Polisi: Bado tunasubiri Polepole aripoti Ofisi ya DCI; taarifa za kutekwa kwake tumeanza kufanyia kazi

Polisi: Bado tunasubiri Polepole aripoti Ofisi ya DCI; taarifa za kutekwa kwake tumeanza kufanyia kazi

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500

TAARIFA KWA UMMA

Jeshi la Polisi lingependa kutoa taarifa kuwa, bado linaendelea kumsubiri Ndg. Humphrey Polepole aripoti katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai.

Ndg. Humphrey Polepole alitumiwa barua ya wito kwa mujibu wa Sheria za nchi aripoti katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai ili atoe maelezo kuhusiana na tuhuma mbalimbali alizozitoa kupitia Mitandao ya Kijamii lakini hadi leo hajatekeleza maelekezo hayo kwa mujibu wa Sheria.

Jeshi la Polisi limeona taarifa zinazosambazwa kwenye Mitandao ya Kijamii na ndugu zake kuwa ametekwa, tayari tumeanza kufanyia kazi taarifa husika ili kupata ukweli wake.

Imetolewa na:
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi
Dodoma, Tanzania

Pia soma


DCI.jpg
 
Siku hizi kuna kasheshe, Kurasa za mitandao ya kijamii ya jeshi la polisi zimefunga comment section, Msemaji mkuu wa serikali kurasa zake zimefunga comment section.

Wao wanatoa taarifa , hawataki kupokea feedback kutoka kwa wananchi.
 
Siku hizi kuna kasheshe, Kurasa za mitandao ya kijamii ya jeshi la polisi zimefunga comment section, Msemaji mkuu wa serikali kurasa zake zimefunga comment section.

Wao wanatoa taarifa , hawataki kupokea feedback kutoka kwa wananchi.
Watu wanajilipua utakamata wangapi?!
Busara wameona wafunge
 
Hiyo maana yake ni kusema hawapo nae bila kusema hawajamchukua wao.

Ndo hapa sasa mimi huwa nagombana na wa Tz wenye tabia za kinafki na uoga kama nyumbu, mtu akijitoa kwaajili yao huwa wanajaza comments na likes kuonyesha wapo nae ila mtu huyo akitendewa unyama wa Tz huwa hawako tayari kutoa hata tone moja la jasho kwaajili ya huyo mtu achilia mbali damu hata tone la jasho hawatatoa kwaajili ya huyo mtu.

Mimi nitaendelea kugombana na keyboard warriors wote popote pale nitakapokutana nao humu jf maana ni wanafiki na ni nyumbu hawana wanachoweza kufanya kwaajili ya anaewatetea.

Hata Lissu kaachwa mahabusu miezi 6, Mbowe, Soka, Mdude pia wameachwa na hawa wanafiki wa mitandaoni.
 
Tayari wasiojulikana watakuwa wameshaMdude Nyagali.

Ila nitamuona boya sana kama alikuwa Bongo. Huwezi kutishia kupambana na wenye mifumo yao halafu ubakie salama. Nilifikiri bado yuko Cuba au sehemu nyingine salama kama kwa kina Mange huko au kwa akina Ansbert Ngurumo. Total miscalculation!
 
Ndio maana mimi kila siku huwa nasema kama upo bongo na unabifu na serikali , bora ule ugali ujambe na kulala tu, wamatumbi bado tupo hatua ya mabadiliko.
 
Siku hizi kuna kasheshe, Kurasa za mitandao ya kijamii ya jeshi la polisi zimefunga comment section, Msemaji mkuu wa serikali kurasa zake zimefunga comment section.

Wao wanatoa taarifa , hawataki kupokea feedback kutoka kwa wananchi.
Sioni mantiki ya wao kufanya hivyo, Yani unapost kitu then unafunga comment section.
Na mbaya zaidi ni vyombo vya umma, Inasikitisha sana.
 
Back
Top Bottom