Andindile
JF-Expert Member
- Mar 18, 2009
- 304
- 19
Hatimaye professor Mwesiga Baregu amesaini mkataba na chuo kikuu cha mtakatifu Augustino baada ya kuzuiliwa na serikali kufundisha chuo kikuu Dar. Habari za ajira yake zimethibitishwa na Mkuu wa idara ya Mawasiliano ya Umma wa SAUT Padri Dr. Joseph Matumaini kwenye gazeti la Tumaini letu toleo la Ijumaa, Feb. 19-25, 2010. Dr. Tumaini amesema kuwa ajira yake ni ya mkataba wa miaka mitatu na unaweza kupitiwa upya kila umalizikapo. Atakuwa anafundisha kampasi ya Dar es salaam na Mwanza. Natumai Prof. ataendeleza imani yake katika uhuru wa kitaaluma huko aliko na atakuwa kichocheo cha taaluma SAUT na ikizingatiwa kuwa SAUT kimekuwa chuo cha kwanza Tanzania kuanza kutoa shahada za uzamili na uzamivu katika tasnia ya habari na mawasiliano ambako uhuru wa kutoa habari ni jambo la msingi sana. Namtakia mafanikio mema Prof. Baregu