Polisi: Waandishi wa Habari wa Jambo TV na Manara TV wamekamatwa kwa Kuendesha Online TV Zisizosajiliwa

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Jeshi la Polisi lingependa kutoa ufafanuzi kuhusiana na Waandishi wa Habari wawili waliokamatwa na kushikiliwa kwa mahojiano na kukamilisha ukusanyaji wa vielelezo ambavyo vilikuwa vimesha kusanywa toka walipoanza kufuatilia kutokana na tuhuma zinazowakabili.

Waandishi hao ni Baraka Lucas anayefanya kazi na Jambo TV na Ezekiel Nicco Mollel anayefanya kazi na Manara TV.

Sababu za kukamatwa mbali na kufanya kazi na Vyombo vinavyojulikana na vilivyosajiliwa wanatuhumiwa kuendesha Online Tv zao binafsi ambazo hazijasajiliwa kitendo ambacho ni kinyume na Kanuni ya 4 (1) za Kanuni za Maudhui Mtandaoni za Mwaka 2020 kama zilivyofanyiwa marekebisho 2022. Kanuni hizo zimetolewa chini ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta.

Soma Pia: Waandishi wa habari wa Jambo TV na Manara TV washikiliwa Arusha

Uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili unakamilishwa ili hatua zingine za kisheria zifuatwe kwa wakati.
 
Hakuna lolote ni kuwakamata watu ambao wameonesha Big akijitawala pale Ikulu 😃
 
Kweli walijipanga kuzima kila kitu Kuelekea Oktoba kutakua na Mengi Sana
 
Kuna utitiri wa akaunti nyingi Youtube, za udaku, podcast, siasa, habari, hii sheria inawahusu wote au wenye maoni tofauti na wakuu?
 
Kuna utitiri wa akaunti nyingi Youtube, za udaku, podcast, siasa, habari, hii sheria inawahusu wote au wenye maoni tofauti na wakuu?
Kuna vyombo vinazungumza uasherati tu kila uchwao! Sijui kwanini hawavifungii? Au ndio stories za usiku huo ndio wanazitumia kuchukulia sheria mikononi 😃
 
Hivi ushungi wa mama umesajiliwa BASATA ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…