Polisi kuanza 'doria' mtandaoni!

Polisi kuanza 'doria' mtandaoni!

Adrian Stepp

R I P
Joined
Jul 1, 2011
Posts
2,764
Reaction score
2,600
Jeshi la polisi Tanzania limeandaa kitengo maalumu kitakacho fanya 'doria' mtandaoni kufuatilia wasanii pamoja na wale wanaotumia mitandao ya kijamii vibaya kutuma picha za utupu na video zisizo na maadili.

Akizungumza na waandishi wa Habari mapema hii leo, Msemaji wa jeshi la polisi Tanzania (ACP) Barnabas Mwakaluka amesema kuwa kutokana na wasanii wengi kukaidi agizo la kuacha kusambaza picha zisizofaa wameamua kuunda kitengo cha kusimamia na sheria zitaanza kufuatwa kwa wote watakaopatikana na hatia hiyo kwa kupelekwa mahakamani.
 
Wamechelewa kuchukuwa uamuzi huu. Vyema kabisa
 
Hivi ndio inaanza leo , nilidhani hili jambo lilikuepo kabla
 
Hilo la wasanii ni geresha tu. Hii ni mbinu mpya ya Bwana Mkubwa Jiwe kutafuta wanaomtukana mitandaoni.
Huko tunakoelekea mpaka majumbani mwetu tutawekewa vikosi maalum sasa.
Wozeeeeeer 2020
 
Hatuna dira ya kueleweka .... badala ya kushughulika na mambo ya maana wanashughulika na vitu visivyoongea?

Picha zisizokuwa za maadili sipo siku nyingi na zinatendelea kuwepo. Cha maana ni kuwafundisha vijana wetu madhara ya kuangalia picha hizo.

Badala ya kupiga marufuku kamali zilizojazana kila kona wanaangaika na picha?

Kamali ninazoziongelea ni hizi
3 mzuka
Jackpot bingo
kubeti
pool table
karata tatu n.k
 
Wajitahidi sana.. hata kuuza chupi hadharani iwe kosa.
Sababu ile nguo ukiiona tu.. Inaleta taswira ya tako.

Asante
 
Itakuwa wale malaika wa kuifunga mitandao wamekula kona..

sasa ni kubanana humu humu ukitoa lugha isiyofaa,paaap..alarm inalia police
 
Wamjibu Kangi Lugola kwanza.

Wasipende mteremko.

Badala ya kukaa kwenyw instagram kuangalia nani katuma picha ya mattako ya kina wema

Wangechukua mitutu na kwenye pale mto wami ili magari yapite usiku.

Tatizo la polisi wetu wamezoe mlenda mlenda sanaaa.
 
waje wakague na avatar za ke' humu jf...nyingine zinafadhaisha san
 
Back
Top Bottom