Wafuatao ni Watu wenye sifa na hadhi za Kimataifa za kuwa Marais wa nchi ya TANZANIA kulingana na muda:- 1.Dr.W.P.SLAA 2.F.A.MBOWE 3.Prof.A.SAFARI 4.S.A.ARFI 5.M.N.MARANDO 6.S.I.MOHAMED 7.T.A.M.LISSU 8.Z.Z.KABWE 9.G.J.LEMA 10.J.J.MNYIKA 11.E.D.WENJE 11.H.M.YOUSUF 12.H.J.MDEE 13.E.WASSIRA 14.M.MSABAHA na wengine wengi wanaozidi kuandaliwa na CHADEMA nchi nzima. Kwa safu hiyo hapo juu, TANZANIA inaweza kuongozwa na marais toka CHADEMA kwa miaka 70 mfululizo hata kama wataongoza miaka mitano mitano kila Rais. Yaani toka mwaka 2015 hadi 2085 kama Mungu akipenda nchi itaongozwa kizalendo na CHADEMA miaka yote hiyo. Safu kama hiyo ipo pia kwa ngazi zote za chini, yaani kila jimbo la uchaguzi, kila kata/shehiya na kila kijiji/mtaa kwa sasa nchini. Hivyo jukumu kubwa lililopo mbele kwa sasa ni kuwaandaa Wananchi kisaikolojia kuupokea uongozi mpya wa Tanzania ifikapo Novemba 2015 baada ya wao kupiga kura na kuufutilia mbali utawala wa kale. Tafiti zinaonyesha wazi kuwa watanzania wengi vijijini wanataka mabadiliko, hivyo iwapo haki itatendeka kwa ccm kuacha kuhonga wapiga kura na kununua shahada zao, asilimia zaidi ya 80% ya majimbo yataenda CDM 2015 na kumwezesha rais mpya kutekeleza vema ilani na sera za chama chake kwa manufaa ya wote. MODS MSIUNGANISHE UZI HUU NA MWINGINE ILI WATU WAWEZE KUUJUA UKWELI HUU UNAOPOTOSHWA MASAA 24 NA MAKADA WA CCM WALIOKOSA UZALENDO NA KUENDEKEZA MAKUNDI NA FEDHA CHAFU. Karibuni kwa mjadala.