Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 25,946
- 38,656
Ndugu Humphrey Polepole akizungumza na jamii kupitia Social Media siku chache zilizopita, amemtaka Rais Samia kuzungumzia masuala ya Wanyonge, Ujamaa, haki na kadhalika kwenye kampeni zake kuelekea uchafunzi mkuu hapo 29 Oktoba 2025.
Pamoja na mambo mengine, mimi ninakubaliana na baadhi ya hoja za Polepole. Lakini hili la kumshauri Samia aseme nini kwenye kampeni zàke, ninaona ni kama Polepole anatupiga changa la macho kwa maneno yanayojipinga
Haya ndiyo maoni na mtazamo wangu kwenye hili la kumshauri Samia
Pamoja na mambo mengine, mimi ninakubaliana na baadhi ya hoja za Polepole. Lakini hili la kumshauri Samia aseme nini kwenye kampeni zàke, ninaona ni kama Polepole anatupiga changa la macho kwa maneno yanayojipinga
Haya ndiyo maoni na mtazamo wangu kwenye hili la kumshauri Samia
- Polepole anatuambia anapinga uchaguzi mkuu kufanyika kwa sababu taratibu, utamaduni na desturi nzuri za ndani ya CCM zimekiukwa
- Polepole anatufumbua macho kuhusu CCM kuingilia uchaguzi kupitia muunganiko wa kimtandao baina ya NIDA na NEC chini ya udhibiti wa CCM
- Polepole anauanika mtandao wa mafisadi na mbinu zao za kuibagaza na kuibananga Tanzania.
- Polepole sasa anakuja na hoja za kumshauri Samia aongee nini kwenye kampeni zake. Hapa pia analalamikia msaidizi aliyepo ofisi binafsi ya Rais kwa kumshauri vibaya.