Pingamizi lililokuwa limewekwa na mgombea ubunge kupitia CUF na washirika wake dhidi ya Chadema limetupiliwa mbali na msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Chalinze jioni hii.
Msimamizi wa uchaguzi baada ya kupokea majibu ya Chadema na kuyapitia amesema hoja zote za CUF hazina msingi wowote.
Amesema CUF wameshindwa kuthibitisha chochote na hivyo kuonekana wanapoteza muda tu.
Hivyo msimamizi amemtangaza Rasmi Mathayo Torongey kama mgombea halali wa CHADEMA.
Katibu mkuu wa Chadema Dr Wilbroad Slaa ambaye leo alishangiliwa kwa maneno... Rais...Rais..Rais na maelfu ya waendesha Bodaboda Dar anatarajiwa kuzindua Rasmi kampeni za Chadema Jumapili hii.
Msimamizi wa uchaguzi baada ya kupokea majibu ya Chadema na kuyapitia amesema hoja zote za CUF hazina msingi wowote.
Amesema CUF wameshindwa kuthibitisha chochote na hivyo kuonekana wanapoteza muda tu.
Hivyo msimamizi amemtangaza Rasmi Mathayo Torongey kama mgombea halali wa CHADEMA.
Katibu mkuu wa Chadema Dr Wilbroad Slaa ambaye leo alishangiliwa kwa maneno... Rais...Rais..Rais na maelfu ya waendesha Bodaboda Dar anatarajiwa kuzindua Rasmi kampeni za Chadema Jumapili hii.