Kidudu Mtu
Member
- Nov 7, 2009
- 64
- 0
Nimesoma kisa cha DC na DED kutoelewana kwa miezi kadhaa bila ya hatua kuchukuliwa kuweka mambo sawa.
Nadhani tatizo ni kuwa wote huteuliwa na Rais na hivyo ndiye mwenye mamlaka ya kuwachukulia hatua na hata kutengua uteuzi wao. Hii inaonyesha jinsi mlundikano wa madaraka kwa mtu mmoja (Rais) unavyoweza kuathiri utendaji kazi hasa pale maamuzi ya haraka yanapotakiwa.
Serikali yawa bubu msuguano wa DC na Mkurugenzi Bagamoyo
Serikali imekataa kuelezea uamuzi wake kuhusu uhusiano mbaya uliopo kati ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani, Rhoda Nsemwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Magessa Mulongo, ambao unadaiwa kusababisha shughuli za maendeleo ya wananchi wilayani humo kuzorota.
Hatua hiyo imedhihirika, baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Celina Kombani, kukataa kuelezea uamuzi wake kuhusu tatizo hilo licha ya Mkurugenzi Mtendaji huyo kuiomba serikali kuu kuingilia kati tatizo hilo ili kurejesha maelewano na maendeleo wilayani humo.
Kombani alikataa kutoa msimamo wa serikali alipoulizwa na Nipashe wiki hii kueleza uamuzi wa serikali kuhusu uhusiano huo kati ya Mkurugenzi Mtendaji na Mkuu huyo wa Wilaya.
Wasiliana na mkuu wa mkoa, tunaenda kwa protocal (itifaki), alisema Kombani kwa ufupi.
Alipoelezwa na Nipashe kuwa Mkurugenzi Mtendaji ameiomba serikali kuu kuingilia kati tatizo hilo, Kombani alishikilia msimamo wake wa kutaka suala hilo aulizwe mkuu wa mkoa kwa kusema: Mkuu wa Mkoa ndiye serikali kuu ya mkoa na mkuu wa wilaya ndiye serikali kuu ya wilaya. Hiyo ndiyo itifaki ya serikali.
Nipashe iliwasiliana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Hajati Amina, ambaye naye alikataa kuelezea uamuzi wa serikali kuhusu tatizo hilo, badala yake alimtaka mwandishi awasiliane na uongozi wa wilaya, au wananchi au viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Bagamoyo. Sina cha kuzungumza. Serikali kuu iko pia wilayani, alisema Hajati Amina.
Alipoelezwa kuwa kwenye uongozi wa wilaya ndiko uhusiano mbaya uliko kati yake na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Hajati Amina alisema: waulizeni wananchi, pia chama kipo. Mimi sijui kama kuna ugomvi, naomba nisizungumze kitu ambacho sikijui.
Wiki mbili zilizopita, Mkurugenzi Mtendaji huyo, alizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), wilayani humo na kuiomba serikali iingilie tatizo hilo, kwa kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya mmoja wao au kumhamisha kikazi, kwa vile hali hiyo imekuwa ikisababisha shughuli za maendeleo ya wananchi kuzorota.
Mimi na Mheshimiwa DC (Mkuu wa Wilaya) hatupikiki kabisa, kuna tatizo kubwa kati yetu. Naiomba serikali kuu iingilie kati, ama ichukue hatua za kinidhamu au uhamisho. Mimi ni Mkristo nabeba msalaba, siridhishwi kabisa na hali hii kwani maendeleo ya wananchi yanakuwa hayapatikani, alisema Nsemwa.
Alisema uhusiano mbaya kati yake na Mkuu wa Wilaya umekwenda mbali zaidi kwani tangu Agosti, mwaka huu, wamekuwa wakinuniana na kwamba, wamekuwa wakiongea kupitia Katibu Tawala Mkoa (RAS).
Alisema hali hiyo imekuwa ikimkosesha amani kiasi cha kufikia kukata shauri la kutaka kuandika barua kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kuomba kujiuzulu kazi ndani ya saa 24, lakini amekuwa akizuiwa kufanya hivyo na baadhi ya jamaa zake wa karibu.
Alipoulizwa sababu gani iliyowafikisha yeye na Mulongo katika hali hiyo, Nsemwa alisema hajui sababu ni nini, lakini ana wasiwasi huenda inatokana na Mkuu huyo wa Wilaya kufanya kazi bila kujua miongozo ya serikali.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Mulongo alipotakiwa kutoa ufafanuzi kuhusiana na madai yaliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji huyo, hakuwa tayari badala yake akasema: "(Mkurugenzi Mtendaji) aliamua kuwatania tu... Karibu.
