Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Mama mmoja amehudhuria mahafali ya chuo kikuu kwa niaba ya mwanawe aliyefariki baada ya kuuawa na jeshi la polisi siku ya tarehe 29 Oktoba, wakati wa mauaji ya vijana waliodai mabadiliko nchini.
Kijana huyo aliuawa akiwa anarudi nyumbani, siku chache kabla ya kuhitimu masomo yake.
Katika mahafali hayo, mama yake alivaa mavazi ya wahitimu na kubeba picha ya mwanawe kama ishara ya kumuenzi na kutambua juhudi zake za kufikia hatua ya kuhitimu.
Tukio hilo limeacha simanzi kubwa na kuibua upya maswali kuhusu uwajibikaji juu ya vifo vya vijana vilivyotokea siku hiyo.
Tukio hilo limeacha simanzi kubwa na kuibua upya maswali kuhusu uwajibikaji juu ya vifo vya vijana vilivyotokea siku hiyo.