Muhongo 2015!
Tatizo la mzee nae ana dharau sana,ushauri asipokee kwa sababu hauna tija lakini sio kwa vile umetolewa na mtu ambae hajasoma petroleum geology
Tusipojenga taifa la kuheshimu taaluma za watu tutaishia kuwapeleka Mabwepande....
Asante mkuu, Mimi ningesema tumejenga taifa lisiloheshimu taaluma ndiyo maana wengi wameishia na wataendelea kuishia Mabwepande.......Tusipojenga taifa la kuheshimu taaluma za watu tutaishia kuwapeleka Mabwepande....
kapotolo
Uko sawa kabisaaa lakini haileti maana kwa kitu usichokijua kujifunza kwa kukosoa na pili kodi katika madini haiimaninishi kuyajua madini na kimsingi ni vitu viwili tofauti ni vizuri tukaheshimu wataalam kwanza, mfano kumejengeka tabia ya wajuaji wa jinsi kama hii anayoisemea prof kuingilia hata majukumu ya kidaktari kama kutangaza kwa kusisitiza mtu kafa wakati yeye siyo daktari ama mtu fulanin kaiba wakati yeye siyo auditor, na mambo mengine mengi. wabunge wetu wetu kwa idadi kubwa hupenda sana wasikike kuliko maslahi yataifa letu nawaomba waache.
Tusipojenga taifa la kuheshimu taaluma za watu tutaishia kuwapeleka Mabwepande....
Asante sana Ben:
1. Tumemsikiliza Prof. na hakutaja jina la mtu endapo Zitto na yeyote kwa sababu za upambe au binafsi au kuchonganisha watu atafikiria hivyo basi ni wao ndio wenye hayo matatizo tena watakuwa wamethibitika kuwa ndio wanaosemwa maana duniani wapotoshaji wapo kila mahala. Mimi nikisema hapa kuwa kuna wapotoshaji wanasema kuwa JF ni mtandao wa usalama wa Taifa Tanzania. Halafu wewe kati ya watu zaidi ya milioni 45 (Watanzania) ukafikiria kuwa nakusema wewe basi itakuwa ni kweli kuwa wewe ndiye unayesema hayo!!Nitakuwa sina cha kukusaidia zaidi ya kuendelea kukufuatilia miendo yako ili nijue unachotafuta ni nini zaidi?
2. Prof. Sospeter amefafanua vyema alipoulizwa kuwa je, sasa tusiosoma tusitoe mawazo au tusisikilizwe; alisema la hasha, wananchi wote watoe mawazo yao kwenye kuchangia sera nzuri ya gesi lakini alisema anawazungumzia WAPOTOSHAJI tena wenye elimu ndogo ya certificates of attendance ambao amewapa onyo.
Naumuunga sana mkono huyu Waziri. Kwanza lazima taaluma za watu ziheshimiwe maana hata yeye mwenyewe hajifanyi kujua mambo ya mafuta maana hiyo si taaluma yake ambayo alibobae ndio maana anawaheshimu wataalamu wa eneo uzalishaji wa gesi na amesema watahusishwa sana. Pili kuna watu wenye elimu ndogo katika jambo hujifanya wajuaji na kupotosha ukweli ni lazima tuwamulike na kuwaseme maana ni wa hatari sana! Hii si ajabu kukuta hata form two students wakawa wasumbufu (kiujuaji)kuliko a form four or six student, au Private akawa mkali na mwenye majingambo (Kijeshi)kuliko Luteni au Captain wa jeshi ndivyo ilivyo watu wachache wenye vyeti vya chini wanaweza kujifanya kuwa wajuzi wa kila kitu na kudharau kazi anayoifanya Prof. Sospeter eti kwa vile tu wamepata mafunzo fulani ya muda mfupi au kaenda ziara mahala na kuuliza kuhusu Uranium au natural gas exploration.
Nimemsikiliza huyu mtu, nampa muda atekeleze anachosema na kuamini na nitamuhukumu baada ya kupima alipofikia katika yale anayoahidi lakini si upuuzi wa kupotosha. Mfano watu walisema kuwa alitaka tu bajeti ipite baada ya hapo nchi yote ingeingia gizani!! Upuuzi mtupu!! maana tunajua kuwa kuna utofauti kati ya umeme kukatika kwa sababu za uchakavu wa mitambo na miundombinu kwa ujumla na mgawo wa umeme kwa sababu za uchache wa umeme (megawatts) zinazozalishwa!! Na hili pia amelifafanua leo- well done!
Huyu jamaa kweli si mwanasiasa hata utamsikia utofauti wake na mtu anayetaka kujiingiza katika malumbano yasiyo na tija. Nilifurahia jibu alilotoa kuwa hawana mkakati wa kuwadhibiti wapotoshwaji bali wao wataendelea kuhakikisha kuwa wananchi wanapata umeme wa uhakika na hayo ndiyo tunayatafuta ukiongezea kuwa uwe ambao tunaweza kumudu gharama zake.
