WA TZ WENZANGU KWANZA NAWASALIMU NYOTE HABARINI NA NATUMAI HAMJAMBO POPOTE MULIPO KWANI HII NI MARA YANGU YA KWANZA KUJIUNGA NA MTANDAO HUU AMBAO NADHANI NI MTANDAO ULIO HURU NA UNAOKARIBISHA MAWAZO TOFAUTI TOFAUTI AU SIJUI NIMEKOSEA?
BAADA YA KUSEMA HAYO LEO NIMESOMA POST MOJA KTK GAZETI LA RAIA MWEMA NA KWA KWELI NIMEVUTIWA SANA NA MGOMBEA URAIS WA CUF PROFESA LIPUMBA NA NAWAOMBA NA NYINYI HEMBU SOMENI SERA ZA CHAMA HICHI CHA CUF HALAFU TUJADILI TUONE KAMA KUNA CHAMA KINGINE CHENYE SERA BORA ZAIDI YA HIKI ASANTENI:
Prof. Lipumba: Tanzania kwanza vyama baadaye
Felix Mwakyembe
Septemba 22, 2010
Amshukia Kikwete na mkewe kwa matumizi mabaya
Mikutano yake yajaa hoja za kisomi, si burudani
Asisitiza kuunda serikali ya umoja wa kitaifa
KUNA tofauti kubwa kati ya mikutano ya kampeni za mgombea nafasi ya urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete na mgombea wa nafasi hiyo kupitia Civic United Front (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba.
Wakati ile ya mgombea wa CCM huchukua sura ya tamasha la muziki wa kizazi kipya (maarufu kama fiesta) kutokana na muda mwingi kutumika kwa burudani za wasanii mbalimbali maarufu kwa wakati huu hapa nchini, ile ya CUF inachukua sura ya mihadhara ya kisomi zaidi, ikiwa imejaa hoja nzito za kitaifa kuliko burudani.
Kutokana na sura hizo mbili tofauti za mikutano ya kampeni za wagombea hao, baadhi ya wafuatiliaji wa kampeni jijini Mbeya wanaamini kuwa ndiyo sababu vile vile ya tofauti ya idadi ya wasikiliza katika mikutano ya wagombea hao ambapo Kikwete alionekana kukusanya umati mkubwa wakati alipofanya kampeni zake mkoani Mbeya kuanzia mwishoni mwa mwezi Agosti hadi mwanzoni mwa Septemba tofauti na aliopata Prof. Lipumba aliyekuwepo jijini humo siku ya Jumamosi na Jumapili.
Wananchi waliohudhuria mikutano ya Prof. Lipumba walikuwa wachache lakini kila aliyepata hiyo bahati alionekana wazi kushiba hoja za mchumi huyo aliyebobea hapa nchini, na kama uwezo wa mgombea ndio kingekuwa kigezo kikuu cha wapiga kura, hapana shaka katika wagombea hao wawili waliopita jijini hapo hadi sasa, basi wa CUF angeibuka kidedea mkoani Mbeya .
"Kama kuzungumza, Prof. Lipumba anajenga hoja nzito sana. Sijui tu mtazamo wa wananchi na hicho chama, lakini kwa kweli hoja zake ni nzito sana," anasema mkazi mmoja wa Jiji la Mbeya.
Miongoni mwa hoja zilizowakuna zaidi waliohudhuria mikutano ya Prof. Lipumba, ni pamoja na ile ya kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa ambapo msimamo wake wa kuwaingiza kwenye serikali yake Watanzania wenye uwezo na waadilifu pasipo kujali itikadi za vyama ulipokelewa vizuri na wakazi wa mkoa huo.
Katika hoja hiyo Prof. Lipumba anasema: "Nitaunda serikali ya umoja wa kitaifa. Nitatumia watu waadilifu walioko kwenye vyama mbalimbali vya siasa. Sio kwamba walioko CCM wote ni mafisadi, wapo Watanzania wazuri tu kule, na wengine hawana vyama lakini wanashindwa kuingia kwenye uongozi kutokana na sheria zetu zilizopo."
