Polepole asingekuwa mjamaa angepata support zaidi!

Ndio maana sishabikii chama chochote...

Sababu kwa Africa hata kwa mfano CDM kwa Tanzania wangeshika nchi, na wao wangekataa kuachia serikali kwa kuja na sheria zao za nywii nywii ili waedelee kuishi, tumeona Kenya wameshauwana sana kutokubali chama kingine kuachia halafu huko KANU kama CCM ilishajifia zamani, lakini haya mauaji ni kati ya vyama vipya....
Zanbia nao ni vile vile,....kila siku fujo wakati ZANU ilishakufa zamani....
 
Hiii issue imetokea jana. Anyway, you are missing the point. Haya sio mashindano ya nani anaongelewa na nchi ngapi. Huo ni utoto, distraction.

Jambo muhimu ni kupinga haya matendo maovu kwa raia yoyote wa Tanzania. Haki za msingi za raia zilizopo kwenye katiba ya JMT zinatakiwa kuheshimiwa.

Kama mtu yoyote ana makosa, amekosea akamatwe na polisi kwa mujibu wa sheria na sio kutekwa, kufikishwa mahakamani na sio kufichwa, kuteswa,kupotezwa, kuuwawa na haki itendeka akifikishwa mahakamani kwa mujibu wa sheria za JMT zetu na ushahidi usio na shaka.
 
Mabeberu hawana msaada wowote kwenye issue ambazo ni domestic.Ingekuwa wana msaada leo Tundulissu angekuwa huru maana ni mfuasi wa falsafa za kibepari.Kapigwa risasi kibao walisaidia nini?
Ukishasema neno beberu tayari kuna shida hapo,
Hakuna bure
 
Kila nchi ina matatizo yake sasa, Wenye nchi/wananchi msipopambana na hali yenu hakuna wa kuwasaidia.

Huu sio wakati wa siasa za kukomboa nchi kwenye mikono ya ukoloni.
 

Karibu sana sisi tumeongea haya kwa miaka 10 sasa naona ndiyo misukule mnatoka usingizini
 
TL ana connection kubwpa
 
Karibu sana sisi tumeongea haya kwa miaka 10 sasa naona ndiyo misukule mnatoka usingizini
Hoja yake ni kwamba Lissu angetekwa kungekuwa na Kelele nyingi. Kwamba unahamasisha watu wasijali sababu aliyetekwa ni Polepole sio? Unahamisha mjadala, nguvu kwenda sehemu ambayo haina tija, haisaidii Taifa.

Sasa hii hoja yako inatusaidiaje leo kukomesha huu uhuni? Ni maoni yako kwamba hizi issue za wahuni tuwaachie wewe na Lissu pekee wapambane nazo? Machawa wa Samia wanapenda iwe hivyo pia.

Wewe lengo lako inaonekana ungependa watu wakae kimya, unakerwa sana na watu wengi kujitokeza kupiga kelele haya matukio ya wahuni. Watekaji wangependa iwe hivyo, mpo timu moja na wahuni kwa kujua au kutokujua.

Upo tayari kujigawa na kugawanywa ndio maana mnatawaliwa na genge, familia chache za wahuni kwa kutumia uvyama, ukabila, dini, name calling.

Watanzania wengi wamevuka hizo level za kufikiri ndio maana unaona kelele nyingi za watu kutoka sehemu zote za Watanzania kwa yeyote anayetekwa upende usipende.
 
Maoni yanayopotosha kama haya huchukiza
Hao unaosema mabeberu huo msaada kwa nini hawautoi kwa wanaoonewa na kuuwawa Kenya, Uganda, Rwanda? Au huko napo wanaoonewa na kuuwawa ni wajamaa?
Yani nchini nyingine wakutolee msaada ambao upo ndani ya uwezo wa maamuzi ya wananchi?
 
Wasaliti mnatafuta kichaka cha kujisafisha usaliti wenu mlioufanya kwa polepole
 
Umesema vema aisee
 

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…