Gerad2008
JF-Expert Member
- Jun 9, 2009
- 583
- 287
Arusha ni mkoa ambao kwa kiasi kikubwa watumia vyombo vya usafiri wamekuwa wakijiendeshea vyombo hivyo kiholela bila kujali taratibu za uendeshaji na hii inasababisha traffic jam ambayo siyo ya lazima.
Mfano:
A:
Wakati wa jioni kuanzia saa 11 hadi saa 2.00 usiku maeneo ya kuanzia Christ church hadi jakaranda kwenye barabara ya Kijenge - Impala - Moshono, Hiace za abiria zimekuwa na tabia za kutanua na kwenda kuchomekea magari mengine yaliyoko njia kuu na kusababisha jama eneo la Gold crest yaani junction ya barabara ya Haile selasie.
Pamoja na kuwa hii imekuwa kero kubwa huwezi mwona askari yoyote anayesimamia kuhakikisha vurugu hizi zinakomeshwa.
B:
Kwenye hii hii barabara asubuhi kuanzia kituo cha mafuta cha Lalaa hadi junction ya kutoka Kijenge Juu kunamsongamano mkubwa wa magari na hii inatoka na matumizi mabaya ya barabara ya magari kuchepuka kushoto lilipo kanisa la Katoliki na wengine kuchepuka kulia mbele ya bonite na magari yote kujichomeka tena ilipo junction ya kijenge juu.
Hali hii inasababisha magari yaliyoko njia kuu ya lami toka Moshono kuja mjini kushindwa kutembea na wakati mwingine kutoka kwa lalaa hadi daraja la kijenge inaweza chukua hata dakika 20.
Tunatoa ombi lifuatalo:
1. Tunaomba trafiki wasimamie watumia vyombo vya usafiri waweze ku-comply na taratibu za barabarani bila kuwaumiza na kuwachelewesha wanaofuata sheria za usalama barabarani ikiwamo kuzuia Hiace zinazotanua kutoka Christ church hadi Jacaranda.
2. Tunaomba wale trafiki wanaosimama pale impala na kujikamatia magari asubuhi wasogee hadi pale kijenge chini watakamata wahalifu wengi wanaovunja sheria za usalama barabarani na kwa kusababisha msongamano usio na maana.
3. Trafiki wakisimamia vizuri magari barabarani nyakati za jioni na asubuhi wataweza kuingiza kipato kikubwa kupitia faini halali kuliko kuonekana barabarani tu kuanzia saa nne hadi saa 8 na kukamata makosa ambayo hayana hata madhara makubwa kwa watumiaji wengine wa barabara.
4. Trafiki wa Arusha mjini uwepo wenu na umuhimu wenu unatakiwa uonekane asubuhi na jioni mkishughulikia waendeshao magari ovyo na hapo kama ni mapato ya serikali yangeongezeka kwa kiasi kikubwa.
5. nawashauri pia trafiki washughulikie makosa yenye substance na yatakayorudisha heshima ya trafiki na si vitu vidogo vidogo vinavyoweza kuwavunjia heshima.
Mfano:
A:
Wakati wa jioni kuanzia saa 11 hadi saa 2.00 usiku maeneo ya kuanzia Christ church hadi jakaranda kwenye barabara ya Kijenge - Impala - Moshono, Hiace za abiria zimekuwa na tabia za kutanua na kwenda kuchomekea magari mengine yaliyoko njia kuu na kusababisha jama eneo la Gold crest yaani junction ya barabara ya Haile selasie.
Pamoja na kuwa hii imekuwa kero kubwa huwezi mwona askari yoyote anayesimamia kuhakikisha vurugu hizi zinakomeshwa.
B:
Kwenye hii hii barabara asubuhi kuanzia kituo cha mafuta cha Lalaa hadi junction ya kutoka Kijenge Juu kunamsongamano mkubwa wa magari na hii inatoka na matumizi mabaya ya barabara ya magari kuchepuka kushoto lilipo kanisa la Katoliki na wengine kuchepuka kulia mbele ya bonite na magari yote kujichomeka tena ilipo junction ya kijenge juu.
Hali hii inasababisha magari yaliyoko njia kuu ya lami toka Moshono kuja mjini kushindwa kutembea na wakati mwingine kutoka kwa lalaa hadi daraja la kijenge inaweza chukua hata dakika 20.
Tunatoa ombi lifuatalo:
1. Tunaomba trafiki wasimamie watumia vyombo vya usafiri waweze ku-comply na taratibu za barabarani bila kuwaumiza na kuwachelewesha wanaofuata sheria za usalama barabarani ikiwamo kuzuia Hiace zinazotanua kutoka Christ church hadi Jacaranda.
2. Tunaomba wale trafiki wanaosimama pale impala na kujikamatia magari asubuhi wasogee hadi pale kijenge chini watakamata wahalifu wengi wanaovunja sheria za usalama barabarani na kwa kusababisha msongamano usio na maana.
3. Trafiki wakisimamia vizuri magari barabarani nyakati za jioni na asubuhi wataweza kuingiza kipato kikubwa kupitia faini halali kuliko kuonekana barabarani tu kuanzia saa nne hadi saa 8 na kukamata makosa ambayo hayana hata madhara makubwa kwa watumiaji wengine wa barabara.
4. Trafiki wa Arusha mjini uwepo wenu na umuhimu wenu unatakiwa uonekane asubuhi na jioni mkishughulikia waendeshao magari ovyo na hapo kama ni mapato ya serikali yangeongezeka kwa kiasi kikubwa.
5. nawashauri pia trafiki washughulikie makosa yenye substance na yatakayorudisha heshima ya trafiki na si vitu vidogo vidogo vinavyoweza kuwavunjia heshima.