Anasema umasikini unaowakabili Watanzania unatokana na viongozi waliopo madarakani kukosa uadilifu ambapo katika hilo anabainisha akisema: "Ikiwa mtu anakataa serikali ya umoja wa kitaifa, basi, huyo ni ajuza; hajui analolifanya au ana nia mbaya na Tanzania."
Imani ya Prof. Lipumba kuhusu serikali ya umoja wa kitaifa inaenda sambamba na kaulimbiu ya chama hicho isemayo "Tanzania Kwanza Vyama Baadaye" ambayo nayo inaoana na ile ya "Mbeya Kwanza Vyama Baadaye," na anasisitiza akisema iwapo Zanzibar wameweza kwa nini Tanzania Bara wasiweze?
Mgombea huyo wa CUF anaenda mbali zaidi ambapo anasema kukosekana kwa uadilifu katika serikali ya CCM ndiko kulikozaa sera mbili kuu za chama hicho anazozitaja kuwa ni ufisadi na matumizi mabaya ya mali za umma.
"CCM inatekeleza sera mbili, ufisadi na matumizi mabaya ya mali ya umma. Kikwete anaongoza kwa matumizi mabaya. Ni kiguu na njia, hatulii. Ile ndege ya kifahari ya serikali anayotumia inatumia dola za Kimarekani elfu sita kwa saa kila inaporuka, posho yake, Mama Salma, na wapambe.
Mama Salma naye ana safari zake utadhani ni Makamo wa Rais," anachambua mchumi huyo na kubainisha madhara zaidi ya ufisadi na matumizi mabaya ya mali za umma akisema:
"Asilimia 30 ya fedha za serikali huibwa na wajanja wachache. Ukiwa na mapapa ya ufisadi yanamzunguka Rais, naye anaogelea nayo, huwezi kuwaletea maendeleo wananchi."
Katika wizi huo wa fedha za serikali, Prof. Lipumba anafichua kwamba Shilingi trilioni 11.8 zimeibiwa ndani ya miaka mitano ya utawala wa Kikwete, fedha anazosema zingetosha kujenga shule bora za kata zenye maabara, maktaba na walimu; hivyo kutoa elimu bora kwa watoto wa masikini.
Pamoja na kuunda serikali ya umoja, Prof Lipumba anaahidi kuondoa sheria zote kandamizaji, lengo likiwa kuhakikisha utoaji haki sawa kwa kila raia.
Analitaja tatizo jingine la uongozi wa taifa kuwa ni viongozi wa CCM kutanguliza maslahi ya kisiasa zaidi kuliko ya taifa ambapo anatoa mfano wa Uwanja wa Ndege wa Songwe unaoendelea kujengwa kwamba unasuasua kutokana na dhamira ya baadhi ya viongozi ndani ya chama hicho kuua nguvu ya kisiasa ya Prof Mark Mwandosya mkoani Mbeya.
"Uwanja wa Ndege wa Mbeya haukamiliki kwa sababu ya njama za kumkomoa Prof. Mwandosya kwa sababu ndiye aliyeanzisha ujenzi wake. Wametanguliza maslahi ya kisiasa kuliko ya taifa," anasema Prof Lipumba.
Sera ya CUF kuhusu elimu ilikoga nyonyo za wasikilizaji waliohudhuria kampeni hizo za mgombea wao urais, hususani pale Prof. Lipumba anapotamka kwamba serikali yake itatoa elimu bure kwa watoto wote nchini, kuanzia shule ya awali hadi chuo kikuu.
Anaiponda sera ya elimu ya CCM; hususan kuhusu shule za sekondari za kata akisema zinajenga matabaka nchini na kuyataja kuwa ni lile la watoto wa matajiri na viongozi ambao watoto wao husoma kwenye shule za English Medium, au nje ya nchi kama vile Kenya, Uganda na Ulaya.
