Mwana Mpotevu
Platinum Member
- Sep 7, 2011
- 3,295
- 2,505
Ni muda mfupi uliopita polisi wamepiga mabomu ya machozi ya kutosha kusambaratisha maandamano mbinga mkoani Ruvuma.
Maandamano hayo yanalenga kupinga malori yanayobeba makaa ya mawe toka wilayani humo na wazazi wameamua kuwatanguliza watoto katika maandamano hayo jioni hii.
Hadi sasa Polisi imewakamata viongozi wanaodaiwa kuongoza maandamano hayo na kiongozi mkuu ametajwa kuwa ni John John Komba (Haijaelezwa uhusiano wake na Mbunge wa jimbo hilo Kapteni John Komba).
Aidha waandamanaji wameeleza kuwa hawataacha maandamano hayo hadi hapo kitakapoeleweka na makaa hayo yaachwe kusafirishwa kwa namna tyoyote toka wilayani kwao.
Pia wameeleza kuwa hawataki kumuona Mkuu wa wilaya hiyo wala mkuu wa Mkoa kwani wamepelekewa malalamiko mara kadhaa bila kuchukua hatua yoyote.
Star Tv wameeleza katika Breaking news.
Maandamano hayo yanalenga kupinga malori yanayobeba makaa ya mawe toka wilayani humo na wazazi wameamua kuwatanguliza watoto katika maandamano hayo jioni hii.
Hadi sasa Polisi imewakamata viongozi wanaodaiwa kuongoza maandamano hayo na kiongozi mkuu ametajwa kuwa ni John John Komba (Haijaelezwa uhusiano wake na Mbunge wa jimbo hilo Kapteni John Komba).
Aidha waandamanaji wameeleza kuwa hawataacha maandamano hayo hadi hapo kitakapoeleweka na makaa hayo yaachwe kusafirishwa kwa namna tyoyote toka wilayani kwao.
Pia wameeleza kuwa hawataki kumuona Mkuu wa wilaya hiyo wala mkuu wa Mkoa kwani wamepelekewa malalamiko mara kadhaa bila kuchukua hatua yoyote.
Star Tv wameeleza katika Breaking news.