PISTO LERO
JF-Expert Member
- Mar 8, 2011
- 2,819
- 1,455
Baraza la vijana CHADEMA (BAVICHA ) Limefanya mkutano mkubwa katika Jimbo la Bariadi,hali iliyomfanya Chenge kuchanganyikiwa.
Viongozi wa BAVICHA Katibu Mkuu wa BAVICHA Julius Mwita na M/kiti Mstaafu wa Bavicha John Heche,wamevunja record leo katika mkutano wa hadhara uliofanywa leo Bariadi.Mkutano huo ulihudhuriwa na maelfu ya watu wengi wakiwa na hasira na nyuso zilizoonesha kuchoshwa na tabia ya wizi inayofanywa mara kwa mara na Mbunge wao.
Wakizungumza katika mkutano huo na kushangiliwa kwa makofi na wananchi walihudhuria kwa Wingi mkutano huo,John Heche nae Katibu Mkuu wa BAVICHA Julius Mwita,walieleza wazi wazi namna Mbunge huyo anavyoshiriki kuliingiza Taifa hili katika matatizo Sugu ya Ufisadi,yanayopelekea Watanzania kubaki masikini kila kukicha.
Inasemekana pia,mahudhurio ya mkutano huo ndio yalipelekea Chenge kuchanganyikiwa na kujiona kwamba hana chake,hata baada ya mkutano kutaka kuwajeruhi viongozi hao kwa risasi za moto.
Attachments
-
10629575_1571902386412035_3543511444662768711_n.jpg86.4 KB · Views: 2,627 -
10956395_1571901576412116_1846946374404481741_n.jpg98.2 KB · Views: 2,130 -
11169248_1571902153078725_8470126082755604008_n.jpg100.1 KB · Views: 1,954 -
11152337_1571901829745424_63767319643974081_n.jpg68.9 KB · Views: 1,811 -
11174801_1571902523078688_4796740191368535409_n.jpg102.6 KB · Views: 1,766 -
11182315_1571902776411996_2105894708622335930_n.jpg103 KB · Views: 1,880