makoye2009
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,638
- 1,218
Mimi si mwana-CUF lakini leo nimemsikliza Prof. Lipumba wakti akihojiwa na Charles Hilary wa BBC Swahili hii jioni nimefurahishwa sana na jinsi jamaa alivyokuwa anajibu Maswali ya Charles na hoja za Wasikilizaji kwa uhakika na ufahamu mkubwa kuhusiana na mgogoro wa Kiuchumi unaozikumba nchi za Jumuia ya Ulaya. Huyu jamaa yuko juu na ndiyo maana IMF wamemchukua na alikuwa akihojiwa tokea Washington DC.
Nina hakika kabisa kama Prof. Lipumba angelikuwa pale BOT uchumi wetu Tanzania ungelikuwa juu. Lakini kwa vile nchi hii imeshapoteza mwelekeo kutokana na utawala kwa kihuni wa CCM watu kama kina Lipumba wanapuuzwa simply because wako upinzani! Huu ni uhuni tu! CCM wameshindwa kujifunza kwa Nchi kama South Africa,USA, Uingereza na sasa Zambia kwa kutaja chache,kwamba Serikali zao zimeundwa kwa mchanganyiko wa Chama Tawala na Vyama pinzani kwa kujua umuhimu wa Uzalendo na kwamba nchi si ya Chama kilichoshinda kwa kura hata kama ni zaidi ya 50pc.
Tunamshauri Kiwete aunde serikali ya mseto haraka sana kwa Tanzania Bara na awateue watu kama kina Prof. Lipumba kuwa Governor wa Benki Kuu badala ya Prof. ndullu anayeonekana kupwaya kwenye nafasi hiyo au kuwa Waziri wa Fedha badala ya Kibuyu Mustafa Mkullo. Pia kuna vijana matata wa CDM ambao wana ufahamu mkubwa sana wa maswala ya Kisiasa na Kiuchumi ambao kama Kiwete atawatumia ataondoka Madarakani akiwa amejijengea Legacy iliyotukuka!
Siyo jambo la siri kuwa Prof.Lipumba yuko juu kwa mbali sana akilinganishwa na Prof. Ndulu au Mkulloi Hapa ni swala la kuweka uzalendo mbele na si ushabiki wa kisiasa wa kijinga unaoendeshwa na wanamagamba wa kufikiri kuwa Wapinzani ni wahaini ati wanataka kuipindua serikali iliyoko madarakani. Hayo nimmawazo ya ulimbukeni wa siasa, CCM lazima wakili kuwa nchi imewashinda na si vinginevyo. Lakini kwa vile sikio la kufa halisilkii dawa CCM acha wakomae na upumbavu wao,kwa sasa hawana siku nyingi za kuwemo madarakani maana ytayari taa nyekundu inayoonyesha EXIT inapiga indicator!!
Nina hakika kabisa kama Prof. Lipumba angelikuwa pale BOT uchumi wetu Tanzania ungelikuwa juu. Lakini kwa vile nchi hii imeshapoteza mwelekeo kutokana na utawala kwa kihuni wa CCM watu kama kina Lipumba wanapuuzwa simply because wako upinzani! Huu ni uhuni tu! CCM wameshindwa kujifunza kwa Nchi kama South Africa,USA, Uingereza na sasa Zambia kwa kutaja chache,kwamba Serikali zao zimeundwa kwa mchanganyiko wa Chama Tawala na Vyama pinzani kwa kujua umuhimu wa Uzalendo na kwamba nchi si ya Chama kilichoshinda kwa kura hata kama ni zaidi ya 50pc.
Tunamshauri Kiwete aunde serikali ya mseto haraka sana kwa Tanzania Bara na awateue watu kama kina Prof. Lipumba kuwa Governor wa Benki Kuu badala ya Prof. ndullu anayeonekana kupwaya kwenye nafasi hiyo au kuwa Waziri wa Fedha badala ya Kibuyu Mustafa Mkullo. Pia kuna vijana matata wa CDM ambao wana ufahamu mkubwa sana wa maswala ya Kisiasa na Kiuchumi ambao kama Kiwete atawatumia ataondoka Madarakani akiwa amejijengea Legacy iliyotukuka!
Siyo jambo la siri kuwa Prof.Lipumba yuko juu kwa mbali sana akilinganishwa na Prof. Ndulu au Mkulloi Hapa ni swala la kuweka uzalendo mbele na si ushabiki wa kisiasa wa kijinga unaoendeshwa na wanamagamba wa kufikiri kuwa Wapinzani ni wahaini ati wanataka kuipindua serikali iliyoko madarakani. Hayo nimmawazo ya ulimbukeni wa siasa, CCM lazima wakili kuwa nchi imewashinda na si vinginevyo. Lakini kwa vile sikio la kufa halisilkii dawa CCM acha wakomae na upumbavu wao,kwa sasa hawana siku nyingi za kuwemo madarakani maana ytayari taa nyekundu inayoonyesha EXIT inapiga indicator!!