Kama alivyokula matapish mbowe kwakumlamba miguu lowasa
Kweli mkuu ccm ni ile ile. Na mawaziri ni wale wale....Muhongo, Mbarawa, Mwakyembe, Makamba, Nchemba, Lukuvi, etal
Watanzania kwa wivu kwani Waziri aliyekuwepo awamu iliyopita kuna dhambi gani akiteuliwa tena hapa cha muhimu mawaziri wanatekeleza mambo ambayo Rais wa sasa anaagiza. Sasa watu wanataka sura mpya sijui zitoke sayari gani!!!
Basi pombe yako kunywa mwenyewe
Kubomoa kulikua hakuepukiki, hakuna nchi inayoweza kuendelea kuwepo kwa kutumia jina la wanyonge tu bila kujali utaratibu... BTW, waliobomolewa wengi sio wanyonge bali ni wenye uwezo walioamua kupangisha hizyo nyumba
Kuhusu shule, before kuweka bei elekezi, ni lazima kujua kila kitu kinachochangia cost ya kurun every school, serikali inasubsidize shule zake, nani anasubsidize za private???
Kuhusu majibu ya jeuri ya jana, ni kweli kakosea, na nina uhakika kabisa atapata shule ya public speaking... that was not a good gesture
mwezi mzima pombe amejifungia chumbani na Tiss alafu anakuja na nape, mzee wa mabehewa feki na muhongo?
Tulitegemea iwe tamu kwa miaka walau 3. Lkn looh! Imeanza kuharibika mapema mno. Radha ya utendaji kazi wa JPM imeharibiwa na mambo matatu:-
- Bomoaboma inayoumiza wanyonge. Walipewa vibali halali na watendaji wa serikali ya chama chako. Lkn ni watendaji hao hao wanao amka alfajiri na mapema kubomoa nyumba hizo za wanyonge. Wakilia hawasikilizwi. Ni kilio cha samaki.
- Kuufyata kwa serikali ya JPM kwa wamiliki wa shule binafsi. Hawa wamiliki walipo tishia kutofungua shule zao kesho yake KATIBU wa wizara Sifuni Mchome akajichoma mwenyewe. Akayakanusha maandiko ya wizara yake mwenyewe kwa maneno rahisi ati yana nukuliwa vibaya. Lol! Sifuni acha hizo. Sema kweli tu kuwa mumeufyata. Chezea Bongo wewe!? Na hapo bado hamjaanza kuwaghasi wauza sembe. Mtaweza kweli?
- Ni Jana tu JPM alipokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari kwa majibu makavu na nyodo utadhani wake wenza waliogombana. Kila MTU alibakia kinywa wazi akimshangaa JPM kuwa kaingiwa na uwendawazimu wa madaraka ama vipi?
Tuna wasiwasi kama Pombe hii itatufikisha mwisho wa sherehe. Imeanza kuchachuka mapema mno.
hivi kuna mtu alitegemea mapya kutoka ccm ?Mkuu ni mara ngapi tumeambiwa kuwa CCM ni ILE ILE!!!!!
Hakuna Jipya ndani ya CCM.
Fafanua vizuri nani aliyeishi kimazoea????
je, ni wale viongozi mliowateua kusimamia Bandari kisha kupitisha makontena bila Ushuru????
Je, ni wale viongozi mliowateua TRA na kusindwa kusimamia ukusanyaji wa kodi??
je, ni wale mawaziri mliowateua katika wizra na kushindwa kusimamia upatikanaji wa madawa na huduma bora za afya???
je, ni wale viongozi mliowateua katika halmashauri na kushindwa kusimamia usafi wa mazingira??
Je, n wale viongozi mliowateua kusimamia maliasili na mwishowe kusai=firisha twiga wetu ndani ya ndege??
je, ni wale viongozi mliowateua kusimamia mbuga zetu mwishowe wakaua embo na kusafirisha meno nje ya nchi??
