Power of evils

kanali mstaafu

JF-Expert Member
May 17, 2015
4,318
4,104
Nimetafakari kwa kina zaidi juu ya nguvu iliyopo ktk ubaya(nimejikita kutafsiri dhana ya ubaya kwa kadri jamii zetu zinavyoamini) nikaona dhahiri kuwa kwa kiasi kikubwa ubaya una nguvu zaidi ya wema hasa ukizingatia juu ya haya.

1. Mtu anaweza akafanya mema mengi machoni pa watu lakini baya moja likafuta mema yote aliyofanya na hatimae mtu anahesabika kuwa mbaya.

2. Yanayotafsiriwa kama ni ubaya katika jamii ndio yanashawishi zaidi kuliko mema, mfano mtu anashawishika kufnya ngono,kulewa n.k lakini masuala kama kusaidia wagonjwa na wahitaji huwa inahitajika nguvu ya ziada kushawishi watu wafanye.

3. Ni rahisi zaidi kwa muasherati kujulikana katika jamii kuliko yule anayependa kuisaidia watu.

4. Habari mbaya husambaa haraka mithili ya moto katika nyasi kavu lakini habari njema huchechemea kwa mguu mmoja.

5. Wakati mwingine watu wanajua kitu fulani ni kibaya na madhara yake yanafahamika lakini wanafanya tu.

6. Ni rahisi zaidi kwa watu kutoka nje wakashuhudie mzinzi alivyokamatwa kuliko kutoka nje kumsikilza mhubiri anayehubiri.

7. Maovu husisimua yaan yanatengeneza attention kubwa zaidi ya mema, mfano mdada akikatiza kapiga kimini ataamsha hamasa ya watu wengi kuliko yule aliyevaa kwa staha.

8. Kasi ya mabaya inaongezeka kila uchao zaidi ya wema

Sasa suala la kujiuliza ni nini siri ya hii nguvu iliyopo katika mambo tunayoyaita ni mabaya? Iwapo ubaya unafungamanishwa na shetani na wema ni wa mungu ambaye anaaminika kwa wengi ndiye mwenye nguvu zaidi.

Je, kwanini wema uzidiwe na ubaya? Naomba michango yenu wadau juu ya Hilo.
 
Ndugu mleta mada,kwanza kabisa nikupongeze kwa kujaribu kutanua ubongo wako kwa kuufanya ufikiri ki-falsafa zaidi.

Japo muamko wa wawachangiaji umekuwa hafifu...lakini nipende tu kusema,uchangiaji au ujibuji wa swali lako la msingi kabisa hapo mwishoni...linategemea sana kitu kinachoitwa ulimwengu wa ROHO...kama neno UBAYA lilivyo,yakuwa ni neno ambalo udhihirisho wake uko katika tokeo,ambalo huenda limetokana na wazo baya kupelekea tendo baya(ambalo ni dhahiri).....vivyo hivyo ushindani wa mikinzano hii miwili iko katika huo ulimwengu.

Kusema yakwamba ubaya unauzidi wema.....jibu la hili liko dhahiri kama ni msomaji wa maandiko,hasa kwa sisi wakristo katika kitabu cha UFUNUO..imewekawa wazi yakuwa utawala wa ulimwengu huu uko chini ya yule mpingaji...maani imeandikwa OLE WAKO UKAYE DUNIANI MAANA YULE MWOVU AMETUPWA HUKO AKIWA NA GHADHABU KALI(nimenukuu hiki kipengele si kwa usahihi wake,ila kwa ninavyo kumbuka...japo maana inabaki pale pale).

Hivyo basi ndugu yangu....mada yako na uchambuzi wa hili una-base sana ktk huo ulimwengu...maana kila kitu ni ROHO...kwa maana ya wazo(halishikiki wala huwezi kuliona) ijapokuwa hupelekea tendo,kisha tendo husika kuwekwa kweye uzani yakuwa ni je ni baya au jema....hivyo kwa kufungulia tu katika kuelekea kupata ufafanuzi wa hili ni vyema kujikita katika context(muktadha huu).

Nimejaribu kuelezea kwa mtazamo wangu,kama tu njia ya kufungua mjadala zaidi na kukaribisha wachangiaji wengine kujoin.

Ahsante.
 
