'PRESS Conference'...

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,800
Siku hizi tuwe makini.Mwana-CCM yeyote akisema atakuwa na Press Conference tufikiri mara mbilimbili kwenda au kufuatilia. Hawa watu wamechoka na wanatuchezea. Sumaye ndio kasema nini? Kigwangalla yuko wapi? CCM wanadhani kuwa kuchezea akili za watu ni kuwapumbaza na kuwakwamisha wasifanye mambo yao ya maana,ni jambo jema.

Washindwe na wakafe kabisa! Kama wanataka,wawe wanatupa nakala za kauli zao kabla ili tupime na kuamua kwenda au la. Pale kitatupeleka kuangalia sura ya Mtoa Kauli na maneno yake ya nyongeza. Hawa watu wanatuona sisi Mapimbi.Naamini wana-CCM watatufanye turoge,tuue,tutusi,tunune na tutende yasiyo mema...
 
Mi mwenyewe sikuamini kama sumaye keshakuwa mufilisi kisiasa namna ile. Anazungumza mafumbomafumbo tuu utadhani mwimbaji wa taarabu. Mara mtandao umeniangusha, mara rushwa, mara sina uadui na Lowasa, mara simuogopi mtu, mara mtu anaweza akanunua mtandao sijui wilaya ngapi, mara ccm sio mama yangu, mara nitafia hapahapa ccm, mara mara sina mpango wa kwenda CDM eti nikitaka nitapitia humuhumu ccm!!!! Sasa kama ukitaka utapitia humohumo, si ndio tayari umeshataka na wamekupiga chini??? unataka utakeje tena??? siamini kama hizi ni kauli za mtu aliyewahi kuwa waziri mkuu kwenye hii nchi.
 
Kama clarity hakuna urais atauweza kweli. Anashangaa nini! Ccm ndo zao!kma huna mtaji(rushwa) wa kugombea acha !
 
Ukiona hivyo ni laana ya usaliti. Haitaisha na itawasumbua mpaka milele.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom