Uchaguzi 2020 Prof. Kabudi bila mbeleko Kilosa ubunge mgumu kwake. Warabu wa Kilosa wanamzidi kutamka majina ya vijiji vya Kilosa

Mpango buhigwe
Ndalichako kasulu
Kilosa kabudi
Halafu wote watatu hawajui kujieleza mbele ya wananchi wasio na elimu(Majority),wakianza kuleta takwimu zao zile za ki PH.d kwny mikutano ya hadhara wananzengo watawapa majibu yao.
 
 
Kwani Palamagamba ni mgogo, mluguru au mkaguru ?
 
Halafu wote watatu hawajui kujieleza mbele ya wananchi wasio na elimu(Majority),wakianza kuleta takwimu zao zile za ki PH.d kwny mikutano ya hadhara wananzengo watawapa majibu yao.
Mwenzao Tulia ame invest muda sana ili kutambulika na wana Mbeya, japo sio guarantee atashinda.

Kabudi kushinda tu kura ya maoni ndani ya itakuwa shida hana ushawishi Kilosa wananchi wenyewe wameshangazwa kama ni wa kwao, alitumia nguvu kweli kujifanya mwenyeji.

CCM ata wakikata wamuweke yeye kwa lazima kama mgombea chances hilo jimbo litaenda upinzani. Mtu pekee anae muelewa Kabudi ni Magufuli inawezekana kweli anamfanyia kazi nzuri na hilo ndio la msingi boss afurahi.

Ila kwa mtazamo wa wengi Kabudi ni kituko hana lugha ya ushawishi. Kama Boss wake amefurahishwa sana na kazi yake amteue tena, kumlazimishia jimbo kama uchaguzi ni fair ashindi.
 
Jimbo litaenda upinzani wewe ndio unayetangaza??
 
Jimbo litaenda upinzani wewe ndio unayetangaza??
Aitokuwa mara ya kwanza CCM wanapolazimisha kutoa popular local candidates na kulazimisha mambo.

Kabudi ajulikani Kilosa mwanasiasa ni product na brand awareness ni muhimu kwa wapiga kura, hiko ndio kitu Tulia amekuwa akifanya kujulikana na wapiga kura yeye ni nani.

Kwenda kupeleka mtu ambae kwanza hajui porojo wala kuongea na watu wa chini kwa staha uitaji kuwa na kampuni ya marketing kubwa duniani kama Saatchi & Saatchi kujua mgombea wa upinzani anaejulikana na Kabudi nani atashinda Kilosa.

I am a betting
 
Katika siasa ya mambo ya nje tumekuwa tukijipendekeza mno kwa Marekani na Israel
Angalia kura za Tanzania huko Umoja wa Mataifa
Halafu eti tunawakataa mabeberu!
 
Kabudi anachukua jimbo bila tashwishwi wala kupepesa macho! Wananchi wenyewe kama ndio wale niliowaona kwenye mkutano na mkuu nimegundua Tanzania bado sana
 
Kwani lazima agombee Morogoro kilosa!!!
Kwanini asigombee jimbo la Chato kama Mkulu anampenda. Asituletee mikosi tulonayo Morogoro inatosha.
 
Mnaupiga vita ukabila na ukanda huku mkiuendekeza. Wenje alikuwa na udugu gani wakati anagombea hapa Nyamagana?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…