Majok majok
JF-Expert Member
- Aug 3, 2023
- 618
- 1,566
Nafikiri ndio mara ya kwanza kwa kocha Gamondi kwenda kucheza mechi kwenye viwanja vya mikoani na ameonja shubiri ya aina yake.
Viwanja vya mikoani vina aina yake ya uchezaji na vina aina ya wachezaji wanaoweza kucheza kwenye viwanja vya aina Ile, nafikiri pia hakushauriwa vizuri kwenye namna ya upangaji wa kikosi chake kilichoanza, huwezi kwenda viwanja vya mikoani ukaanza na wachezaji aina ya skudu. Unakwenda mikoani unaanza na zawadi mauya ambae hana mechi fitness matokeo yake IHEFU walikuwa wanafika golini kwa Yanga wanavyotaka.
Matokeo yake kiungo kikafa kabisa maana na Sure boy hana match fitness ikatengeneza loop hole ya wachezaji wasiokuwa na msaada pale kwenye kiungo.
Tunakubali rotation ingefanyika kutokana na ratiba ngumu lakini ingefanyika kipindi cha pili baada ya kuwa kikosi cha kwanza kimemaliza kazi yake, mchezaji Kama skudu ni wa kuingia kipindi cha pili tena ikiwa timu ishapata matokeo, mpira wake ni wa show game ambao autakiwi kwa timu inayosaka matokeo kwa udi na uvumba!
Yote kwa yote kuteleza sio kuanguka ndio mpira ulivyo na ndio maana unapendwa na watu duniani, kipigo kitamuamsha kocha na wachezaji wake na kuelewa ya kwamba dharau yoyote Ile inaweza kuwaangamiza na kuwapotezea ramani ya kuusaka ubingwa, sidhani Kama atarudia kupanga kikosi cha majaribio tena kwenye mechi yoyote Ile, kitendo cha kuanza na wachezaji 7 wakaa benchi ambao hawakuwa na mechi fitness yoyote ilikuwa ni kitanzi cha kwanza kwa Gamondi.
Rotation huwa inafanyika kwa umakini ili kubalance nguvu ya timu isipotee kutokana na wengine kutokuwa timamu kimwili, lakini yeye akaingia mkenge!
Maumivu ni kwa mashabiki na wanachama lakini wakae wakijua ili dhahabu iwe dhahabu ni lazima ipite kwenye moto, kipigo cha IHEFU kimempa kocha Gamondi somo zuri na kitamuamsha usingizini na kumkaribisha rasmi kwenye LIGI ya Tanzania.
IHEFU wamefanya kazi yao na wanastahili pongezi lakini waendelee ivyo ivyo na kwenye mechi nyingine na sio waishie kukamia mechi moja tu kati ya mechi 30 za ligi.
NB: Mganga wa Ihefu ni kiboko pale mbalali kashindikana😆😆😆
Viwanja vya mikoani vina aina yake ya uchezaji na vina aina ya wachezaji wanaoweza kucheza kwenye viwanja vya aina Ile, nafikiri pia hakushauriwa vizuri kwenye namna ya upangaji wa kikosi chake kilichoanza, huwezi kwenda viwanja vya mikoani ukaanza na wachezaji aina ya skudu. Unakwenda mikoani unaanza na zawadi mauya ambae hana mechi fitness matokeo yake IHEFU walikuwa wanafika golini kwa Yanga wanavyotaka.
Matokeo yake kiungo kikafa kabisa maana na Sure boy hana match fitness ikatengeneza loop hole ya wachezaji wasiokuwa na msaada pale kwenye kiungo.
Tunakubali rotation ingefanyika kutokana na ratiba ngumu lakini ingefanyika kipindi cha pili baada ya kuwa kikosi cha kwanza kimemaliza kazi yake, mchezaji Kama skudu ni wa kuingia kipindi cha pili tena ikiwa timu ishapata matokeo, mpira wake ni wa show game ambao autakiwi kwa timu inayosaka matokeo kwa udi na uvumba!
Yote kwa yote kuteleza sio kuanguka ndio mpira ulivyo na ndio maana unapendwa na watu duniani, kipigo kitamuamsha kocha na wachezaji wake na kuelewa ya kwamba dharau yoyote Ile inaweza kuwaangamiza na kuwapotezea ramani ya kuusaka ubingwa, sidhani Kama atarudia kupanga kikosi cha majaribio tena kwenye mechi yoyote Ile, kitendo cha kuanza na wachezaji 7 wakaa benchi ambao hawakuwa na mechi fitness yoyote ilikuwa ni kitanzi cha kwanza kwa Gamondi.
Rotation huwa inafanyika kwa umakini ili kubalance nguvu ya timu isipotee kutokana na wengine kutokuwa timamu kimwili, lakini yeye akaingia mkenge!
Maumivu ni kwa mashabiki na wanachama lakini wakae wakijua ili dhahabu iwe dhahabu ni lazima ipite kwenye moto, kipigo cha IHEFU kimempa kocha Gamondi somo zuri na kitamuamsha usingizini na kumkaribisha rasmi kwenye LIGI ya Tanzania.
IHEFU wamefanya kazi yao na wanastahili pongezi lakini waendelee ivyo ivyo na kwenye mechi nyingine na sio waishie kukamia mechi moja tu kati ya mechi 30 za ligi.
NB: Mganga wa Ihefu ni kiboko pale mbalali kashindikana😆😆😆