Prof. Baregu aula SAUT

Kwa taarifa yako Prof. Baregu haamini kama kuna MUNGU. He is totally a pagan. Hii inasikitisha sana. MUNGU amsaidie ili atambue ya kuwa yuko MUNGU aliyeziumba mbingu na nchi na vyote vilivyomo ndani yake.

Mkuu,
Nikushangae kidogo, kabla haujatuambia kama Prof. Baregu haamini kama kuna MUNGU ungemuuliza yeye ana amini nini badala yake?? Nakuona wewe kama muumini mzuri wa MUNGU aliyeletwa Africa na Wazungu, rudi nyuma kabala ya wazungu kuja, waafrika tulikuwa tunaamini nini?? hatukuwa tunapata tunachokiomba????hatukuwa tunasali???? Funguka kidogo kuhusu hicho unachokiamini (Mimi namuani MUNGU)
 
Le'njobe dhana ya Mungu na UUNGU , inatofauti sana , kwa jamii moja na nyingine, Ubora wa Mungu unategemea wewe unaabudu nini, ushenzi kwenye Imani unalalia kwenye dhana ya huyu si wetu, ama mwenzetu. ila kwa ujumla wake, Muhindu akiwatazama Waislamu ama Wakristo anaona viumbe dhalili, visivyomjua Mungu wa kweli, dhana hiyo anayo Muislamu dhidi ya dini za wengine vilevile Kwa Wakristo wao wanawaona wengine kuwa wanaabudu Miungu ilhali imeandikwa ...."mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu wenye wivu nawapatiliza wana maovu ya baba zao hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao na kuzishika amri zangu...."
sasa Ukiitazama Falsafa hiyo hakuna aliesahihi kumuhukumu mwenzake, maana hata yeye umzaniae amepotoka anakuona wewe , au sisi kuwa tuumepotoka kabisa.



Eeee bwana wewe ni kiboko! Umeweka facts zingu unanikuna mkuu!
 
Sio ajabu Baregu ni mlokole zaidi ya walokole wengine wanaojipigia debe, Mungu huangalia moyo wa mtu, hayumbishwi na mitazamo ya watu. Kama sivyo, Daudi asingepakwa mafuta kuwa Mfalme wa Israel mtoto mdogo asiyetarajiwa; Sauli (soma Paulo) asingekuwa mpiga debe maarufu wa Yesu Kristo hata kuwazidi mitume wengi waliotembea na Yesu miaka mitatu mfululizo. Mungu huwainua wangyone na kuwashusha wenye viburi. Nikodemus pamoja na kuwa msomi wa Kisamaria, alilazimika kutambua kwamba pamoja na kujulikana sana machoni pa watu kama mcha Mungu hakuwa na kitu, akalazimika kumwendeaYesu Usiku kula shule namna ya kuingia Mbinguni, Mungu akamkweza sana hata leo tunasoma habari zake. Yusufu ambaye hakutambuliwa na watu kama mwanafunzi wa Yesu akawa ndiye msaada wa kubeba msalaba wa Yesu kuelekea Golgotha wakati waliojulikana waliingia mitini.

Debe tupu mara zote haliachi kutika, Ngombale Mwiru amesemwa kwamba hana dini - ni makosa kusema hivyo, kwa sababu anayo dini ya mababu zake inayomtia nguvu kuwa mtu anayeishi na watu katika principles za imani ya dini yake. Neno zuri tuseme Baregu sio mkristo, hakuna dini ya kipagani. Waebrania waliwasema wasioamini kama wao "pagan", kama wachaga wanavyowaita "Kyasaka" wenzao na wanyakyusa wanavyowaita wenzao "Bhajanga", na wakinga huita "Bhanng'alu"..... Wapagani ni watu wasiokuwa na dini inayofanana na unayoiamini wewe. Kama ni kwa namna hiyo, basi tumtendee haki Baregu. Mbona ni mpole kupindukia na Mungu anapenda watu wapole? Ni mtu wa Mungu yule kama alivyo Mwislam, Mhindu, Myahudi, Mkristo, Budha na kadhalika.
 
