Miji ya sasa hivi hasa dar usihangaike na barabara ya lami mkuu. Wewe angalia barabara zipo za kufika mpaka kwako. Je kiwanja chako hakipitiwi na changamoto za miundombinu kama barabara basi.
Barabara za lami na umeme vitawafuata tu huko. Wewe kama una hela kwa dar. (Japo sio dar tu,siku hizi mpaka mawilayani huko) nunua sana maeneo,angalia tu barabara zinapita kwako.
Ninachotaka kukuambia watu wanaongezeka kwa kasi mno. Hayo maeneo yanaonekana ni mbali au polini kwa sasa. Ipe miaka kuanzia miaka mitano tu.
Mfano kuna mtu kazaliwa Gongo la mboto huko au Mbagala,chanika ,miaka 16 iliyopita hajawahi fika kariakoo. Unajua kwa nini? Ksbb Mbagala ya sasa ni town inayojitosheleza. Kuna kila kitu hadi maduka ya jumla. Wakati kitambo kidogo tu nyuma miaka 10 nyuma ungekukataa. Hata kigamboni tu huko kuna watu mpaka leo wanakukataa. Hawajatembea kuiona inavyokimbia