Mgombea huyo analitaja tabaka la pili kuwa ni lile la Watanzania masikini ambao watoto wao ndio hao wenye kusoma kwenye shule hizo za sekondari za kata.
"Sekondari hizi za kata haziwezi kutuvusha. Ni sekondari za watoto wa masikini - hazina maabara, walimu wala maktaba. Leo watoto wa masikini hawapati fursa ya kusoma katika shule zenye walimu bora, maabara na maktaba," anasema Prof. Lipumba huku akiwashangaa viongozi wa CCM kudai haiwezekani wakati wao, pamoja na wazazi wao wakati ule kuwa masikini lakini walisomeshwa bure hadi chuo kikuu na hata kupelekwa nje ya nchi kwa elimu ya juu zaidi.
Pamoja na kutoa elimu bure kwa watoto wote nchini, katika ilani yake wanayoita "Dira ya Mabadiliko au Vision for Change," CUF wanakusudia vile vile kutoa matibabu bure kwa wananchi wote, kuboresha afya ya mama wajawazito ili kupunguza vifo vyao vinavyozidi kuongezeka nchini kiasi cha kutoyafikia malengo ya milenia.
Prof. Lipumba alikuwa mgombea wa kwanza hadi sasa aliyezungumzia hifadhi ya jamii kwa wazee nchi ambapo alibainisha kuwa itawahusu wazee wote pasipo kujali kama aliwahi kuwa mwajiriwa au la.
Hoja kuhusu umasikini wa Watanzania ilionekana kuvuta hisia kali zaidi za wasikilizaji wake; hususan vijana kutokana na chama hicho kutumia vigezo vinavyojibainisha zaidi katika maisha yao ya kila siku.
Miongoni mwa vigezo vilivyotumika kwenye mikutano ya kampeni za mgombea huyo ni pamoja na makazi na chakula duni, barabara mbovu, elimu duni na kuongezeka kwa ujinga, ambapo viongozi hao wa CUF wanabainisha kuwa inajidhihirisha kwa wananchi kugubikwa na imani potofu zinazojidhihirisha hivi sasa kwa wengi wao kukimbilia kwa waganga kwa ajili ya kupata utajiri, ajira, uongozi na tiba.
"Maisha bora yaliyoahidiwa na CCM yako wapi? Wakati Kikwete anaingia madarakani 2005, bei ya sukari ilikuwa Shilingi 600, leo hii mnanunua shilingi ngapi?", aliuhoji umati uliomsikiliza ambao nao ulijibu kwa sauti: "Elfu mbili..!"
kisha naye huwachoma zaidi akisema,
Prof Lipumba aliwagusa zaidi aliposema: "Bakora za maisha magumu za CCM hazibagui, zinatuchapa wote, CCM na wasio CCM".
Gwiji huyo wa uchumi anaichambua CCM kati kigezo cha umasikini akisema: "Ukitumia kuanzia shilingi 570 kwa siku, wewe sio masikini. Hiki ndio kigezo cha Serikali ya CCM, lakini pamoja na kigezo chao hicho cha chini bado masikini wameongezeka kwa milioni 1.5."
Hata hivyo, ni kwa jinsi gani basi serikali ya Prof. Lipumba itaweza kuwaondoa Watanzania kutoka kwenye umasikini huo uliokithiri, kutoa elimu na afya bure, anasema:
"Tatizo la CCM ni kwamba serikali haikusanyi kodi sawa sawa. Kwa mfano kutoka kwenye wawekezaji wakubwa wakiwemo makampuni ya madini na mafuta, tutaondoa misamaha ya kodi ikiwemo kwenye madini. Hivi sasa serikali inakusanya asilimia 15 tu ya pato la taifa, CUF imelenga kukusanya asilimia 22 hadi 25 ya pato la taifa. Katika madini tunataka serikali ichukue angalau Shilingi 300 katika kila Shilingi 1,000 na sio mrahaba wa asilimia tatu tu kama ilivyo sasa."
