Picha hizi hatuwatendei haki Polisi

Mkuu sipingani na wewe ila nakupa taarifa kuwa Mh.Mwakyembe wakati wa sakata la richmond aliwahi sema ''hakuna haki polisi,haki inapatikana mahakamani''
Na hawa polisi wamekuwa mstari wa mbele kupoka haki za raia kwenye mahabusu zao,sasa kama nao hawakutendewa haki waende mahakamani maana polisi hakuna haki.
 

mkuu mrangi bora umeliona hili . Tulio wengi tunaangalia hapa tulipo mahali ambapo jiwe limedondokea ila hatuangalii hili jiwe limerushwa kutoka wapi na nani karusha....

Hawajiulizi masuala ya EPA, yameishia wapi?
Haya yote yamefichwa kimya lakn hamna na anayehoji na wahusika wote wanazidi kuongezewa mishahara.

Kibaya zaidi siasa imefikia hatua ya kutugombanisha raia na askari wetu, askari polisi wametolewa kafara na sisi kwa upofu wetu tunakubali kuwalaumu na kuwaona ni wanyama kwetu.
 
Last edited by a moderator:



Kumbuka kuwa asilimia kubwa ya polisi unaowaona hasa walioko makao makuu ni watu wanye soo huko walipokuwa,halafu hao ndio watunga sera na watoa maamuzi juu ya askari wadogo walioko nchi nzima.

Na pia polisi walivyo na roho mbaya dhidi ya raia ndivyo walivyo na roho mbaya wao kwa wao.Wanavyoweza kumbambikia raia kesi na kuhakikisha anafungwa ndivyo wanavyokomaliana wenyewe kwa wenyewe mpaka wafukuzane. Wengi wanalaana kama Kamuhanda,hawawezi kutenda kwa utu na ubinadamu zaidi ya kuangalia maslahi yao.

Wananchi na vyombo vya habari sasa pia vitupie macho matendo mabaya ya kinai yanayofanywa na viongozi mbalimbali sio kuangalia vitu vidogo visivyo na madhara makubwa ya kiuchumi na kijamii.

Askari anayewanyanyasa na kuwatumia wauza gongo kama mtaji wake au anayeshirikiana na majambazi na wauza magendo na madawa ya kulevya anaathari kubwa sana kwenye jamii.Chaajabu hao ndio marafiki wakubwa wa wakubwa kwa sababu ya kuwapelekea na kugawana kile wanachopata kwa njia haram.

Tatizo pia ni sheria zinazotumika kuwasimamia askari wadogo ni zile za vibarua wa kikoloni wakati wakubwa wanasimamiwa na sheria za utumishi. Ndio maana askari wadogo wanakata tamaa na maisha na kujiliwaza kwa kukumbatiana kwa fedheha kubwa kwani hawajui hatima yao ya kesho.Mishahara isiyokidhi mahitaji yao na isiyoongezeka mpaka pale tu wanapopandishwa vyeo na sababu pia ya kuwana jeshi lisilo na askari wasio na matumaini.

Sijajua katiba pendekezwa imezungumziaje juu ya haki za haya makundi ya majeshi kimaisha mbali na wajibu wao wa kutii chama tawala na kumtii amiri Jeshi mkuu.

Kwa mtizamo wangu wale askari walioonyesha vitendo vya kifuska na kupigwa picha walistahili kupewa adhabu nyingine ikiwa ni pamoja na kurudishwa Chuoni ili wafunze adabu kwa mwezi mmoja ,lakini kuwafukuza kazi ni adhabu kubwa mno labda kama record yao ya huko nyuma inaonyesha kuwa na tabia mbaya za aina hiyo na kutotii wakubwa wao.
 
Policcm wapewe haki gani wao si wanajifanya wako juu ya sheria hii ndiyo dawa yao hamna namna nyingine tumechoka
 
mtoa mada ukhali gani ndugu yangu...I hope u having beautiful Sunday
hawa polisi unaowatetea somehow ni watu wabaya sana ndugu yangu so we need to expose them..
1 watupige bila makosa
2 watubambikie kesi
3 baadhi ya matrafick wanyanyasaji wakubwa wakiwa katika ile white traffic uniform wanajiita GODS OF THE ROAD
4 mlipa kodi anamlipa huyu polisi mshahara
still anakwenda kucheza na mwanamke muda wa kazi...NA WAFUKUZWE TU
 

Jamaa jmechangia vizuri sana mimi niliposhika tu katiba inayopendekezwa nimesoma surabya kumi na saba ambayo inahusu ulinzi wa jamuhuri ya muungano kwanza nikuhakikishie vyombo vya ulinzi wanavyo vijua wao ni JWTZ,POLICE,NA TISS kwahiyo uhamiaji magereza zimamoto hayajulikani kabisaa na kuhusu ajira kwa policr au mfumo mzima wa ufanyaji kazi wanasema watapokea order tu kwa mkuu wo yani Rais kwaiyo kama ni police wa chini system itaendekea hivyohivyo ilivyo akikosea kidogo tu kisa ni cpl au constable au private aaaah kesho hamna kazi hii katiba ikipitishwa itawekewa vilaka haraka sana aisee haina kitu kipya juu ya haya mambo ya kiulinzi hakuna maboresho yoyote
 
Wapigwe tu picha na zirushwe hewani,kwa hili sitaki kufikiri zaidi kama ambavyo na wenyewe wanavyo tupiga kwa marungu,mabomu na risasi bila kufikiri(its an order).
 
