fangfangjt
JF-Expert Member
- Apr 25, 2008
- 571
- 139
Polisi Dar waijibu Sumatra
Geofrey Nyangoro
SIKU moja baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), kulishtaki Jeshi la Polisi kwa Rais Jakaya Kikwete, kuwa ndiyo kiini cha uvunjaji wa kanuni, sheria na taratibu za usafiri za barabarani, jeshi hilo katika Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limekana tuhumu hizo.
Kukanushwa kwa tuhuma hizo, kulifanywa jana na na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani katika kanda hiyo, Vitus Nikata.Nikata aliliambia Mwananchi kuwa tuhuma hizo hazina ukweli na kwamba Jeshi la Polisi, limekuwa likijitahidi kufanya kazi za Sumatra.
"Sio kweli kuwa polisi ndio wamiliki wa daladala,mimi ninachofahamu ni kwamba kuna baadhi ya maofisa wastaafu wanafanya biashara hiyo. Lakini si kweli kama hiyo ndiyo sababu za kuvunjwa kwa kanuni, taratibu na sheria za usafirishaji zinazoratibiwa na Sumatra,"alisema Nikata.
Kamanda Nikata alikuwa akijibu tuhuma zilizotolea na Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Israel Sekrasa, kuwa mamlaka yake inashindwa kufanya kazi sababu watu waliopewa jukumu la kusimamia sheria, wana ubinafsi unaosababishwa na kuhusika kwao katika biashara ya daladala.
Nikata alisisitiza kuwa tuhuma hizo si za kweli na kwamba vinginevyo Mkurugenzi huyo wa Sumatra atoe orodha ya polisi wanaomiliki daladala hizo.
Geofrey Nyangoro
SIKU moja baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), kulishtaki Jeshi la Polisi kwa Rais Jakaya Kikwete, kuwa ndiyo kiini cha uvunjaji wa kanuni, sheria na taratibu za usafiri za barabarani, jeshi hilo katika Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limekana tuhumu hizo.
Kukanushwa kwa tuhuma hizo, kulifanywa jana na na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani katika kanda hiyo, Vitus Nikata.Nikata aliliambia Mwananchi kuwa tuhuma hizo hazina ukweli na kwamba Jeshi la Polisi, limekuwa likijitahidi kufanya kazi za Sumatra.
"Sio kweli kuwa polisi ndio wamiliki wa daladala,mimi ninachofahamu ni kwamba kuna baadhi ya maofisa wastaafu wanafanya biashara hiyo. Lakini si kweli kama hiyo ndiyo sababu za kuvunjwa kwa kanuni, taratibu na sheria za usafirishaji zinazoratibiwa na Sumatra,"alisema Nikata.
Kamanda Nikata alikuwa akijibu tuhuma zilizotolea na Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Israel Sekrasa, kuwa mamlaka yake inashindwa kufanya kazi sababu watu waliopewa jukumu la kusimamia sheria, wana ubinafsi unaosababishwa na kuhusika kwao katika biashara ya daladala.
Nikata alisisitiza kuwa tuhuma hizo si za kweli na kwamba vinginevyo Mkurugenzi huyo wa Sumatra atoe orodha ya polisi wanaomiliki daladala hizo.