Prof. Lipumba hakubaliani na kigezo cha machinga kujumuishwa kwenye ongezeko la ajira kama walivyofanya CCM. Kwamba ajira 1,300 zilizozalishwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita zimo kwenye sekta binafsi ambayo ni pamoja nawauza karanga, maji na mama lishe.
"Serikali ya CUF itahakikisha tunazalisha umeme kwa kutumia vyanzo mbali mbali vilivyopo ikiwemo makaa ya mawe ya Kiwira. Tanzania haina umeme wa uhakika, inazalisha Kilowati 770 tu. Tatizo viongozi hutumia mwanya wa matatizo ya umeme nchini kujitajirisha. Ni lazima tuwe na umeme wa uhakika ili kukuza sekta ya viwanda," anasema Prof Lipumba na kutumia mfano wa kiwanda kilichokufa cha Zana za Kilimo Mbeya akisema:
"Kiwanda cha Zana za Kilimo cha Mbeya kikifufuliwa, kinaweza kuajiri wafanyakazi 400 ambao watalipwa mshahara wa shilingi laki tatu kila mwezi, kwa mfano. Hii ina maana kuwa Shilingi milioni 120 zitaingia kwenye mzunguko wa Jiji la Mbeya, hapa mafundi seremala watauza fanicha, mafundi nguo watashona nguo mpya sio kuweka viraka nguo zilizochakaa, mama lishe watapata wateja, kwa hiyo zaidi ya watu 2,000 watanufaika," kisha anatoa takwimu za kitaifa akisema
"Leo hii viwanda nchini vimeajiri wafanyakazi wasiozidi 92,000 tu. Huwezi kukuza uchumi katika mazingira haya."
Pamoja na kaulimbiu ya CUF ‘Tanzania kwanza vyama baadaye' kuwavutia wengi mkoani Mbeya, bado wananchi wanashindwa kuwaelewa viongozi wa vyama vya upinzani nchini kwa kushindwa kuelewana na kuwa na mkakati mmoja, hawawaelewi pale wanapopingana na kukashifiana, hatua wanayoibainisha kuwa inawadhoofisha na kuimarisha CCM zaidi
BAADA YA KUSEMA HAYO LEO NIMESOMA POST MOJA KTK GAZETI LA RAIA MWEMA NA KWA KWELI NIMEVUTIWA SANA NA MGOMBEA URAIS WA CUF PROFESA LIPUMBA NA NAWAOMBA NA NYINYI HEMBU SOMENI SERA ZA CHAMA HICHI CHA CUF HALAFU TUJADILI TUONE KAMA KUNA CHAMA KINGINE CHENYE SERA BORA ZAIDI YA HIKI ASANTENI:
Prof. Lipumba: Tanzania kwanza vyama baadaye
Felix Mwakyembe
Septemba 22, 2010
KUNA tofauti kubwa kati ya mikutano ya kampeni za mgombea nafasi ya urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete na mgombea wa nafasi hiyo kupitia Civic United Front (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba.
Wakati ile ya mgombea wa CCM huchukua sura ya tamasha la muziki wa kizazi kipya (maarufu kama fiesta) kutokana na muda mwingi kutumika kwa burudani za wasanii mbalimbali maarufu kwa wakati huu hapa nchini, ile ya CUF inachukua sura ya mihadhara ya kisomi zaidi, ikiwa imejaa hoja nzito za kitaifa kuliko burudani.
Kutokana na sura hizo mbili tofauti za mikutano ya kampeni za wagombea hao, baadhi ya wafuatiliaji wa kampeni jijini Mbeya wanaamini kuwa ndiyo sababu vile vile ya tofauti ya idadi ya wasikiliza katika mikutano ya wagombea hao ambapo Kikwete alionekana kukusanya umati mkubwa wakati alipofanya kampeni zake mkoani Mbeya kuanzia mwishoni mwa mwezi Agosti hadi mwanzoni mwa Septemba tofauti na aliopata Prof. Lipumba aliyekuwepo jijini humo siku ya Jumamosi na Jumapili.