Kwa kweli Prof hana mfano hapa TZ. Tanesco ilikuwa imeshakuwa ni mzigo usiobebeka. Tangu enzi ya mwinyi mpaka wakati huu wa huyu jamaa anaeishi Airport mgao wa umeme na miradi ya umeme wa dharula vilishakuwa vitu visivyoepukika. Leo Prof anasema mgao haupaswi kuwepo. Hii ni ajabu kweli!!!!!!!!!!!!
Prof, as the scriptures say, you are the salt of the earth and the light of the world. Acha wahalifu na magenge yao ya kihalifu wazidi kuwa wahalifu, lakini wewe endelea kubaki nuru ya Tanzania. kama tunavyojifunza habari za akina Socretes na Pilato na wewe tutajifunza kutoka kwako tu. Mungu mbariki Prof, Mungu ibariki Tanzania
kuwa waziri ni sifa tosha ya kukufanya kuwa mwanasiasa maana cheo chenyewe ni cha kisiasa. i only say, within politicians are professionals.Vilevile muwe makini na huyu profesa asiyependa kushauriwa maana mafuta na gas ni mali ya watanzania na ajue watanzania si wote wamesoma na waliosoma wote hawajasoma kuhusu miamba. lakini wanao uhuru na haki kikatiba kuhoji mambo yanayoendelea. jiulize kama mwili wote ungekuwa jicho sikio lingekuwa wapi? ajue hata aliyemteua si mtaalam wa gesi je nae asihoji?watanzania lini tutaacha kuchukulia mambo kishabiki tukaanza kuhoji?Ebu badili heading yako mwenzio nikaenda ITV nkakuta mziki umeniboa
Ila nashukuru kwa kunikumbusha icho kipindi maana uyu mheshimiwa huwa namkubali sana he is a professional not a politician
Profesa aelewe kwamba si kila mtu atakuwa mtaalam wa kila kitu. Lakini hali hii haimuondolei yeyote yule haki ya kutoa maoni. Professa elewa kwamba watu wanao uhuru hata chini ya katiba ya sasa ya kutoa maoni kuhusu mambo yaendavyo katika nchi yao. Hii ni "fundamental right" ya kila raia, mtaalam na asiye mtaalam. Ninachokiona kwa profesa ni "intellectual arrogance."
Prof. Muhungo elewa kwamba ni juu yako na "the so called wataalam" kutafsiri na kuweka katika lugha ya kitaalam yale ambayo raia wa kwaida anayatoa kama maoni yake.
Prof. ndio maana kuna hata kura ya maoni ambayo inawahusisha wataalam na hoi hahe kama sisi. Nchi hii na rasilimali zake ni kwa wote na sio kwa wataalam. We are not children ambao wazazi watusemee.
Kiongozi tena mwenye hadhi ya Waziri anatakiwa kuelewa mambo haya na hasa lugha anayotumia kwa umma.
Nampenda Mbunge Msigwa anaposema " Anapozungumza Profesa huoni tofauti na mtoto wa darasa la pili". Tuweke mbali ushabiki wa kisiasa na tukubali "constructive criticism". There is no one with a monopoly of ideas on how to run the national economy. Certainly it cannot be the so called experts who have put this country in a hopeless situation through dubious deals and agreements signed as related to the exploitation of our mineral wealth.
By the way professor where are the Tanzanian experts with the necessary experience in the gas sector, anyway? Book knowledge, oh come on professor, you are not serious! Aren't we sailing in the same boat?
Good luck!
hapendwi kushauriwa katika lipi ?kuwa waziri ni sifa tosha ya kukufanya kuwa mwanasiasa maana cheo chenyewe ni cha kisiasa. i only say, within politicians are professionals.Vilevile muwe makini na huyu profesa asiyependa kushauriwa maana mafuta na gas ni mali ya watanzania na ajue watanzania si wote wamesoma na waliosoma wote hawajasoma kuhusu miamba. lakini wanao uhuru na haki kikatiba kuhoji mambo yanayoendelea. jiulize kama mwili wote ungekuwa jicho sikio lingekuwa wapi? ajue hata aliyemteua si mtaalam wa gesi je nae asihoji?watanzania lini tutaacha kuchukulia mambo kishabiki tukaanza kuhoji?
Anasema hakuna haja ya kuwa na mambo ya umeme wa dharura kwani ndio chanzo cha ufisadi. Asisitiza hakuna na hakutokuwa na mgao wa umeme. Asema kila mtu anaongelea mambo ya gesi,hata wasiokuwa na utaalamu wanaongelea kama wataalamu na hivyo wanapotosha umma. Kwa hayo na mengine mengi angalia ITV saa 3 usiku leo,kipindi cha dakika 45.