Kamanda Asiyechoka
JF-Expert Member
- Sep 13, 2020
- 3,166
- 4,581
Unazungumzia mambo ambayo yapo wazi kama ukaguzi wa ATCL, deni la taifa, sera za majimbo za CHADEMA hizi ni hoja zipo wazi. Na mwananchi wa kawaida sasa ambae maisha yake yamekuwa duni haya masuala uliofafanua hayana msaada kwake.
Tunataka utuambie kwa nini maisha yamekuwa magumu uraiani na kwa nini CCM haisadii wananchi?
Watu wana maisha magumu wanashindia mihogo ya kukaanga. Biashara zimefungwa na watu wanashindwa kujiajiri maana hamna uwezo wa watu kununua, ndio maana biashara zinakufa. Mbona haya hujafafanua na kutoa majibu maana wananchi wana hali mbaya sana. Alafu unaleta tabasamu la kinafiki sababu wewe una uhakika wa maisha.
Tunataka utuambie kwa nini maisha yamekuwa magumu uraiani na kwa nini CCM haisadii wananchi?
Watu wana maisha magumu wanashindia mihogo ya kukaanga. Biashara zimefungwa na watu wanashindwa kujiajiri maana hamna uwezo wa watu kununua, ndio maana biashara zinakufa. Mbona haya hujafafanua na kutoa majibu maana wananchi wana hali mbaya sana. Alafu unaleta tabasamu la kinafiki sababu wewe una uhakika wa maisha.