Wananchi waliohudhuria mikutano ya Prof. Lipumba walikuwa wachache lakini kila aliyepata hiyo bahati alionekana wazi kushiba hoja za mchumi huyo aliyebobea hapa nchini, na kama uwezo wa mgombea ndio kingekuwa kigezo kikuu cha wapiga kura, hapana shaka katika wagombea hao wawili waliopita jijini hapo hadi sasa, basi wa CUF angeibuka kidedea mkoani Mbeya .
"Kama kuzungumza, Prof. Lipumba anajenga hoja nzito sana. Sijui tu mtazamo wa wananchi na hicho chama, lakini kwa kweli hoja zake ni nzito sana," anasema mkazi mmoja wa Jiji la Mbeya.
Miongoni mwa hoja zilizowakuna zaidi waliohudhuria mikutano ya Prof. Lipumba, ni pamoja na ile ya kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa ambapo msimamo wake wa kuwaingiza kwenye serikali yake Watanzania wenye uwezo na waadilifu pasipo kujali itikadi za vyama ulipokelewa vizuri na wakazi wa mkoa huo.
Katika hoja hiyo Prof. Lipumba anasema: "Nitaunda serikali ya umoja wa kitaifa. Nitatumia watu waadilifu walioko kwenye vyama mbalimbali vya siasa. Sio kwamba walioko CCM wote ni mafisadi, wapo Watanzania wazuri tu kule, na wengine hawana vyama lakini wanashindwa kuingia kwenye uongozi kutokana na sheria zetu zilizopo."
Anasema umasikini unaowakabili Watanzania unatokana na viongozi waliopo madarakani kukosa uadilifu ambapo katika hilo anabainisha akisema: "Ikiwa mtu anakataa serikali ya umoja wa kitaifa, basi, huyo ni ajuza; hajui analolifanya au ana nia mbaya na Tanzania."
Imani ya Prof. Lipumba kuhusu serikali ya umoja wa kitaifa inaenda sambamba na kaulimbiu ya chama hicho isemayo "Tanzania Kwanza Vyama Baadaye" ambayo nayo inaoana na ile ya "Mbeya Kwanza Vyama Baadaye," na anasisitiza akisema iwapo Zanzibar wameweza kwa nini Tanzania Bara wasiweze?
Mgombea huyo wa CUF anaenda mbali zaidi ambapo anasema kukosekana kwa uadilifu katika serikali ya CCM ndiko kulikozaa sera mbili kuu za chama hicho anazozitaja kuwa ni ufisadi na matumizi mabaya ya mali za umma.
"CCM inatekeleza sera mbili, ufisadi na matumizi mabaya ya mali ya umma. Kikwete anaongoza kwa matumizi mabaya. Ni kiguu na njia, hatulii. Ile ndege ya kifahari ya serikali anayotumia inatumia dola za Kimarekani elfu sita kwa saa kila inaporuka, posho yake, Mama Salma, na wapambe.
Mama Salma naye ana safari zake utadhani ni Makamo wa Rais," anachambua mchumi huyo na kubainisha madhara zaidi ya ufisadi na matumizi mabaya ya mali za umma akisema:
"Asilimia 30 ya fedha za serikali huibwa na wajanja wachache. Ukiwa na mapapa ya ufisadi yanamzunguka Rais, naye anaogelea nayo, huwezi kuwaletea maendeleo wananchi."
Katika wizi huo wa fedha za serikali, Prof. Lipumba anafichua kwamba Shilingi trilioni 11.8 zimeibiwa ndani ya miaka mitano ya utawala wa Kikwete, fedha anazosema zingetosha kujenga shule bora za kata zenye maabara, maktaba na walimu; hivyo kutoa elimu bora kwa watoto wa masikini.
