Mpalakugenda
JF-Expert Member
- Jun 2, 2015
- 4,649
- 5,074
Katika mahojiano na kituo cha BBC Swahili DSM Humphrey Polepole amedai wale walioipinga katiba pendekezwa ya wananchi wamehama hivyo amependezewa na jambo hilo.
Nimemsikia Polepole pia na ndio nikaelewa ni kwa nini nchi za wenzetu mfano kocha akishinda kombe kubwa anaamua kujiuzulu.
Huyu bwana alikuwa amefanya kazi fulani nzuri katika katiba na angeliamua kukaa kimya kama Jaji Agustino heshima yake isingeshuka kiasi hiki. Mwalimu alitufundisha juu ya kura nyama ya mtu na ni wazi Polepole ana chuki binafsi na EL ambapo naamini hata Lowassa asipokuwepo ataiamishia kwa mtu mwingine. Chuki binafsi sio nzuri.
Na katanabaisha wazi kuwa walijadiliana ndani ya chama ili kuwakata watu fulani na wakahakikisha wamekatwa (sina uhakika kama miongoni mwao alikuwemo Jaji Ramadhani, Pinda, Sumaye, Mahiga nk), ushahidi mwingine wa wazi kuwa taratibu za chama chao zilikiukwa na kuna wakubwa waliokuja na majina mifukoni!
HP alikuwa moto wa kuotea mbali wakati wa vikao vya mbunge la katiba lilikuwa likiendelea Dodoma, nilidhani anauchungu na maoni ya wananchi, kumbe kajamaa na katiba ya wananchi ni vitu viwili tofauti......
Mi nadhani kuna fungu ametengewa na CCM kwa kazi kubwa anayoifanya, sio bure
anasema ukweli kama kweli ukweli leo hii slaa aliyegomea katiba yuko wapi,au na wewe umenunuliwa kwenye bilion 10 za mbowe,
na kama anayoyasema hayana ukweli na hayawagusi kwanini mnamfata usiku saa nane mnataka kunfanya nini kama anachokisema hakiwagusi?
mungu atalipa tu maana malipo ni duniani
ccm imepotosha vijana wengi sana , huyu polepole kajisahau anaongea kama vile hatakuwepo tena mwakani !
Nashukuru hata POLEPOLE AKIONGEA HAJUI nini nini kinamshitaki ktk porojo zake zote.