Mwanzoni mwa mwaka huu mpenzi ambaye nilimpenda kumuamini na kumthamini alinisaliti na kwenda kwa mtu mwingine ambaye ni mtoto wa pedeshee mmoja hapa mjini. Iliniuma sana mpaka ikapelekea kuchanganyikiwa na kusababisha nisimwamini msichana yeyote yule ktk uso wa dunia hii. Baada ya hapo nilijianzishia kajitabia cha kwenda kwa kina dada powa(malaya) kumalizia haja zangu hasa maeneo yale ya mwananyamala, mpaka nikaja kuzoeana na dada mmoja hivi ambaye anaitwa Irene ambaye ni mmoja wa wanaouza mwili maeneo hayo, huyu dada ndo aliyenifanya nipende kwenda karibu siku zote hii yote kwa uzuri aliokuwa nao. Irene alikuwa ni msichana ambaye yuko tofauti na wasichana wengine maeneo yale, hii yote ni kwa uzuri aliokuwa nao kwani alijaaliwa sura yenye mvuto iliyopambwa na tabasamu mwanana ambalo ndani yake kuna mwanya mzuuri uliochangia uzuri wa sura yake. Mbali nakuwa na sura yenye mvuto pia Irene alikuwa na umbo zuri lililojaa hasa maeneo yaleee ya nyuma a.k.a uani, pia uzuri wake ulichangiwa na weupe aliokuwa nao, kwa kumuangalia tu Irene hakustahili kufanya ile kazi kwani ni mdada ambaye angeliweza kuolewa na mtu mwenye fedha zake, vitu hivi viliinifanya nizoeane na huyu mdada mpaka siku nyingine huwa nasahau kutumia kinga. Kwenye mwezi wa tano nilipata safarii ya kikazi jijini Arusha ya karibu miezi miwili, safari hii ilinisababisha nimisi kweli mambo ya Irene, kwani mbali na uzuri wake pia huyu mdada alikuwa anajua mambo yetu yalee ya kunako sita kwa sita na kufanya hata mshahara wako au mauzo yako ya wiki nzima ukamkabidhi yeye kutokana na mambo yake. Baada ya miezi miwili nilirudi Dar na siku hiyohiyo nilifika ofisini kwa Irene kupata ile kitu roho inapenda, nilivyofika maeneo yale sikumkuta Irene nilivyomuulizia nilipata majibu ambayo yalinifanya nidondoke kwa mshtuko kwani Irene alishafariki tangu wiki kadhaa zilizopita kwa ugonjwa wa ukimwi, siku hiyo ndo siku ambayo niliyogundua paa la chumbani kwangu limetobotoboka hii yote ni kwa kukosa usingizi kwa mawazo. Asubuhi yake nilikwenda kituo cha afya kwenda kupima kama nami nimo ktk listi ya IZRAEL. Majibu nilyoyapata ya kanifanya nizimie siku tatu kwani nami nilikuwa nimeathirika na ugonjwa hatari wa Ukimwi. Yaliiyofata ni majuto kwani maamuzi niliyoyachukua baada ya mpenzi wangu kunisaliti yamenifanya kupata gonjwa ambalo sikulitarajia kulipata ktk maisha yangu. NB: simulizi hii ni ya kutunga na haiusiani na mimi hata kidogo bali nimeiandika kwa lengo la kutufumbua macho na kukumbushana juu ya swala zima la Ukimwi na kuwa waaminifu ktk ndoa au mahusiano yetu.