Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,234
Haya Polisi wanachekesha sana! Yani mpaka watu wapige kelele wao ndio wanatoa kusema wamemchukuwa wao
Na hayo makosa ya kimtandao mbona kama yamekuwa mengi au kisa wanaikosoa serikali?
================
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limetoa taarifa ya kumkamata mtuhumiwa mmoja kwa tuhuma za makosa ya Kimtandao.
Taarifa hiyo ya leo Septemba 25, 2025 iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro, imesema mtuhumiwa huyo anafahamika kwa jina la Paul Chuwa, maarufu zaidi kama "Kiduku" ambaye ni mkazi wa Kijichi Temeke, ambapo taarifa hiyo imesema uchunguzi unakamilishwa na mtuhumiwa atafikishwa kwenye mamlaka zingine za kisheria.
"Jeshi la Polisi halitasita kumuhoji na kumkamata mtu yoyote anayejihusisha na tuhuma za kihalifu" imeeleza barua hiyo ya polisi.
Soma Pia: Kiduku Ofisa Ngiri mtumiaji wa mtandao X zamani twitter achukuliwa na watu wasiojulikana
Hata hivyo, taarifa hiyo ya Jeshi la Polisi imebainisha kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Septemba 24, 2025, majira ya saa 07:00 mchana, lakini haijaweka wazi aina ya makosa ya kimtandao ambayo yamefanywa na mtuhumiwa huyo.
Na hayo makosa ya kimtandao mbona kama yamekuwa mengi au kisa wanaikosoa serikali?
================
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limetoa taarifa ya kumkamata mtuhumiwa mmoja kwa tuhuma za makosa ya Kimtandao.
Taarifa hiyo ya leo Septemba 25, 2025 iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro, imesema mtuhumiwa huyo anafahamika kwa jina la Paul Chuwa, maarufu zaidi kama "Kiduku" ambaye ni mkazi wa Kijichi Temeke, ambapo taarifa hiyo imesema uchunguzi unakamilishwa na mtuhumiwa atafikishwa kwenye mamlaka zingine za kisheria.
"Jeshi la Polisi halitasita kumuhoji na kumkamata mtu yoyote anayejihusisha na tuhuma za kihalifu" imeeleza barua hiyo ya polisi.
Soma Pia: Kiduku Ofisa Ngiri mtumiaji wa mtandao X zamani twitter achukuliwa na watu wasiojulikana
Hata hivyo, taarifa hiyo ya Jeshi la Polisi imebainisha kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Septemba 24, 2025, majira ya saa 07:00 mchana, lakini haijaweka wazi aina ya makosa ya kimtandao ambayo yamefanywa na mtuhumiwa huyo.