Kwa wana JF wote,
Hili ni wazo ambalo nimekuwa nikilifikiria kwa muda mrefu sasa licha ya kwamba professional yangu sio sheria ( in short mi sio lawyer).
Kwa mtazamo wangu, nchi yetu imefikia mahala ambapo inahitajika law firms and lawyers waangalie namna ya ku-introduce huduma hii ndani ya soko ya tanzania kutokana na ukweli ufuatao:
- Watu wengi wamepoteza haki zao pale wanapopatwa na matatizo ambayo yanahitaji msaada wa kisheria kutokana na gharama kubwa ambazo wanasheria wanatoza; mfano: kwenye ubakaji, kubambikiziwa kesi, ukatili wa kijinsia, utapeli unaotokana na bogus contracts n.k
- Watu wenye fedha au nyadhifa kubwa serikalini wameweza kutumia pesa pamoja na nguvu zao kuwafanyia maskini wanyonge vile wanavyotaka; mfano mzuri ni Mh. Andrew Chenge, Marehemu Ditopile, Mh. Zombe just kuwataja wachache
Mimi nafikiria na ninaomba kama kuna mtu ambaye anaweza aka-initiate hiki kitu ambacho operating model yake ni similar na microinsurance policies zainavyo-operate atakuwa kasaidia watanzania wengi mno.
Kinachotakiwa na ku-design packages mbalimbali ambazo watu watakuwa wana-contribute pesa ndogondogo! na endapo litatokea la kutokea lawyers wanakuwa standby kuanza kazi ya utetezi ( lakini wa Haki).
Angalizo:
- kwa nature ya nchi yetu, elimu ndo swala la msingi before and after introduction of any service/product in the market
- Nina shaka na willingness ya watu kwenye contribution, licha ya kwamba unaweza ukatumia njia mbadala kama vile mtu ku-send SMS ambayo atakatwa kiasi fulani cha pesa na wakati huohuo ana-pata points kadhaa za kuingizwa kwenye bahati nasibu ( ndo watanzania wanapenda jamani)
Kama kunamtu yeyote yuko interested: mcahngo wangu utakuwa ni kwenye kusaidia kuandaa operating model, pamoja na kufanya brainstorming ili kutouch angle mbalimbali.
Nawakilisha!