Pressure za kuoa na umri


Kuna jamaa zangu wengi wanaishi Boston, sijui ndio nyie!
 
Usivute mke toka Tz ...utajutra...labda utafute waliokuja US kusoma...jichanganye utapata mke...lakini usitumie mtu nauli...narudia utajutra na hao ma opportunist....
Mama nyumba kubwa heshima kwako..na hii ndo dilema tunayopata maana..kusema ukweli african american woman hawaoleki-wachache sana wenye attitude nzuri..na kuvuta mtu kutoka bongo huwezijua anaweza kuja kukujimbia tumeona haya(hasa wale mademu mawenge wenge na walimbukeni).. Ni kazi sana..na usr bachelor ndo unazidi kukolea..dah
 
it seems wewe ni domo zege maana kwa maelezo yako unasuuzia ulikuwa unatafuta maisha as if ulihama dunia kwenda sayari ya MARS kutoishi na watu usiowajua si sababu ya kutokuwa na mtu kwa umri wako.. huwa huna socialization activities hapi ulipo kwenye nyumba za ibada, kutembelea marafiki etc. BADILIKA kiongozi maisha si kazi/pesa tu
 
Kuwa na staha basi mwenzako yuko real na anaomba ushauri,...You to accept other people attitude and behavior.....
 
Nakupongeza sana kwa maamuzi thabiti uliyoyaganya. Kila uamuzi unaochukua siku zote una faida na hasara zake. Sioni kama una kitu cha kujilaumu. Ulikuwa uamuzi sahihi kwa nchi kubwa kama Marekani. Nadhani ni muda sasa umtafute mwenzi wako ukizingatia tabia yake zaidi. Kwa kuwa una green card nadhan unaweza kuja Bongo kwq muda kama miezi 3 hivi ukimshirikisha MUNGU utampata mke kipenzi cha moyo wako. Amini ktk Yeye akutiaye nguvu. Amina.
 
Kuchelewa kumaliza chuo/elimu ya juu sio tatizo sana coz kwa wengi wetu finances zilikuwa magumashi kwa hiyo ilibidi tuchelewe kidogo. Tatizo kwa mleta mada ni kutojichanganya na wadada hasa alipokuwa late twenties and early thirties. Kujichanganya ni muhimu sana pia huwa akili ya mapenzi ni tofauti na akili ya kawaida. Ukitaka upime vitu in details kwa mdada huwezi kupata mtu wa kuoa...coz hayupo mtu perfect.
 
Kuna movie moja nilikuwa naangalia ...nimecheka mdada baada ya pressure za kuambiwa umri umeenda haolewi...

Amekuja na list ndeefu ya vigezo viiingi...handsome, urefu, sijui nini...alichoniacha hoi ni kumalizia na 'asiwe na mama'

Mwenzake anamshangaa ...how...amejizaa mwenyewe? eti anajibu ... si amekufa...
 

eti wanakuchaguli kwan wew huna macho? fanya roho yako inapenda usiwasikilize ndugu tho mueleweshe mama yako ndo mtu muhimu. pole
 

Umri unapozidi kwenda choice inazidi kupungua ...si kwa wanawake wala wanaume...possibility ya kupata magumashi ni kubwa sana ...kwa sababu huna muda tena wa kuchunguza...mfano wengi tuliolewa na watu ambo hatukuanza kujuana kwa gia ya ndoa...ndoa ilikuwa matokeo ya kiridhika kuwa tunaendana na tunaweza ishi pamoja.. .

Lakini umri ukienda kila relationship inakuwa serious hata kama hai deserve...
kwa kuwa unakimbia na muda...
 

Binafsi siamini katika courtship ya mda mrefu. Nilichelewa kumaliza chuo lakini bado haikuwa sababu ya kuathiri uwezo wangu kimahusiano. Nikikutana na mdada ndani ya mwaka inatodha kufanya maamuzi.