Je, ni wale viongozi mliowateua kusimamia benki kuu mwishowe wakagawana ESCROW na EPA???
Je, je, Je, Je, Je Je Je, je, Je, Je, Je Je !!!!!!!!!!
Ni akina nani hao???? Naomba ufafanuzi ili niendelee kuchangia hoja hii!!!!!
SErikali ya Awamu ya Tano bado imekumbatia wale wale ambao walikuwa Awamu iliyopita.
Hivyo tutegemee madudu makubwa kuliko Awamu ya NNE endapo kama Mh. Rais hatokuwa makini na kuwaondoa kwani tayari wameshaanza kumuharibia katika awamu yake ili yatimie yale aliyosema Mh. fulani kuwa:-
"WANAOKWEPA KODI HAWATAACHA KIRAHISI............." by JK
siku moja baada ya sifuni mchome kuteuliwa katibu wizara ya elimu kuna mdau wa jf aliandika hivi nanukuu , " NAPINGA SIFUNI MCHOME KUTEULIWA KATIBU MKUU WIZARA YA ELIMU " mwisho wa kunukuu , uzi upo humuhumu jf , na baada ya muda mfupi ikaletwa divisheni 5 .je, kwa hiyo katibu wa Wizara Sifuni Mchome alikula matapishi yake??????
hatukutegemea mtu kama Katibu wa Wizara anaweza kutoa kauli kisha akaja kuikanusha mwenyewe!!!!!
Ni aibu kwa Taifa letu ina maanisha Serikali inawaogopa Wafanyabiashara!!!! Je, tukisema kuwa shule binasfi ni za Viongozi Serikalini mtatukatalia????
Mkuu naona jamaa hujamuelewa vizuri. Anachokosoa nikwamba tangu uhuru serikali nimoja tu ya Ccm na Tanu. Watumishi wa serikali hii hii ndio waliotoa vibali kwa raia wakajenga maeneo yasiyo ruhusiwa. Sasa iweje hukumu iwashukie wananchi tu bila wahusika upande wa serikali kuchukuliwa hatua?
Hill jina unalotumia tu tayari unaonesha fikra zako zimekaaje ..sema unataka wapi leo ukakeshe kigodoro?
Ni kweli usemayo mkuu. Huyu mtu hatokuwa na jipya. Anaendeshwa na mfumo ccm. Na ccm ni ile ile..
Tatizo lenu kubwa mnakosa uvumilivu, lakini pia mmezoea majungu.
Magufuli ndiyo kwanza ameanza kufanya kazi yake tulieni tumpe muda na ushirikiano sio kila kitu ni kuponda tu!
Eti huyu mtu hatokuwa na jipya... Kumbe mwenye jipya ni nani...Mbowe, Mbatia au Lowassa?
Tunajua wachache hampendi kuona Magufuli hakifanikiwa, lakini wengi tunamuombea kwa Mungu!
Near Tegeta Machinjioni.
Ukimwona anayelia kuliko wote huyo huyo ndo mchawi wako ..unaonekana ulikuwa unahusika sana na sahivi tumefunga Magufuli, katambike mizambwa yako
hiv inamana mtu ukiwa bavicha ndo unatokwa na akili kiasi hiki?yaani sioni points zaidi ya mipasho na wivu wakike,rudini kwenu mtuachie nchi yetu mb.wa nyie
Tatizo lenu kubwa mnakosa uvumilivu, lakini pia mmezoea majungu.
Magufuli ndiyo kwanza ameanza kufanya kazi yake tulieni tumpe muda na ushirikiano sio kila kitu ni kuponda tu!
Eti huyu mtu hatokuwa na jipya... Kumbe mwenye jipya ni nani...Mbowe, Mbatia au Lowassa?
Tunajua wachache hampendi kuona Magufuli hakifanikiwa, lakini wengi tunamuombea kwa Mungu!
Near Tegeta Machinjioni.