Polisi asante kufundisha vyama ustaarabu katika siasa

Polisi asante kufundisha vyama ustaarabu katika siasa

YEHODAYA

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2015
Posts
36,900
Reaction score
52,036
Tumeona jiji likiendelea na shughuli zake za kiuchumi kama kawaida pasipo bugudha mabarabarani za wanasiasa wagombea uraisi walipokuwa wakirudisha fomu za ugombea uraisi tume.Hali ni tofauti na walipochukua fomu ambapo watu walijaa mabarabarani wa vyama vyote na kulifanya jiji lionekane kama jiji la maruhuni kwa masaa mengi.
Watu daladala zetu zilishindwa kufanya kazi.Biashara zilisimama yaani ilikuwa taabu juu ya taabu.

Polisi tunashukuru kwa kuvifundisha vyama ustaarabu kwenye siasa.Yaani hakuna bughudha kwa mwananchi msaka riziki yake.Jiji limetulia hadi raha/Siasa zinaendelea na watu wanaendelea na shughuli za maisha kama kawaida.
Asante polisi
 
Hawana akili hiyo, waliona mafuriko ya Lowassa yankuwa makubwa kuliko ya Magufuli wakaogopa aibu.

Anyway, kampeni zinaanza na mafuriko itakua daily dose mpaka kieleweke.
 
lakini chadema na ukawa wataanza kutoa povu kana kwamba sheria imewalenga wao tu kumbe ni vyama vyote
 
Wanafanya hivyo kwa kuionea huruma ccm jinsi itakavyopata aibu
 
Jiji lenyewe lina miundombinu ya hovyo kupata kutokea.

Barabara zote ndogo na finyu ambapo kukitokea na shughuli kubwa ya kitaifa inabidi kuna watu wateseke.

Yangekuwa majiji mengine, yale maandamano yasingeleta athari yeyote.
 
Back
Top Bottom