Nafsi hupenda yale yanayo ifurahisha, si yanayo ihuzunisha. Nimeanza kwa kusema hivi kwa maana mambo yote maovu ndio ambayo ukiyafanya itakua ni 7bu ya nafsi yko kufurahi, ulevi, uzinzi, dhulma na hata kuuwa, maana unaua ili upate ki2 flani na hicho utakacho kipata ndio itakua 7bu ya nafsi yko kufurahi, na mambo yote yaliyo mema ukiyafanya unaiumiza nafsi yko, mf: umetafuta pesa kwa shida halafu leo unazitoa bure kuwasaidia maskini, unapesa ila unaizuia nafsi yako kufanya anasa yoyote,,,, kwa maana hiyo mambo mabaya yanaonekana kua na nguvu ushawishi na hamasa kubwa ktk jamii kwa 7bu ndio mambo yanayo zifurahisha zaid nafsi za watu kuliko mambo mema.
 
Nimetafakari kwa kina zaidi juu ya nguvu iliyopo ktk ubaya(nimejikita kutafsiri dhana ya ubaya kwa kadri jamii zetu zinavyoamini) nikaona dhahiri kuwa kwa kiasi kikubwa ubaya una nguvu zaidi ya wema hasa ukizingatia juu ya haya.

1. Mtu anaweza akafanya mema mengi machoni pa watu lakini baya moja likafuta mema yote aliyofanya na hatimae mtu anahesabika kuwa mbaya.

2. Yanayotafsiriwa kama ni ubaya katika jamii ndio yanashawishi zaidi kuliko mema, mfano mtu anashawishika kufnya ngono,kulewa n.k lakini masuala kama kusaidia wagonjwa na wahitaji huwa inahitajika nguvu ya ziada kushawishi watu wafanye.

3. Ni rahisi zaidi kwa muasherati kujulikana katika jamii kuliko yule anayependa kuisaidia watu.

4. Habari mbaya husambaa haraka mithili ya moto katika nyasi kavu lakini habari njema huchechemea kwa mguu mmoja.

5. Wakati mwingine watu wanajua kitu fulani ni kibaya na madhara yake yanafahamika lakini wanafanya tu.

6. Ni rahisi zaidi kwa watu kutoka nje wakashuhudie mzinzi alivyokamatwa kuliko kutoka nje kumsikilza mhubiri anayehubiri.

7. Maovu husisimua yaan yanatengeneza attention kubwa zaidi ya mema, mfano mdada akikatiza kapiga kimini ataamsha hamasa ya watu wengi kuliko yule aliyevaa kwa staha.

8. Kasi ya mabaya inaongezeka kila uchao zaidi ya wema

Sasa suala la kujiuliza ni nini siri ya hii nguvu iliyopo katika mambo tunayoyaita ni mabaya? Iwapo ubaya unafungamanishwa na shetani na wema ni wa mungu ambaye anaaminika kwa wengi ndiye mwenye nguvu zaidi.

Je, kwanini wema uzidiwe na ubaya? Naomba michango yenu wadau juu ya Hilo.
Sababu kubwa ni kuwa binadamu tumeumbwa (kama sio man made)au kujengwa kuzingatia mambo hasi (mabaya) zaidi kuliko mema.

Hii nafikiri inaweza kuwa sababu kubwa zaidi
 
Kwanza,unajuaje kuwa hiki kitu ni chema,na hiki ni kibaya?

Kitu kinachowaongoza kutenganisha ubaya na wema ni kipi?

Na kwanini,Mungu anahusishwa na mema na shetani anahusishwa na ubaya?

Na tunauhakika gani kuwa Mungu yupo?au shetani yupo?
 
hapo tatizo kubwa ni nini chema na nini kibaya,hiyo ni mitazamo tu ya watu.hata muuaji kuna wakati anaua kwa sababu ambayo ni njema. kwa hiyo inakuwa ngumu kutenganisha ili kufikiri kipi kinafanyika sana maana kuna unachoona wewe kibaya ambacho wengine wanakiona chema
 
hapo tatizo kubwa ni nini chema na nini kibaya,hiyo ni mitazamo tu ya watu.hata muuaji kuna wakati anaua kwa sababu ambayo ni njema. kwa hiyo inakuwa ngumu kutenganisha ili kufikiri kipi kinafanyika sana maana kuna unachoona wewe kibaya ambacho wengine wanakiona chema
We call it deviance
 
Kwanza,unajuaje kuwa hiki kitu ni chema,na hiki ni kibaya?

Kitu kinachowaongoza kutenganisha ubaya na wema ni kipi?

Na kwanini,Mungu anahusishwa na mema na shetani anahusishwa na ubaya?

Na tunauhakika gani kuwa Mungu yupo?au shetani yupo?
Hapa ndo kwenye msingi wa hoja yenyewe..Maswali yako yakijibiwa hayo ya juu ukiacha hilo la mwisho,nadhani jibu pia la mtoa mada litakuwa limepatikana!
 
Kwanza,unajuaje kuwa hiki kitu ni chema,na hiki ni kibaya?