Pamoja na kuunda serikali ya umoja, Prof Lipumba anaahidi kuondoa sheria zote kandamizaji, lengo likiwa kuhakikisha utoaji haki sawa kwa kila raia.
Analitaja tatizo jingine la uongozi wa taifa kuwa ni viongozi wa CCM kutanguliza maslahi ya kisiasa zaidi kuliko ya taifa ambapo anatoa mfano wa Uwanja wa Ndege wa Songwe unaoendelea kujengwa kwamba unasuasua kutokana na dhamira ya baadhi ya viongozi ndani ya chama hicho kuua nguvu ya kisiasa ya Prof Mark Mwandosya mkoani Mbeya.
"Uwanja wa Ndege wa Mbeya haukamiliki kwa sababu ya njama za kumkomoa Prof. Mwandosya kwa sababu ndiye aliyeanzisha ujenzi wake. Wametanguliza maslahi ya kisiasa kuliko ya taifa," anasema Prof Lipumba.
Sera ya CUF kuhusu elimu ilikoga nyonyo za wasikilizaji waliohudhuria kampeni hizo za mgombea wao urais, hususani pale Prof. Lipumba anapotamka kwamba serikali yake itatoa elimu bure kwa watoto wote nchini, kuanzia shule ya awali hadi chuo kikuu.
Anaiponda sera ya elimu ya CCM; hususan kuhusu shule za sekondari za kata akisema zinajenga matabaka nchini na kuyataja kuwa ni lile la watoto wa matajiri na viongozi ambao watoto wao husoma kwenye shule za English Medium, au nje ya nchi kama vile Kenya, Uganda na Ulaya.
Mgombea huyo analitaja tabaka la pili kuwa ni lile la Watanzania masikini ambao watoto wao ndio hao wenye kusoma kwenye shule hizo za sekondari za kata.
"Sekondari hizi za kata haziwezi kutuvusha. Ni sekondari za watoto wa masikini - hazina maabara, walimu wala maktaba. Leo watoto wa masikini hawapati fursa ya kusoma katika shule zenye walimu bora, maabara na maktaba," anasema Prof. Lipumba huku akiwashangaa viongozi wa CCM kudai haiwezekani wakati wao, pamoja na wazazi wao wakati ule kuwa masikini lakini walisomeshwa bure hadi chuo kikuu na hata kupelekwa nje ya nchi kwa elimu ya juu zaidi.
Pamoja na kutoa elimu bure kwa watoto wote nchini, katika ilani yake wanayoita "Dira ya Mabadiliko au Vision for Change," CUF wanakusudia vile vile kutoa matibabu bure kwa wananchi wote, kuboresha afya ya mama wajawazito ili kupunguza vifo vyao vinavyozidi kuongezeka nchini kiasi cha kutoyafikia malengo ya milenia.
Prof. Lipumba alikuwa mgombea wa kwanza hadi sasa aliyezungumzia hifadhi ya jamii kwa wazee nchi ambapo alibainisha kuwa itawahusu wazee wote pasipo kujali kama aliwahi kuwa mwajiriwa au la.
Hoja kuhusu umasikini wa Watanzania ilionekana kuvuta hisia kali zaidi za wasikilizaji wake; hususan vijana kutokana na chama hicho kutumia vigezo vinavyojibainisha zaidi katika maisha yao ya kila siku.
Miongoni mwa vigezo vilivyotumika kwenye mikutano ya kampeni za mgombea huyo ni pamoja na makazi na chakula duni, barabara mbovu, elimu duni na kuongezeka kwa ujinga, ambapo viongozi hao wa CUF wanabainisha kuwa inajidhihirisha kwa wananchi kugubikwa na imani potofu zinazojidhihirisha hivi sasa kwa wengi wao kukimbilia kwa waganga kwa ajili ya kupata utajiri, ajira, uongozi na tiba.
