Prof. Baregu ndani ya kipindi cha kipima joto ITV

Prof. Baregu ndani ya kipindi cha kipima joto ITV

Ilianza UKAWA mara tanzania kwanza.................... sasa ni ex-tume members!

picha inaendelea..............
 
prof baregu akichambua rasmu ya katiba ambayo yeye alikuwa ni mjumbe wa katiba. Kasema viongozi wa tz ni wanafiki, watu wanaopenda kujipendekza na kuacha uongo utawale. Kasema kinachofanyika kwa sasa ni kuchochea wananchi waichukie tume. Kama machafuko yatakuja apa nchini kasema wale wanaopinga maoni ya wananchi basi watabeba lawama hii chama tawala na serikali yake. Kila mtu anataka maoni yake yawemo kwenye katiba, lakini ata yeye aliyekuwa kwenye tume, maoni yake hayakuingizwa baada ya mchakato mzito. Mwisho kasema bunge maalumu la katiba limeenda kuidhinisha matakwa ya wananchi na si kutengua kile walichopendekeza waananchi. Nimetafuta line ili nimuulize prof baregu, je mh. Dr mwakyembe na prof shivji wako sawa kulingana na taaluma yao kwamba wanapendekeza serikali 2?
Wanasheria kama warioba na Baregu sijui wanafanyiwa na nani dessertation na thesis zao. Kama hata hawajui sampling kiasi cha kusema hao waliotaka serikali 3 wanawakilisha watanzania sijui tusemeje. Kama nia yao ni kuwasaidia kina jussa na seif kuvunja taifa wawe wazi. Tunajua zanzibar nani walichukua mashoka na mapanga kujikomboa na utumwa. Kwenye bunge la katiba tumewaona wakitoa msimamo wao kwa hasira na jazba kubwa kuwapinga wale wanaotaka kuvunja muungano. Sasa kama unafikiri watu hao ni wachache znz ujue unafanya makosa makubwa.
 
Pia kasema kwa sasa tunaishi(nahisi alimaanisha Viongozi) KINAFIKI,KWA KUOGOPANA NA KWA UZEMBE(yaani yale tu/wanayokubaliana hawayatekelezi na hamna anayemuuliza mwingine)...ndio maana katiba ya Zanzibar 'ilivunja' katiba ya Muungano lakini nani kati ya viongozi wa jamhuri ya Muungano ambao wameapa kuitetea na kuilinda katiba ya Muungano na Muungano wenyewe alosema na/au kufanya chochote?..(not a direct quotation)
 
Hata mie nimestuka????

Napenda kutoa taarifa hii rasmi
kwa wana JF wote na Mods kwa
ujumla kuwa tumeondokewa na
mwanachama mwenzetu ambaye
alijiunga na Jukwaaa hili tangu
Octoba 2010.
Alikuwa anatumia ID ya Kanjunju .
Hivyo tunaomba tumwombee.
Alifariki dunia katika hospitali ya
Mkoa Ruvuma wiki iliyopita.
RIP Kanjunju.
 
Wanasheria kama warioba na Baregu sijui wanafanyiwa na nani dessertation na thesis zao. Kama hata hawajui sampling kiasi cha kusema hao waliotaka serikali 3 wanawakilisha watanzania sijui tusemeje. Kama nia yao ni kuwasaidia kina jussa na seif kuvunja taifa wawe wazi. Tunajua zanzibar nani walichukua mashoka na mapanga kujikomboa na utumwa. Kwenye bunge la katiba tumewaona wakitoa msimamo wao kwa hasira na jazba kubwa kuwapinga wale wanaotaka kuvunja muungano. Sasa kama unafikiri watu hao ni wachache znz ujue unafanya makosa makubwa.

nani kakwambia baregu ni mwanasheria...tatixo letu ni fikra za kitumwa mlizo nazo..kutumia midomo yenu kusema mlioambiwa badala kutumia vichwa na akili zenu kuelezea mnayoaamini..kujifanya wasomi na watalaam kumbe elimu zetu za mpakazo..elezea unachoamini kwa ushahidi wa kitafiti siyo kutema mapovu ya ----- wa wanaotawala fikra zako...uhuru wako ndio thamani yako,,,lakini utumwa wako ndio hatma yako
 
Mkuu tatizo la Prof.Baregu ni kwamba hajui kiujikomba kwa watawala.

hiyo ndiyo thamani ya binadamu mwenye fikra huru....na utumwa unaondekezwa na CCM na watu wake...wao wanaamini kat7ka kufuata mawazo ya mwenyekiti hata kama hayana mantiki...wana CCM wanaishi katika utumwa uliopindukia kwa sababu ya kusikiliza sana matumbo yao badala ya utu na thamani ya ubinadamu wao....kwao taifa si kipaumbele isipokuwa matumbo na tamaa zao za mali
 
HUYU BAREGU ni miongoni mwa wale MANABII WA UONGO.
na kwa sababu SIKU ZOTE KWELI ITASIMAMA.....
Nina hakika kabisa BAREGU NA MANABII wenzake WATAAMGUKA..... ANGUKO KUUU.
Hello hello TANZANIAAAAAAAAAAÀAAAAAAAA
 
Ukitaka uone uwezo wa akili wa huyu Professor unapotea ghafra basi ajiunge na CCM, hutaamini kwamba ni yeye. CCM is the cancer of the brain of this country! ni lazima tuiondoe hii cancer katika vichwa vya wasomi wetu.
 
HUYU BAREGU ni miongoni mwa wale MANABII WA UONGO.
na kwa sababu SIKU ZOTE KWELI ITASIMAMA.....
Nina hakika kabisa BAREGU NA MANABII wenzake WATAAMGUKA..... ANGUKO KUUU.
Hello hello TANZANIAAAAAAAAAAÀAAAAAAAA

Nawewe unajiita GT? Duuuh, kazi ipo.
 
nani kakwambia baregu ni mwanasheria...tatixo letu ni fikra za kitumwa mlizo nazo..kutumia midomo yenu kusema mlioambiwa badala kutumia vichwa na akili zenu kuelezea mnayoaamini..kujifanya wasomi na watalaam kumbe elimu zetu za mpakazo..elezea unachoamini kwa ushahidi wa kitafiti siyo kutema mapovu ya ----- wa wanaotawala fikra zako...uhuru wako ndio thamani yako,,,lakini utumwa wako ndio hatma yako
Kama lissu mnachojua ni kutukana na kudhani mnayo monopoly kutoa mawazo. Sijui kwa nini mnajiamini na kua na hakika na mambo ya ovyo.
 
Back
Top Bottom