Ndugu wadau wa JF currently kuna mchakato wa kozi ya pre-entry ya dipoloma kwa wanafunzi wa masomo ya sayansi na hisabati pamoja na kiingereza wenye ufaulu wa S na E. Na kwabahati mbaya wamekuja na msamiati wao wanaita BRIDGING COURSE ambayo itafundishwa kwa miezi mitatu halafu baadae watajiunga na Ordinary diploma (masomo ya kawaida ya diploma). Hapa wadau najaribu kuona mantiki ni ipi kwasababu kama tatizo ni kiingreza basi wangekwenda hata ambao wanatarajia kuchukuliwa kwenye masomo mengine maana nao watatumia kiingereza kufundisha na bado hawakifahamu sawasawa . Je wadau huu utaratibu niwaukweli? AU NISEHEMU YA KULA PESA TU YA WATANZANIA? je ndani ya miezi mitatu hawa wanafunzu watakuwa competent zaidi ya miaka miwili waliyokuwa sekonadari? (maana hapa najaribu kutafuta tatizo binafsi silioni kabisa, au assumptions ni kuwa hawa jamaa hawakuelewa vizuri content wakati wakiwa shule) jamani au nimaelekezo ya watoa fungu (wafadhili) ili wachache wale kupitia migongo ya watu ambao eti wamefeli? Kimsingi hawa wanafunzi kwa muda wote wa kozi hii hawatalipia chochote. WADAU HEBU TULITAFAKALI HILI.