Pombe sio chai

Aloyce Mkwizu

Member
Dec 19, 2016
70
53

upload_2018-1-26_20-26-23.png


NA: ALOYCE MKWIZU.

Pombe sio chai wala maji ya kunywa. Pombe sio mboga kwamba lazima ule na chakula. Pombe sio dawa useme nipo kwenye dozi ya mwaka. Vijana wanawaiga wazee kunywa, wamesahau methali inayosema kuwa "ukimuiga tembo kunywa, utachanika msamba." Pombe sio mbaya ila madhara yake ndio mabaya. Kwanini ujitese wakati kuna juisi na maziwa.

Walevi wangapi wanataka;
  • Kisukari.
  • Matatizo ya moyo.
  • Saratani ya ini.
  • Msongo wa mawazo.
  • Kusinyaa kwa ubongo.
  • Ugonjwa wa kongosho.
  • Kupoteza hisia.
  • Shinikizo la damu.
  • Anemia.
  • Maumivu ya misuli.
  • Kusinyaa kwa uso.
  • Kuharibika kwa mfumo wa uzazi.
  • Kitambi na kunenepa ovyo.
Pombe ni ghali kuliko maziwa, juisi na asali lakini umeamua kupoteza hela zako kwa kitu ambacho hakina ladha wala faida katika mwili wako. Wala sikushauri uache pombe, pesa ni yako na afya ni yako. Nimetimiza wajibu tu ili mwisho wa siku usiseme sikujua.
Wahenga walisema "Sikio la kufa halisikii dawa."

Kwa ushauri nasaha:
+918448628500
aloycemkwizu99@gmail.com
 
Wewe endelea kunywa hizo juice zako na maziwa sie acha tuendelee na pombe zetu but mwisho Wa siku mnywa juice na mnywa pombe wote tutarudi udongoni
 
Muhudum ongeza balimi mbilimbili harafu umependeza chukua na ww walau bia mbili.na chenji baki nayo.sawa mrembo
 
Back
Top Bottom