Sio ajabu Baregu ni mlokole zaidi ya walokole wengine wanaojipigia debe, Mungu huangalia moyo wa mtu, hayumbishwi na mitazamo ya watu. Kama sivyo, Daudi asingepakwa mafuta kuwa Mfalme wa Israel mtoto mdogo asiyetarajiwa; Sauli (soma Paulo) asingekuwa mpiga debe maarufu wa Yesu Kristo hata kuwazidi mitume wengi waliotembea na Yesu miaka mitatu mfululizo. Mungu huwainua wangyone na kuwashusha wenye viburi. Nikodemus pamoja na kuwa msomi wa Kisamaria, alilazimika kutambua kwamba pamoja na kujulikana sana machoni pa watu kama mcha Mungu hakuwa na kitu, akalazimika kumwendeaYesu Usiku kula shule namna ya kuingia Mbinguni, Mungu akamkweza sana hata leo tunasoma habari zake. Yusufu ambaye hakutambuliwa na watu kama mwanafunzi wa Yesu akawa ndiye msaada wa kubeba msalaba wa Yesu kuelekea Golgotha wakati waliojulikana waliingia mitini.

Debe tupu mara zote haliachi kutika, Ngombale Mwiru amesemwa kwamba hana dini - ni makosa kusema hivyo, kwa sababu anayo dini ya mababu zake inayomtia nguvu kuwa mtu anayeishi na watu katika principles za imani ya dini yake. Neno zuri tuseme Baregu sio mkristo, hakuna dini ya kipagani. Waebrania waliwasema wasioamini kama wao "pagan", kama wachaga wanavyowaita "Kyasaka" wenzao na wanyakyusa wanavyowaita wenzao "Bhajanga", na wakinga huita "Bhanng'alu"..... Wapagani ni watu wasiokuwa na dini inayofanana na unayoiamini wewe. Kama ni kwa namna hiyo, basi tumtendee haki Baregu. Mbona ni mpole kupindukia na Mungu anapenda watu wapole? Ni mtu wa Mungu yule kama alivyo Mwislam, Mhindu, Myahudi, Mkristo, Budha na kadhalika.

Hizi ndo zinaitwa hekima za watu wa dunia hii ambazo zimepoteza wengi. Unataka kutuambia kuwa kama babu yako alikuwa mwizi au jambazi na wewe ungependa kuwa kama yeye? Kisa cha mababu zetu kuabudu mizimu na mashetani na kuendekeza uchawi ndo unataka na sisi tuendelee kuabudu hayo? A big NO. Kingunge alishasema hana dini wewe unataka kumlazimisha awe na dini ya mababu zake kama nayo haitaki je? Si anao uhuru wa kuchagua atakacho mwenyewe?
 
Hizi ndo zinaitwa hekima za watu wa dunia hii ambazo zimepoteza wengi. Unataka kutuambia kuwa kama babu yako alikuwa mwizi au jambazi na wewe ungependa kuwa kama yeye? Kisa cha mababu zetu kuabudu mizimu na mashetani na kuendekeza uchawi ndo unataka na sisi tuendelee kuabudu hayo? A big NO. Kingunge alishasema hana dini wewe unataka kumlazimisha awe na dini ya mababu zake kama nayo haitaki je? Si anao uhuru wa kuchagua atakacho mwenyewe?
Bwana Mazingira una haki kuamua kuelewa utakavyo, lakini bahati mbaya unavyonitaka nione kama ndivyo namaanisha sivyo. Sikia, dunia ipo tangu watu wawekwe na aliyewaweka. Watu huondoka lakini yenyewe dunia inaendelea kuwapo na wala wenye mawazo ya aina ako sio haba, usije ukajidanganya kwamba wewe ndie pioneer. Kingunge alikuwa anawaambia wasiotaka kufikiri kwa kina ili wakae walivyo. Ni vema ukitafuta kujua nini maana ya neno DINI, wala usimeze maneno kama unavyoyasikia. Dhana ya aina yako ndiyo JKN aliyowazodoa nayo waandishi wa habari wa Nairobi waliokuwa wanafikiria mambo juu juu kwa kuacha mambo aliyodhania yeye ni nyeti na wao hawakuona umuhimu. Waziwazi aliwaambia hawana akili kwa kuandika "Raisi Nyerer ampiga mkewe" badala ya kuandika mambo ya kimsingi yanayowasumbua watu ili kupata majibu yake. Aliwauliza kama Mr Kibuyu kule Musoma anampiga kila siku mkewe kwa jadi yao mbona hawaioni ni news ila Nyerere akimpiga mkewe kofi la mahaba tu inakuwa news ilhali naye anatoka jadi ileile ya Musoma.

