pansophy
JF-Expert Member
- Nov 13, 2011
- 502
- 320
Kwa kweli inasikitisha kuona raia hawana amani na Jeshi la Polisi nchini.
IGP na viongozi wengi wamekuwa wakiomba umma kutoa ushirikiano kwa Polisi ili kuweza kukomesha vitendo vya kihalifu. Lakini hali inakuwa tofauti pale raia wema wanapojitolea kutoa taarifa kwa Polisi tena hii imetokea kwa Mkuu wa Kituo na mkuu wake wa upelelezi.
Taarifa zilipokelewa na vipolisi hivi (nasema vipolisi kwani hawana hadhi kuwa polisi) na mtuhimiwa alikamatwa, katika hali ya kushangaza vipolisi hivi vikamtaja raia aliyetoa taarifa zilizopelekea mtuhumiwa kukamatwa.
Tena kwa kujitapa kabisa wakasema "Kwani ni sisi, Mzee XXY (Jina nalihifadhi) ndio alituambia kuhusu wewe na mambo unayoyafanya, uwe makini na vizee kama hivi".
Sasa najiuliza kama huyu mzee aliyejitolea kutoa taarifa halafu anaanikwa na kuhatarisha maisha yake hiyo intelejensia ya polisi iko wapi?Weledi wa hawa Polisi uko wapi?
Kwa hali hii polisi sahauni kupata ushirikiano kutoka kwetu
IGP na viongozi wengi wamekuwa wakiomba umma kutoa ushirikiano kwa Polisi ili kuweza kukomesha vitendo vya kihalifu. Lakini hali inakuwa tofauti pale raia wema wanapojitolea kutoa taarifa kwa Polisi tena hii imetokea kwa Mkuu wa Kituo na mkuu wake wa upelelezi.
Taarifa zilipokelewa na vipolisi hivi (nasema vipolisi kwani hawana hadhi kuwa polisi) na mtuhimiwa alikamatwa, katika hali ya kushangaza vipolisi hivi vikamtaja raia aliyetoa taarifa zilizopelekea mtuhumiwa kukamatwa.
Tena kwa kujitapa kabisa wakasema "Kwani ni sisi, Mzee XXY (Jina nalihifadhi) ndio alituambia kuhusu wewe na mambo unayoyafanya, uwe makini na vizee kama hivi".
Sasa najiuliza kama huyu mzee aliyejitolea kutoa taarifa halafu anaanikwa na kuhatarisha maisha yake hiyo intelejensia ya polisi iko wapi?Weledi wa hawa Polisi uko wapi?
Kwa hali hii polisi sahauni kupata ushirikiano kutoka kwetu