Kitu kinachowaongoza kutenganisha ubaya na wema ni kipi?

Na kwanini,Mungu anahusishwa na mema na shetani anahusishwa na ubaya?

Na tunauhakika gani kuwa Mungu yupo?au shetani yupo?


Ndugu Einstein....labda tu nijaribu kudadavua swali/maswali yako,kama ifuatavyo nikianaza na ni nini hasa kinachokufanya kutambua ubaya na wema...jibu hapa ni simple kabisa....mwanadamu ana kiungo kimoja hatari sana..ambacho ni "UBONGO".katika organ hii ndipo hasa huo ulimwengu wa ROHO unapo cheza ngoma zake.Hapo ndipo mapambano hasa yana-take place.

Kiungo hiki(UBONGO) ndicho kinacho channel na kukuruhusu wewe ku-control "FREEWILL"(UHURU WA KUJIAMULIA).Hii FREEWILL ni sawa na daftari tupu,ambapo ni wewe sasa kuandika kwa uzuri au kulichafua.....utakapo andika kwa uzuri,ndipo unakuta MEMA yakitawala maisha ya mtu...ukiandika kwa ubaya...ndipo utakuta UBAYA ukiyatawala maisha ya mtu.

Hivyo uchambuzi wa hoja ya mleta mada bado narudia tena una-base sana katika kumakinika na kujua hasa nini maana ya ULIMWENGU WA ROHO......Mimi naamini yakuwa sisi tumeumbwa(tume-kuwa programmed katika kutenda mema).Ndio maana kama unabisha we jaribu kutembea kinyumenyume badala ya kimbelembele uone kama hata ww mwenye hutajishanaaa....mfano huu unamaanisha ya kuwa MUUMBAJI WETU amekusudia kuuishia WEMA.

Katika kujaribu kulijibu swali la pili...niseme tu MUNGU anahusishwa na WEMA kwa sababu ndie muumbaji wetu...na ametuumba vyema kabisa,bila fikra ovu..kama unabisha tizama sana ukuaji wa mtoto....ambapo jinsi utakavyo mlea katika kufuata WEMA ndivyo atakavyo kulia...hii ina maana uovu,mabaya,chuku,wivu,....yoote haya mtu hufunza au hujifunza na si kwamba anazaliwa akiwa na hivi vitu......Upendo,kwa mfano ni kitu ambacho tunazaliwa nacho naturally...hii ikichukulia mfano upendo wa mtoto kwa mama tangu akiwa mdogo kabisa na kadhalika.

Swali lako la tatu,pia nalijibu kama ifuatavyo...mimi binafsi yangu naamini kuwa MUNGU yupo..kwa sababu chache zifuatazo miongoni mwa nyingi...moja tizama jinsi ulimwengu ama DUNIA yetu ilivyo umbwa..huwezi hata kidogo kuniambia ni BIG BANG THING..kila ukionacho juu ya uso wa DUNIA si kwa bahati mbaya...kila kitu kinakitegemea kingine katika mpangilio mzuri kabisa...chukulia swala la unyeshaji wa mvua.....MUWAKO WA JUA....BAHARI KUWA HEATED....EVAPORATION.....CONDENSATION...PRECIPITATION(MVUA)...Je uratibu huu ni BIG BANG THING which happened and started just from nowhere...ndio ulipelekea coordination ya hizi taratibu.HAPANA...hii ni dhahiri ya kuwa yuko MUWEZA,MASTER-PLANNER aliye coordinate na ambaye ana-supervise haya yote.

Kwa uchache ndugu yangu Einstein na wadau wote katika uzi huu....hivi ndivyo binasfi yangu ninge jaribu kujibu maswali yaliyo ulizwa hapo juu.

Karibuni kwa michango na maoni zaidi.

Ahsanteni.
 
Ubaya umekuwa na nguvu kwa sababu mwili unahitaji kuongozwa na roho,,either ya binadamu au ya MUNGU..Binadamu aliumbwa aishi maeneo mawili kwa wakati mmoja.Roho ya binadamu ndo ilitakiwa kuwa na nguvu ndani ya mwili,,na ndipo tungeyashinda mabaya.Wakati wa Adam alikuwa uchi na asitambue,,ni kwa sababu roho yake ilikuwa ndo imedominate.Mwili ulikuwa vazi tu na ndivyo ulivyoumbwa uwe.Lakini baada ya Adamu kula tunda mfumo wa maisha yetu umechange kabisa.Tuko mwilini zaidi ya rohoni,na mwili umekuwa compromised kwa mengi.
 
