Picha: Usahili post ya Mkaguzi msaidizi wa Uhamiaji - Uwanja wa Taifa

Likwanda

JF-Expert Member
Jun 16, 2011
3,910
1,131
Watu ni wengi sana na bado wanazidi kuja, kama ni mechi basi ni sawa na wale wanaoingia katika mechi za simba/yanga wanapocheza na timu za mikoani.

Ulinzi naona ni jukumu la askari magereza.

Nimehudhuria interview na kufanya ila hii ya uhamiaji kwa mie imevunja record.

attachment.php



attachment.php
 
Watu ni wengi sana na bado wanazidi kuja, kama ni mechi basi ni sawa na wale wanaoingia ktk mechi za simba/yanga wanapocheza na timu za mikoani. Ulinzi naona ni jukumu la askari magereza.

whaat!! tumefikia huko?
 
ninoomaaaa yaan...niko hapa..hata sehem ya kupumua hakuna...good thing nimekutana na mates weng nliosoma nao..tangu primary mpk chuo kikuu..watu ni nyomiii
 
Bila shaka leo hawa vijana wanaanza usaili wao pale Taifa. Mungu awatangulie na wawe tayari kwa lolote ninawaombea sana wale wasio na baba,mama, shangz,mjomba, kaka, dada nk.

Yani wasio na mchongo kama mimi mana shetani ameshikilia sana uonevu kwetu katika maswala ya ajira.

Mungu awatangulie
 
Sure mzazi. Nawaombea wale wasio na mtegemezi, wajue Mungu yupo pamoja nao. Pia, wakumbuke kuna kupata na kukosa.

PS: Ni marufuku kukata tamaa.
 
Kwa kweli saa 12:15 nilikuwa hapo Uwanja wa Taifa. Hali inatisha. Vijana ni wengi mno. Nimeshindwa kupata picha baada ya simu yangu kuishiwa chaji. Kwa hakika tukio la usaili la aina hii sijawahi kuliona wala kuliwazia katika Tanzania. Tunaposema ukosefu wa ajira ni bomu linalosubiri kulipuka, kwa hakika tunamaanisha hivyo. Ningefarijika kama wapiga picha za televisheni wangefika hapo uwanjani ili kuwaonyesha Watanzania na walimwengu namna vijana zaidi ya 10,000 walivyoitwa kuwania nafasi 70 tu. Narudia kusema, hali inatisha!!!!
 
Mungu awatie nguvu jamani, Hakika ni Mungu pekee ndiye anayejua kwa kutupeleka sisi wasakatonge.
 
duh..Mungu awatangulie ndugu zangu..msikate tamaa hakuna jambo lisiloshindikana
 
Back
Top Bottom