Uongozi wa Chama ni kama ndoa ya Kiislam, ukiamua kuacha uongozi ni kama kuacha mke kwa talaka moja, siku ukijisikia utakuwa uko huru kumrejelea bila kipingamizi chochote, hivyo Lipumba alitoa talaka moja tuu, yuko huru kumrejelea mkewe uongozi wa CUF! .
Na hata ukiacha mke kwa talaka tatu bado pia unaweza kumrejelea kwa sharti kwamba kwanza aolewe na mtu mwingine, aachike ndipo na wewe umuoe tena! .
Kama talaka ya Lipumba ni talaka tatu, then ajiunge Chadema, ajitoe, arejee CUF.
Kwa bahati nzuri sana, Lipumba hana shughuli nyingine yoyote ya kufanya zaidi ya uongozi wa CUF, ila pia CUF, haina mtu mwingine yoyote ,mwenye long experience ya uzoefu wa muda mrefu wa uenyekiti wa CUF, kiasi kwamba yeye na Maalim ndio wagombea pekee wa kudumu wa urais kwa CUF kwenye Chaguzi zote ilipokuja uchaguzi wa 2015 CUF ilimuunga mkono mgombea wa UKAWA, Lipumba akaamua kususa na kutoa talaka! .
CUF mrudishieni Lipumba mkewe Uenyekiti wa CUF! .
Pasco