Wachangiaji wengi wamejikita kwenye imani ya Dini, nami pia namuamini Mungu lakini naelewa kwamba hata bila kumwamini Mungu bado binadamu anaweza kuwa mtu mwema, na ndio msingi wa kutungwa kwa sheria za nchi nyingi zisizo na serikali za kidini. Kuna mambo ambayo jamii yote inakubaliana kwamba kimtazamo hayo ndio mambo mema.

Tatizo uovu huvuta zaidi hisia za watu kwa vile mara nyingi uovu huambatana na mitazamo mikali ya kihisia 'sharp feelings' wakati ambapo matendo mema kwa kiasi kikubwa huambatana na mitazamo mi-pole 'cool feelings'. Mfano ya uovu: Mtu amekomeshwa, ameuawa, amefanya mapenzi hadharani, ametelekeza familia, amempiga mkewe na kumtukana, amekwapua pochi yenye hela, amefumaniwa, amechambwa, ametapeliwa n.k yaani panakuwa na masham sham Fulani kutaka kujua ehe baada ya aibu hiyo, au baada ya tukio hilo mhusika/wahusika wameendeleaje,wamejisiskiaje n.k. wakati ambapo kwa matendo mema mfano: amewavusha watoto wadogo barabara, amemsamehe deni, ametembelea kituo cha wasiojiweza, amempisha kiti mjamzito kwenye daladala, amemletea mke/mume zawadi, amesomesha watoto wake shule nzuri na kuwalea vizuri n.k. hakuna anayetafakari mara mbili......Mema mengi yanachukuliwa kama wajibu au 'ndivyo inavyopaswa kuwa' na kinyume chake ndio uovu.
 
Mkuu mimi jamaa amenigusa sana kusema umetenda mema mengi sana lakini baya moja linafanya mema yote kusahaulika.Ubaya uko kama kimchanga kutoka sink la toilet ukautumbukiza kwenye ndoo kubwa ya maji ya kunywa.Chanzo na asili huwezi refer pengine zaidi ya vitabu vya dini.
 
Hata mimi huwa nashangaa mfano hawa haters huwa wana broadcast feilure tu lakini wana whisper succes
 
Kweli mkuu kwa ulimwengu huu tunaoishi mema yanakandamizwa sana na maovu!
Wakati mwingine mtu unafanya Jambo jema kwa moyo safi lakini jinsi yatakavyo pokewa kwa mitizamo hasi mpaka utajuta kwa nini ulifanya.
Hakawii kusema yule ananunua sifa, mara ile ni gia kuficha ouvu wake mara ooh.. ati ndo moja ya masharti alipewa na mangungu... almuradi hakuna jema bila malengo!
 
Nimetafakari kwa kina zaidi juu ya nguvu iliyopo ktk ubaya(nimejikita kutafsiri dhana ya ubaya kwa kadri jamii zetu zinavyoamini) nikaona dhahiri kuwa kwa kiasi kikubwa ubaya una nguvu zaidi ya wema hasa ukizingatia juu ya haya.

1. Mtu anaweza akafanya mema mengi machoni pa watu lakini baya moja likafuta mema yote aliyofanya na hatimae mtu anahesabika kuwa mbaya.

2. Yanayotafsiriwa kama ni ubaya katika jamii ndio yanashawishi zaidi kuliko mema, mfano mtu anashawishika kufnya ngono,kulewa n.k lakini masuala kama kusaidia wagonjwa na wahitaji huwa inahitajika nguvu ya ziada kushawishi watu wafanye.

3. Ni rahisi zaidi kwa muasherati kujulikana katika jamii kuliko yule anayependa kuisaidia watu.

4. Habari mbaya husambaa haraka mithili ya moto katika nyasi kavu lakini habari njema huchechemea kwa mguu mmoja.

5. Wakati mwingine watu wanajua kitu fulani ni kibaya na madhara yake yanafahamika lakini wanafanya tu.

6. Ni rahisi zaidi kwa watu kutoka nje wakashuhudie mzinzi alivyokamatwa kuliko kutoka nje kumsikilza mhubiri anayehubiri.

7. Maovu husisimua yaan yanatengeneza attention kubwa zaidi ya mema, mfano mdada akikatiza kapiga kimini ataamsha hamasa ya watu wengi kuliko yule aliyevaa kwa staha.

8. Kasi ya mabaya inaongezeka kila uchao zaidi ya wema

Sasa suala la kujiuliza ni nini siri ya hii nguvu iliyopo katika mambo tunayoyaita ni mabaya? Iwapo ubaya unafungamanishwa na shetani na wema ni wa mungu ambaye anaaminika kwa wengi ndiye mwenye nguvu zaidi.

Je, kwanini wema uzidiwe na ubaya? Naomba michango yenu wadau juu ya Hilo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom