Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 57,103
- 128,722
Wanabodi
Leo nimepata tena fursa ya kuwaletea PMNA.
Kwa vile hii PMNA ni kitu kipya, hizi siku za mwanzo nitakuwa kila siku nikifafanua PMNA ni nini.
PMNA ni news analysis, uchambuzi wa habari, kufuatia kuwepo kwa gaps kwenye news analysis kwenye media zetu, kuanzia magezeti, radio, TV na online media, hakuna uchambuzi wa habari on serious issues zinazolikabili taifa letu.
Kufuatia uzoefu wangu wa long experience ya zaidi ya miaka 30 newsroom, nina uwezo wa kufanya News analysis ya habari yoyote.
Kwenye News analysis yangu
Kwanza nitakuwekea News yenyewe
Kisha nitakuchambulia kilichosemwa au kuripotiwa kwenye News hiyo nikieleza ni what does it mean
Mwisho nitamalizia umuhimu wake kwa Taifa letu kwa maslahi ya taifa
PMNA ya leo ni kauli hii ya Makamu wa Rais, Balozi Dr Emmanuel Nchimbi, akikemea ujinga ujinga fulani ambao ni kweli upo sana tuu.
Kwanza tumsikilize Dr. Nchimbi kwenye video hii
View: https://youtu.be/6bTfOAJgt3w?si=Fr0vq9VdzfOcbQhV
Baada ya kuisikia tuje kwenye
nakala ya maneno (transcript) kutoka kwenye video hiyo. Video hiyo inamwonyesha Dr. Emmanuel Nchimbi (Makamu wa Rais) akizungumzia umoja wa kitaifa na umuhimu wa kuacha migogoro ya kisiasa.
Hapa Makamu Rais Balozi Dr Nchimbi, anathibitisha jinsi anavyokerwa na vitu fulani fulani vya kijinga jinga vinavyofanywa na viongozi wenzake, moja ya vitu hivyo vya kijinga ni kwa viongozi wa vyama vya siasa kugombana gombana kwasababu ya tofauti za kisiasa na tofauti za vyama. Huko Kugombana gombana amekuita ujinga.
Hii maana yake viongozi wetu wanaogombana kwasababu ya vyama, viongozi hao ni wajinga na huko Kugombana gombana kwasababu ya vyama ni ujinga!.
Akakumbushia alipokuwa KM wa Chama Kubwa, Chama Cha Mapinduzi, alikuwa akiona viongozi wa CCM wanatoa kauli mbofu mbofu dhidi ya upinzani, alikemea.
Amemalizia kwa kusisitiza usawa wa vyama kwa mujibu wa Katiba, watu wote wa vyama vyote wako kihalali kikatiba na kisheria kwenye vyama tofauti na vyote viko kwa maslahi ya taifa letu moja la Tanzania.
My Take
Hili jambo niliwahi kulizungumza humu hadi kuliandikia makala kwa kumpongeza yule Rais Samia wa enzi zile Asante sana Rais Samia kwa kuliponya Taifa. Umeonesha kwa kauli na matendo; tunajenga nyumba moja, hakuna sababu ya kugombea fito!
Hivyo natoa wito kwa wana JF na Watanzania kwa ujumla, tuunge mkono kauli hii ya Makamu wa Rais Dr Emmanuel Nchimbi kwa kuukataa kabisa huu ujinga wa kugombana kwa ajili ya tofauti za kiitikadi au za vyama, na tusiihie kuukataa huo ujinga, bali pia tuwakatae, hao wajinga!.
Mungu Ibariki Tanzania
Paskali
Pia soma > Nchimbi: Mimi hata mambo ya kugombana kivyama vyama siyapendi naona ni ujinga tu
Leo nimepata tena fursa ya kuwaletea PMNA.
Kwa vile hii PMNA ni kitu kipya, hizi siku za mwanzo nitakuwa kila siku nikifafanua PMNA ni nini.
PMNA ni news analysis, uchambuzi wa habari, kufuatia kuwepo kwa gaps kwenye news analysis kwenye media zetu, kuanzia magezeti, radio, TV na online media, hakuna uchambuzi wa habari on serious issues zinazolikabili taifa letu.
Kufuatia uzoefu wangu wa long experience ya zaidi ya miaka 30 newsroom, nina uwezo wa kufanya News analysis ya habari yoyote.
Kwenye News analysis yangu
Kwanza nitakuwekea News yenyewe
Kisha nitakuchambulia kilichosemwa au kuripotiwa kwenye News hiyo nikieleza ni what does it mean
Mwisho nitamalizia umuhimu wake kwa Taifa letu kwa maslahi ya taifa
PMNA ya leo ni kauli hii ya Makamu wa Rais, Balozi Dr Emmanuel Nchimbi, akikemea ujinga ujinga fulani ambao ni kweli upo sana tuu.
Kwanza tumsikilize Dr. Nchimbi kwenye video hii
View: https://youtu.be/6bTfOAJgt3w?si=Fr0vq9VdzfOcbQhV
Baada ya kuisikia tuje kwenye
nakala ya maneno (transcript) kutoka kwenye video hiyo. Video hiyo inamwonyesha Dr. Emmanuel Nchimbi (Makamu wa Rais) akizungumzia umoja wa kitaifa na umuhimu wa kuacha migogoro ya kisiasa.
- Kila Mtanzania ana Wajibu: Dr. Nchimbi anasisitiza kuwa kila mtu ana nafasi na wajibu wa kuitumikia nchi, na hatupaswi kutegemeana bali kila mmoja atumie nguvu zake zote [00:00].
- Kupinga Migogoro ya Vyama: Alieleza kutopendezwa kwake na migogoro ya vyama vya siasa, akiiita kuwa ni "ujinga" [00:11]. Anahoji kwanini watu wagombane ilhali nchi ni moja na ni ya wote [00:21].
- Kukemea Lugha Chafu: Alikumbushia wakati akiwa Katibu Mkuu, alikuwa akimkemea mwana-CCM yeyote aliyekuwa akizungumza maneno ya ovyo dhidi ya vyama vya upinzani [00:29].
- Vyama vya Siasa na Katiba: Alibainisha kuwa vyama vyote vimeundwa kwa mujibu wa katiba, na kujiunga na chama kingine ni njia tu ya kutaka kuitumikia nchi kwa mtazamo tofauti, lakini mwisho wa siku yote ni "utumishi" [00:35].
Hapa Makamu Rais Balozi Dr Nchimbi, anathibitisha jinsi anavyokerwa na vitu fulani fulani vya kijinga jinga vinavyofanywa na viongozi wenzake, moja ya vitu hivyo vya kijinga ni kwa viongozi wa vyama vya siasa kugombana gombana kwasababu ya tofauti za kisiasa na tofauti za vyama. Huko Kugombana gombana amekuita ujinga.
Hii maana yake viongozi wetu wanaogombana kwasababu ya vyama, viongozi hao ni wajinga na huko Kugombana gombana kwasababu ya vyama ni ujinga!.
Akakumbushia alipokuwa KM wa Chama Kubwa, Chama Cha Mapinduzi, alikuwa akiona viongozi wa CCM wanatoa kauli mbofu mbofu dhidi ya upinzani, alikemea.
Amemalizia kwa kusisitiza usawa wa vyama kwa mujibu wa Katiba, watu wote wa vyama vyote wako kihalali kikatiba na kisheria kwenye vyama tofauti na vyote viko kwa maslahi ya taifa letu moja la Tanzania.
My Take
Hili jambo niliwahi kulizungumza humu hadi kuliandikia makala kwa kumpongeza yule Rais Samia wa enzi zile Asante sana Rais Samia kwa kuliponya Taifa. Umeonesha kwa kauli na matendo; tunajenga nyumba moja, hakuna sababu ya kugombea fito!
Hivyo natoa wito kwa wana JF na Watanzania kwa ujumla, tuunge mkono kauli hii ya Makamu wa Rais Dr Emmanuel Nchimbi kwa kuukataa kabisa huu ujinga wa kugombana kwa ajili ya tofauti za kiitikadi au za vyama, na tusiihie kuukataa huo ujinga, bali pia tuwakatae, hao wajinga!.
Mungu Ibariki Tanzania
Paskali
Pia soma > Nchimbi: Mimi hata mambo ya kugombana kivyama vyama siyapendi naona ni ujinga tu