"Maisha bora yaliyoahidiwa na CCM yako wapi? Wakati Kikwete anaingia madarakani 2005, bei ya sukari ilikuwa Shilingi 600, leo hii mnanunua shilingi ngapi?", aliuhoji umati uliomsikiliza ambao nao ulijibu kwa sauti: "Elfu mbili..!"
kisha naye huwachoma zaidi akisema,
Prof Lipumba aliwagusa zaidi aliposema: "Bakora za maisha magumu za CCM hazibagui, zinatuchapa wote, CCM na wasio CCM".
Gwiji huyo wa uchumi anaichambua CCM kati kigezo cha umasikini akisema: "Ukitumia kuanzia shilingi 570 kwa siku, wewe sio masikini. Hiki ndio kigezo cha Serikali ya CCM, lakini pamoja na kigezo chao hicho cha chini bado masikini wameongezeka kwa milioni 1.5."
Hata hivyo, ni kwa jinsi gani basi serikali ya Prof. Lipumba itaweza kuwaondoa Watanzania kutoka kwenye umasikini huo uliokithiri, kutoa elimu na afya bure, anasema:
"Tatizo la CCM ni kwamba serikali haikusanyi kodi sawa sawa. Kwa mfano kutoka kwenye wawekezaji wakubwa wakiwemo makampuni ya madini na mafuta, tutaondoa misamaha ya kodi ikiwemo kwenye madini. Hivi sasa serikali inakusanya asilimia 15 tu ya pato la taifa, CUF imelenga kukusanya asilimia 22 hadi 25 ya pato la taifa. Katika madini tunataka serikali ichukue angalau Shilingi 300 katika kila Shilingi 1,000 na sio mrahaba wa asilimia tatu tu kama ilivyo sasa."
Prof. Lipumba hakubaliani na kigezo cha machinga kujumuishwa kwenye ongezeko la ajira kama walivyofanya CCM. Kwamba ajira 1,300 zilizozalishwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita zimo kwenye sekta binafsi ambayo ni pamoja nawauza karanga, maji na mama lishe.
"Serikali ya CUF itahakikisha tunazalisha umeme kwa kutumia vyanzo mbali mbali vilivyopo ikiwemo makaa ya mawe ya Kiwira. Tanzania haina umeme wa uhakika, inazalisha Kilowati 770 tu. Tatizo viongozi hutumia mwanya wa matatizo ya umeme nchini kujitajirisha. Ni lazima tuwe na umeme wa uhakika ili kukuza sekta ya viwanda," anasema Prof Lipumba na kutumia mfano wa kiwanda kilichokufa cha Zana za Kilimo Mbeya akisema:
"Kiwanda cha Zana za Kilimo cha Mbeya kikifufuliwa, kinaweza kuajiri wafanyakazi 400 ambao watalipwa mshahara wa shilingi laki tatu kila mwezi, kwa mfano. Hii ina maana kuwa Shilingi milioni 120 zitaingia kwenye mzunguko wa Jiji la Mbeya, hapa mafundi seremala watauza fanicha, mafundi nguo watashona nguo mpya sio kuweka viraka nguo zilizochakaa, mama lishe watapata wateja, kwa hiyo zaidi ya watu 2,000 watanufaika," kisha anatoa takwimu za kitaifa akisema
"Leo hii viwanda nchini vimeajiri wafanyakazi wasiozidi 92,000 tu. Huwezi kukuza uchumi katika mazingira haya."
Pamoja na kaulimbiu ya CUF ‘Tanzania kwanza vyama baadaye' kuwavutia wengi mkoani Mbeya, bado wananchi wanashindwa kuwaelewa viongozi wa vyama vya upinzani nchini kwa kushindwa kuelewana na kuwa na mkakati mmoja, hawawaelewi pale wanapopingana na kukashifiana, hatua wanayoibainisha kuwa inawadhoofisha na kuimarisha CCM zaidi