Naombeni msaada wadau, anaejua POSTAL/ZIP CODE YA TANZANIA naomba anitajie
Postal code kwa tz ni mfumo ambao umeanzia arusha as pilot project, ila kujua postcode yako itategemea upo mkoa gani na wilaya gani, na kata gani, kwa mfumo wetu huu wa postcode uliopendekezwa huwa una tarakimu tano mfano kama ungekuwa unaishi Arusha,
kwa hyo unatoa postcode ya eneo ambako barua yako yapaswa kufika mfano kama utataka barua yako ipitie posta, tuchukulie unaishi arusha mjini, na anuani yako ipo posta ya mjini, utaandik,
Mr ..............
1 BOMA ROAD
P.O. BOX 600
23100
TANZANIA
POSTCODE HAPO NI 23100( YENYE MAANA ZIFUATAZO, 2=KANDA YA KASKAZINI, 3=MKOA KATIKA KANDA YA KASKAZINI AMBAO NI ARUSHA, 1= WILAYA KUU KATIKA MKOA WA ARUSHA, AMABAYO NI ARUSHA MJINI, 00= NI POSTA KUU KATIKA WILAYA YA ARUSHA MJINI)
Hivyo kama ungekuwa arusha mjini, postcode yako ingekuwa 23100, sasa itategemea upo wapi.