MJERUMANI MDACHI
Member
- Jun 2, 2014
- 68
- 21
Umeongea point sana.mfano kama mtu amesomea LLB akaajiriwa TRA inambidi asome postgraduate ya TAXATION ili imsaidie kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.au umesomea LLB ukaajiriwa JUBILEE INSURANCE kama mwanasheria wao hivyo ili uwe competent unalazimika kupata general knowledge ya mambo ya insurance hivyo unalazimika kusomea postgraduate ya insurance.kwahiyo sio lazima mtu awe na gpa ndogo sometime.
Jamani kwa uelewa wangu mtu mwenye post graduate diploma ni mtu mwenye degree tayari ila alikuwa ana ufaulu mdogo degree wa kuweza kuendelea na masters so ina mbidi asome post graduate diploma kubost qualification zake ili aendelee kusoma master....asante
Shardcole acha kupotosha watu jifunze kuuliza kabla ujapost kitu kishabiki.
Mtu anaesoma Post-graduate diploma maana yake anayo degree ya kitu kingine mfano Bsc in Agriculture so anahitaji asomee education hivyo anajiunga na kusomea Post-graduate diploma ya elimu na anasoma mwaka mmoja maana yake atasoma course za elimu pekee na anakuwa vizuri tena sana tu.
Advanced diploma is equivalent to Degree hamna tofauti yoyote, na mtu mwenye Advanced diploma akitaka kuendelea anasoma masters kama kawaida.
Kweli wengi tunataka ufafanuzi,ni nani mwenye elimu kubwa kati ya hawa!
Kwa hiyo form six sawa na Degree ya kwanza??? kuweni makini
Za muda tena wadau wa jukwaa hili!
Naomba kujua je! mtu mwenye post graduate diploma iliyo tofauti na digrii yake ya kwanza anaweza kuwa na ufanisi ulio sawa katika utendaji na mtu mwenye bachelor degree ya kozi husika? Kalibuni sana.
Neno au kiambishi "POST-" maana yake baada ya "after" kwa hiyo,POSTGRADUATE maana ya mafunzo au taaluma anayosomea mtu baada ya kuwa na SHAHADA(1st degree ) mtu ambaye hana shahada au degree hawezi soma kozi ambayo ni post graduate diploma au masters.
Postgraduate diploma ni mafunzo au kozi ya kukupa uelewa au ujuzi fulani juu ya degree yako. Mf, mtu aliyesoma LLB lakini akajiunga na ualimu wa sekondari anarudi masomoni jusomea elimu huyu atasoma POSTGRADUATE DIPLOMA in Education. Au mtu alisoma Bsc Geology lakini hana elimu ya gas and petrofuel anaamua kuongeza ujuzi anawezasoma POSTGRADUATE DIPLOMA in Natural Gas and Petro Fuel.
Swali lako ni je,wa degree na postgraduate diploma wanaweza kuwa na ufanisi sawa? Suala la ufanisi linategemea mhusika pia na elimu na ujuzi katika eneo husika pia na upenzi wake kwenye fani na marupurupu.
Huwezi kufananisha mlimao na mchungwa japo vyafanana, huwezi kufafanisha kadiploma na Degree, mwenye degree ana akili sana tofauti na mwenye kadiploma ka manati even though kanaweza kupachikwa jina la Advanced diploma baada ya mtu kuongezea kaelimu but ukweli utasimama daima.
Nani kakudanganya kwamba adv.dip ndo post?hivi hua mnasomaga mada kabla yakujibu?nani umemuona anadiploma akaenda kusoma post bila kua na Bsc?yani hiki kizazi Mungu atuokoe tu maana kama hata wewe unadegree basi tuna tatizo kubwa.samahani lakini inatia mashaka
Yaani wewe ndo umehit target...Siyo lazima Mtu kuwa Na ufaulu mdogo Ndo usome Post Graduate Diploma, Post Graduate Diploma mara nyingi inasomwA km course ya ujuzi maalum! Mfano, Una shahada ya sheria,unaamua kusoma Post Graduate Diploma in Criminology,Hapo unakuwa umeongeza ujuzi wa sheria Za makosa ya jinai,So ujuzi Ama utaalam maalum!
Post Graduate Diploma inasomwa katika condition zifuatazo
(1) Mtu mwenye PASS na anataka kusoma Master, baadhi ya vyuo vinataka mtu apitie PGD ili wamkubali asome Master
(2) Watu wenye Advance Diploma, Baadhi ya vyuo havipokei watu wenye Advance Diploma kusoma Master mpaka asome PGD ili akubalike
(3) Kwa mtu mwenye degree ya fani fulani kama Engineer, law nk anataka asome fani nyingine ili aongeze ujuzi tofauti au hapo baadaye asome master ya kitu alichosemea kwenye PGD
Yap kaka/mkuu. Uko sahihi kabisa. Nikupe LIKE ya maandishi.
Tuhitimishe kwa kusema tu kuwa PGD ni kubwa kuliko Bachelor Degree na ndogo kuliko Masters Degree!
Pia kwangu mimi, simsemei mwingine kwamba: Advanced Diploma ni Kubwa sana kuliko Diploma lakini ni ndogo( kidogo kwa content) kuliko Bachelor Degree
Jamani kwa uelewa wangu mtu mwenye post graduate diploma ni mtu mwenye degree tayari ila alikuwa ana ufaulu mdogo degree wa kuweza kuendelea na masters so ina mbidi asome post graduate diploma kubost qualification zake ili aendelee kusoma master....asante
Nakumbuka wakati nipo Undergradutae tulikuwa tunasoma na watu wa Advance Diploma baadhi ya kusoma, na wakati nasoma Master tulikuwa pia tunashea baadhi ya course na watu wa PGD, na wengine niliokuwa nasoma nao Master waliunga tokea PGD
Kiuhalisi hakuna tofauti kati ya Advance Diploma na Undergraduate ila ni kama kuwakomoa tu ili wasome PGD, ila Master na PGD hazipo sawa