitaki kumtetea mtu, bali tusioneshe hali fulani ya chuki, giliba, fitina au kijicho hasa tukitambua sisi sote ni binadamu.
 
ukweli unabaki pale pale kwamba kuna matumizi mabaya ya fedha kwa vitu ambavyo havina tija kwa chuo.

Hivi huo ni ukweli ama umechagua kuamini hivyo kwa kuwa zinaponda ccm??

Kama ungeelewa lengo la mtoa mada ilikuwa tu kufikisha ujumbe wa mwisho.. Mkandara yupo Marekani.

Ila nataka kujua hivi vyuo za serikali vinajiendesha vyenyewe kimapato au inatokana funds kutoka serikalini kwenye maswala ya miradi kama majengo??
 
UDSM wamefanya mambo makubwa sana Kwa hivi sasa ukipita pale kuna renovation inaendelea, juzijuzi tu jengo jipya LA UDBS lilifunguliwa. Lectures wengi wamepelekwa kusoma PhDs nje ya nchi. Ukizingatia pia chuo kinajitegemea kwa kiasi kikubwa. Fanya utafiti usitoe mada za kuambiwa.

Vipi kuhusu kutapakaa kwa kinyesi na taka zenye kufanana na hizo Hall 1 & Hall V?

Wewe uliyefanya tafiti, umegundua nini juu ya kufungwa kwa vyoo pale bondeni jirani na jengo la Kiswahili (mwaka sasa havitumiki)

Tafiti zako zimetoa majibu gani juu ya utiririkaji wa Maji machafu karibia miaka miwili sasa pale Academic Bridge kama waelekea School of Law Building?

Tupe majibu ya tafiti zako kwa kuziba na kutofanyiwa marekebisho vyoo vya pale SRs na Thieta halls.

Tupe majibu ya wewe na tafiti yako, kwanini chuo kikubwa kama kile Maktaba ina Choo kimoja tu kinachoweza kutumika? (Law Collection).
 
Chuo kimerudisha heshima yake, na kiko liquid balaa. Kwa mara ya kwanza kabisa wana research fund ya kutosha. Hongera sana VC, uongozi wote na bila kusahau aliyeiona hazina ndani yako hadi akakuteua kutoka miongoni mwa wasio maarufu wala wenye godfathers
 
"Toka Lini Udsm Ilijiendesha? Miaka Nenda Miaka Rudi Udsm Haijawai Kujiendesha Toka Kipindi Cha Mwalimu Nyerere"
 
Wakati huohuo wanafunzi waudsm wanatembea vifua mbele kwamba UDSM is the best
 
Back
Top Bottom