Kingunge anapokuambia sina DINI alimaanisha haambatani na imani ya mtu yeyote, anazo itikadi zake na ndizo anaoziamini. Huwezi kutenganisha DINI na IMANI, maana mtu anatimiza matakwa ya dini yake kutegemea imani aliyo nayo katika dini yake hiyo. Kwa Kingunge Katiba ya chama chak huitumia kuapa badala ya Quran au Biblia kama wafanyavyo wengine. Halaaniwi kwa kufanya hivyo na anaheshimiwa na imani yake. Hiyo ndiyo dini yake. Hao babu zako uwasemao walikuwa wanamwabudu Mungu wao kwa mila zao, wazungu wamekuja na mila zao nasi tumeshawishiwa kupokea. Waliomba mvua ikaja, ni Mungu aliyewasikiliza kupitia mababu zao - kwa jina la mambabu zao, wazungu wanasema na Mungu kwa jina la Yesu, Waarabu kwa jina la Mohammad. Wote ni sawa tu, anayejua nani ni sahihi zaidi ni Mungu Peke yake, wengine tunawatumia kufikisha maombi yetu kwa Mungu yeye yule. Mungu ni tofauti na miungu. Mbona kila kabila lina jina la Mungu kwa namna walivyozoea kumwita tangu kale na hata tafsiri za Mungu anayesemwa kwenye misahafu mingine bado majinna ya asili ya Mungu hayafutwi??? Kyala, Mulungu, Nguluvi, Imana, mbona huelewi mkuu?

Naona unataka kupindisha dhana ya thread ya mwenzio aliyeianza. Msisitizo hapa ni kwamba KILA MTU ANA DINI YAKE, Upagani ni neno la dharau kama ilivyo KAFIR. Tuheshimiane katika imani tunazotofautiana ili tuishi kwa amani.
 
rudini kwenye mada....mambo ya dini yametokea wapi?? Wabongo yani ukiwaminya kidogo tu udini uko next door...lol
 
Baregu nenda baba, vijana Mwanza wanangojea kupata elimu kupitia kipaji chako, wewe ni mwanazuoni uliekomaa, kweli nakuombea kila raheli, na baraka zote ziwe juu yako.
waache UDSM waendelee kuhubiri siasa ktk elimu, waache wasambaratishe taaluma ya vijana wetu maana JK aliyataka, kuleta wanasiasa ktk nafasi za Utendaji, watu walijua baada ya kuona mr Redet anakabidhiwa kile chuo kama mtendaji mkuu.
 
I am happy for this BUT one question mbona Sengondo Mvungi ni mwanachama wa NCCR nauris aligombea na mara kwa mara amekuwa akitoa maoni kukosoa serikali lakini wanamwacha. Pia ni kwamba Tanzania kuna uhaba wa waadhiri kila nyanja mpaka wanaemploy foreigners kwa wingitoka India, Nigeria nk.
 
I am happy for this BUT one question mbona Sengondo Mvungi ni mwanachama wa NCCR nauris aligombea na mara kwa mara amekuwa akitoa maoni kukosoa serikali lakini wanamwacha. Pia ni kwamba Tanzania kuna uhaba wa waadhiri kila nyanja mpaka wanaemploy foreigners kwa wingitoka India, Nigeria nk.
wanalia timing afikishe sitini wamtoe nduki, na kama UDASSA Haitasimama kidete kweli elimu mlimani itaingia kaburini kabisa kabisa, maana bado ipo mahututi ICU
 
Uongozi wa UDSM wanaogopa kivuli chake na pia serikali katika kutaka kuwatisha waadhiri ambao wanakwenda kwenye upinzania ili wasiende kufanya hivyo. ila sheria ya kukataza siasa katika vyuo vikuu ni mbaya sana katika Taifa letu maana inawazuia watu makini kuwa na vision ya kuogoza hata Jk alianza chuo je iweje leo
 
Back
Top Bottom