Pitching ya uwekezaji

Pitching ya uwekezaji

Mhina Martin

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2017
Posts
202
Reaction score
261
PITCH YA KILIMO– MANTO FARMING SOLUTIONS(MARTIN MHINA

Habari za wakati huu Ndugu,Jina langu naitwa Martin Mhina, mimi ni Bwana Shamba na mwanzilishi wa MANTO FARMING SOLUTIONS.

Tunajishughulisha na uzalishaji wa mazao ya chakula kwa mpangilio wa misimu ili kuhakikisha tunazalisha mwaka mzima bila kukosa soko.

Lengo letu kuu ni kuzalisha chakula kwa wingi, ubora na kwa faida, huku tukiwapa wawekezaji fursa ya kupata mapato ya uhakika kupitia kilimo cha kisasa.

Sekta ya kilimo Tanzania inakabiliwa na changamoto kuu tatu:
  • Uzalishaji usio na mpangilio wa misimu
  • Wakulima kukosa mtaji wa uhakika

Hasara kutokana na kushuka kwa bei sokoni
Lakini ukweli ni huu:
  • Mahitaji ya chakula yanaongezeka kila siku Lakini uzalishaji wa uhakika bado ni mdogo
Hii inamaanisha kuna fursa kubwa ya biashara kwa yeyote atakayefanya kilimo kwa mpangilio na uwekezaji sahihi.

MANTO FARMING SOLUTIONS tumekuja na suluhisho la vitendo:
Tunafanya kilimo kwa vipindi vitatu kwa mwaka, kuhakikisha uzalishaji unaendelea muda wote Kwa Ratiba ya mazao ifuatayo
  • Desemba – Machi: Nyanya, Mahindi, Mpunga wa kumwaga.
  • Aprili – Juni: Mpunga wa umwagiliaji (scheme), Maharage ya njano
  • Agosti – Oktoba: Vitunguu, Viazi mviringo,hoho
Mfumo huu unatupa faida kubwa
- Hakuna kukaa bila uzalishaji
-Tunatumia vizuri misimu ya mvua na umwagiliaji
-Tunapunguza hatari ya hasara

Kwa sasa tunaingia kwenye kilimo cha mpunga wa umwagiliaji (scheme) — ambayo ni moja ya biashara yenye uhakika mkubwa wa chakula na soko.

Huu ndio mfano halisi wa uwekezaji:
Gharama:
Ekari 1 = Tsh 1,300,000
Ekari 5 = Tsh 6,500,000 (mpaka kuvuna)
MAPATO ,Uzalishaji:
-Minimum: Gunia 22 × 5 ekari = 110 magunia
-Maximum: Gunia 28 × 5 ekari = 140 magunia
Baada ya kukoboa (mchele):
-110 gunia = Kilo 7,480
-140 gunia = Kilo 10,080
Mauzo:
Bei ya kilo = Tsh 2,000
Mapato ya chini:
7,480 × 2,000 = Tsh 14,960,000
Mapato ya juu:
10,080 × 2,000 = Tsh 20,160,000
FAIDA
Ukitoa gharama ya Tsh 6,500,000:
-Faida ya chini:
Tsh 8,460,000
-Faida ya juu:
Tsh 13,660,000
Hii ni kwa msimu mmoja tu.

Kilimo hiki kina uhakika kwa sababu:
-Mahitaji ya mchele ni ya kudumu
-Tunatumia umwagiliaji (hakuna kutegemea mvua pekee)
-Tunauza mchele (thamani kubwa kuliko mpunga)
-Tunafanya kwa mfumo wa kitaalamu

Na kama tunavyosema:
“Kidole kimoja hakivunji chawa — karibu tushirikiane,Tunakaribisha wawekezaji kushirikiana nasi kwa:
-Kuongeza mtaji wa uzalishaji
-Kupata sehemu ya faida kulingana na makubaliano
Mfano:
Uwekezaji wa ekari 5 = Tsh 6.5M
Faida inaweza kufika hadi zaidi ya Tsh 13M kwa msimu.

Kilimo sio tu chakula — ni biashara yenye faida kubwa sana ikiwa itafanywa kwa mpangilio sahihi.
MANTO FARMING SOLUTIONS tuko tayari kushirikiana na wawekezaji wanaotaka:
  • Faida
  • Uhakika
-Ukuaji wa muda mrefu
MAWASILIANO
Simu 0716898393, email maritinmuhina@gmail.com Korogwe Tanga
Karibu tushirikiane kujenga mafanikio kupitia kilimo.
 

Attachments

  • IMG_20260404_080812.jpg
    IMG_20260404_080812.jpg
    998.6 KB · Views: 1
  • IMG_20260404_072844.jpg
    IMG_20260404_072844.jpg
    1.2 MB · Views: 1
  • IMG_20260404_073702.jpg
    IMG_20260404_073702.jpg
    876.3 KB · Views: 1
  • IMG_20260404_081113.jpg
    IMG_20260404_081113.jpg
    873 KB · Views: 1
  • IMG_20260322_172856_HDR.jpg
    IMG_20260322_172856_HDR.jpg
    713.1 KB · Views: 1
  • IMG_20260404_073806.jpg
    IMG_20260404_073806.jpg
    1 MB · Views: 1
Back
Top Bottom