Alichokosea ni kutojichanganya na wanawake kwa hiyo hata approach yake kwao ni tatizo. Na kwa umri huo wa 37-40 ndio atapata shida sana.
 

Nashukuru kwa mawazo lakini kwenye dongo la domo zito siko hivyo. Mimi sio mtu wa kutokea kila demu lakini nina bahati ya kupendwa na nina mwangalio mzuri hivyo sijawahi kupata shida ya kupata wanawake lakini kama nilivyosema huko nyuma nili avoid kwa muda mrefu kujenga uhusiano wa kudumu. Katika umri huu hakuna cha domo tena hata hivyo ni ule umri wa watu kuangalia una nini!. Ukiwa na kazi ya professional kama yangu na una vibali vimetulia huhitaji kuongea sana lakini unaweza kwa kirahisi kubambikizwa bila mapenzi. Kigumu zaidi ni ukweli kwamba kwa umri huu kila mwanamke anakuja kwa kuolewa tu hivyo inabidi uwe mwangalifu.
Kwa sisi miaka hiyo niliona rafiki zangu wakifungwa, wengine kujiingiza kwenye mambo ya dili na kufungwa, wengine ulevi na hata madawa ya kulevya. Wengi wa marafiki zetu tuliokuja nao miaka hiyo wamerudi au kurudishwa Tanzania bila elimu na wengine bila hata posho kidogo. Hivyo nilivyo acha pombe na kupunguza mambo ya wanawake nilikuwa na nia njema na niliona mengi kwa wakati ule. Kama mnakumbuka mlishasikia Watanzania wanafungwa miaka iliyopita mambo yalikuwa si mazuri kishawishi miaka hasa ya 2000-2005
 
This is some REAL topic. I feel y'all , na kuelewa hasa ni vipi mda unaweza pita kirahisi rahisi. Na because the cause of such situations is multifactorial.

Ila ningependa kuuliza kwa mfano NN, dont you think kuwa kuna some compromise inayotakiwa?
Sidhani kwamba ikija tokea ukawa na mwenza ni kwamba yeye hajaona fault yeyote kwako. Some things can be compromised fellas!
 
Kamundu naona endelea kuwa mvumilivu uoe mtu utakayeridhia wewe..kuwa mwangalifu ya hao unaochaguliwa possibility ni kubwa wakaficha makubwa for the sake ya ndoa kama unavyojua wadada na ndoa tena..mean while don't be desperate otherwise utapata bomu..all the best
 
Last edited by a moderator:
Hivi why do indian arranged marriages have a higher success rate then most other marriages hata kwa walioko western world?
 

Nimecheka lol
 
Kuna wazee wana miaka 45 na wanaoa mabinti wadogo!!!!!we jichanganye utapata mke wewe tu ndio unajichelewesha
 
Hivi why do indian arranged marriages have a higher success rate then most other marriages hata kwa walioko western world?

Mambo ya Wahindi si kama tunavyodhani...labda wahindi wa Tz...ila huko kwao ndoa ni majanga tu...hao wanaobaka watoto wadogo na kuwatundika mitini?

Ma feminist huko ndio mwake..nina marafiki zangu 3 wote hawana hata mpango na kitu kinaitwa ndoa...na umri umeshasonga....mmoja anakaribia 50...mwingine ana approach 40...hakuna cha arranged mchumba wala nini...upper class hao...
 

Eti wanasema bata ukimchunguza sana humli,so mi nijichukulie tuuuu kisa baba au mama anaweza kudead bila kumuona mjukuu aaaarghhhhhhhhhh ila kuna uncle wangu mmoja wa kanisani aliniacha hooi one day,kuna cheo kimoja alikuwa ananishauri kugombea pale kanisani kutokana na elimu yangu ila tatizo criteria moja nilikuwa namiss (to have a wife) uncle mi nikamwambia sina mtu kwa sasa akanijibu kwa hiyo unasubiri wakufuate wakwambie uwaoe??:sleepy:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…