CHANZO: NIPASHE
Nadhani tatizo ni kuwa wote huteuliwa na Rais na hivyo ndiye mwenye mamlaka ya kuwachukulia hatua na hata kutengua uteuzi wao. Hii inaonyesha jinsi mlundikano wa madaraka kwa mtu mmoja (Rais) unavyoweza kuathiri utendaji kazi hasa pale maamuzi ya haraka yanapotakiwa.
Serikali yawa bubu msuguano wa DC na Mkurugenzi Bagamoyo
Serikali imekataa kuelezea uamuzi wake kuhusu uhusiano mbaya uliopo kati ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani, Rhoda Nsemwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Magessa Mulongo, ambao unadaiwa kusababisha shughuli za maendeleo ya wananchi wilayani humo kuzorota.
Hatua hiyo imedhihirika, baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Celina Kombani, kukataa kuelezea uamuzi wake kuhusu tatizo hilo licha ya Mkurugenzi Mtendaji huyo kuiomba serikali kuu kuingilia kati tatizo hilo ili kurejesha maelewano na maendeleo wilayani humo.
Kombani alikataa kutoa msimamo wa serikali alipoulizwa na Nipashe wiki hii kueleza uamuzi wa serikali kuhusu uhusiano huo kati ya Mkurugenzi Mtendaji na Mkuu huyo wa Wilaya.
Wasiliana na mkuu wa mkoa, tunaenda kwa protocal (itifaki), alisema Kombani kwa ufupi.
Alipoelezwa na Nipashe kuwa Mkurugenzi Mtendaji ameiomba serikali kuu kuingilia kati tatizo hilo, Kombani alishikilia msimamo wake wa kutaka suala hilo aulizwe mkuu wa mkoa kwa kusema: Mkuu wa Mkoa ndiye serikali kuu ya mkoa na mkuu wa wilaya ndiye serikali kuu ya wilaya. Hiyo ndiyo itifaki ya serikali.
Nipashe iliwasiliana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Hajati Amina, ambaye naye alikataa kuelezea uamuzi wa serikali kuhusu tatizo hilo, badala yake alimtaka mwandishi awasiliane na uongozi wa wilaya, au wananchi au viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Bagamoyo. Sina cha kuzungumza. Serikali kuu iko pia wilayani, alisema Hajati Amina.
Alipoelezwa kuwa kwenye uongozi wa wilaya ndiko uhusiano mbaya uliko kati yake na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Hajati Amina alisema: waulizeni wananchi, pia chama kipo. Mimi sijui kama kuna ugomvi, naomba nisizungumze kitu ambacho sikijui.
Wiki mbili zilizopita, Mkurugenzi Mtendaji huyo, alizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), wilayani humo na kuiomba serikali iingilie tatizo hilo, kwa kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya mmoja wao au kumhamisha kikazi, kwa vile hali hiyo imekuwa ikisababisha shughuli za maendeleo ya wananchi kuzorota.
Mimi na Mheshimiwa DC (Mkuu wa Wilaya) hatupikiki kabisa, kuna tatizo kubwa kati yetu. Naiomba serikali kuu iingilie kati, ama ichukue hatua za kinidhamu au uhamisho. Mimi ni Mkristo nabeba msalaba, siridhishwi kabisa na hali hii kwani maendeleo ya wananchi yanakuwa hayapatikani, alisema Nsemwa.
Alisema uhusiano mbaya kati yake na Mkuu wa Wilaya umekwenda mbali zaidi kwani tangu Agosti, mwaka huu, wamekuwa wakinuniana na kwamba, wamekuwa wakiongea kupitia Katibu Tawala Mkoa (RAS).
Alisema hali hiyo imekuwa ikimkosesha amani kiasi cha kufikia kukata shauri la kutaka kuandika barua kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kuomba kujiuzulu kazi ndani ya saa 24, lakini amekuwa akizuiwa kufanya hivyo na baadhi ya jamaa zake wa karibu.
Alipoulizwa sababu gani iliyowafikisha yeye na Mulongo katika hali hiyo, Nsemwa alisema hajui sababu ni nini, lakini ana wasiwasi huenda inatokana na Mkuu huyo wa Wilaya kufanya kazi bila kujua miongozo ya serikali.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Mulongo alipotakiwa kutoa ufafanuzi kuhusiana na madai yaliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji huyo, hakuwa tayari badala yake akasema: "(Mkurugenzi Mtendaji) aliamua kuwatania tu... Karibu.
CHANZO: NIPASHE