Pole sana bwana afande kwa kuguswa. Umeona jinsi inavyouma, sasa sisi mnapotunyanyasa na kubambika kesi uwa tunaumia hivyo ama mkiamrishwa "Piga" tunaumia hivyo. Sisi hatuna kwa kushitaki ninyi maana mnatugeuzia hizo kesi sasa hiyo ndio njia yetu ya kufikisha ujumbe. Na tutawapiga sana ndio mkome muungane na sisi japo kufukuzwa naona kama mnaonewa mbona waheshimiwa hawafukuzwi?
 

hahahaaaa! Mm sio afande bhana ni raia mwema kama ww.
Ila nafikisha ujumbe tu kwa watu wenye mawazo kama yako
 
Mkuu hayo ni matokeo ya kuporomoka kwa maadili ya kazi kuanzia kwa viongozi wa juu na sasa watendaji wa chini wanamalizia tu ila ndio hivyo hakuna haki wadogo wanasulubiwa ili kuonesha utendaji lakini wakubwa kimyakimya.Unakumbuka mkubwa fulani aliyezusha CUF wameingiza majambia alishawahi kukumbwa na skendo ya kuzaa na dada wa kazi kwani iliishia wapi? Hapo ndio ujue maadili yakiporomoka na hadhi inashuka.
 
hahahaaaa! Mm sio afande bhana ni raia mwema kama ww.
Ila nafikisha ujumbe tu kwa watu wenye mawazo kama yako

Haya asante mkuu kuna nyingine ninayo hapa picha mupyaaaa ya jana tu JWTZ kauchapa kweli kweli nielekeze namna ya ku-upload nitupie naye huyu kiote nyasi, ila ni jamaa yangu maskini sema anaboa mambo yake ya kikuda
 
%98hakuna watu wenye roho mbaya na ya kwanini kama hawa, sio wa kuhurumia hawa walafi na malaghai urafiki wao ukiwapa hongo. hapana hawastahili hiyo huruma.
 
Si mnaona katiba pendekezwa inavyowalinda vigogo? Hawataki kusika kitu kuwajibishwa
. Kwa hiyo dagaa tupige kura ya HAPANA mpaka kieleweke
 
kosa moja haliwezi kuhalalishwa kwa kosa lingine. Polisi wana makosa mengi ambayo sio rahisi kupata ushahidi. Wananchi wana usongo nao sana. Baadhi ya makosa hayo ni pamoja na kudai rushwa, kubambikia watu kesi, kuwapiga watuhumwa wakifika kituo cha polisi hata kabla ya kufika kituoni. Wananchi wanaofanyiwa madhira haya ni wananchi wanyonge wasio na kipato wala cheo. Tena wananchi hawa hufanyiwa na polisi wa vyeo vya chini. Wakubwa hawaguswi hata kidogo. Kwa ufupi ni kuwa katika nchi yetu wanyonge tunaoneana wenyewe kwa wenyewe wakati wakubwa hulindana wao kwa wao, hawatulindi sisi na wala hawajui uchungu tulionao. Mpaka wetu na wao ni mkubwa unaanzia kichwani 'Capture the brain, the trunk will follow by itself' Akili zetu bado hazijajua kama tunaumizana wao kwa wao hivyo kujiongezea shida juu ya shida. Tumetekwa akili kama mtumwa kulindwa na mtumwa mwenzie unyapala ni kilemba cha ukoka tu.
Polisi hawa wana makosa gani wakati sifa mojawapo ya kuajiriwa kazi ya polisi lazima uwe rijali na mapenzi humea popote na wakati wowote, mapenzi nidawa ya msongo wa mawazo, huondoa uchovu. Sio ajabu kukuta boss anapendana na PS (Katibu muhtasi) wake tena pengine ofisini mbele ya picha ya Rais.
Kibaya zaidi hawa polisi walipigwa picha na polisi mwenzao. Wakubwa, licha kupeana mapenzi kazini pia huhongana vyeo na wananchi tunawalipa wapenzi wao mishahara kwa kodi zetu. Si nia yangu kuwa wadogo tusiwe waadilifu la hasha, nataka tuige kusaidiana kama wanavyosaidia wakubwa wetu
 
Lakini mleta mada tuende mbele turudi nyuma,unafaham dhamana ya askar police akiwa ndani ya uniform?

Kufanya jambo la ajabu kama lile ilikuwa ni kuikosea adabu bendera viunoni mwao.wanastahili,tustafute huruma kwa kusema eti mbona furani ni nani amefanya hakuna kilichotokea.tunakosea kosa ni kosa ila kila mtu anajua kuwa amesimamia wapi nchi hii ili asianguke.

Yaani kuna kaswali kanajirudia kichwani hivi walishindwa nn kuvumilia mpaka watoke kwenye majukumu???,na kwann wapige picha???.wakajaribu kilimo sio mbaya.

Alafu lile la kike lina pete ya ndoa.maza fanta.
 
Bro nimependa comment yako, upo right
 
.. mkorinto elewa ya kwamba siyo kosa tu la kukaa kimahaba ukiwa na uniform ndiyo uadabishwe peke yake, mfano askari akikuomba rushwa akiwa na uniform huku kavaa mkanda wa bendera kiunonI ni kosa kubwa...tujaribu kuangalia na makosa mengine pua ya askari na viongozi wengine wa serikali
 
Last edited by a moderator:

umeongea point sana mkuu...
Hicho ndicho kinaumiza sana tunaumizana sisi wanyonge wakat wakubwa ambao ndio makupe wanakula bata...

Ndio maana niliongea pale mwanzo kuwa sio askari wote wanapenda kunyanyasa wananchi bali unyonge na umaskin ndio huwafanya wafanye hvyo.

Askari mdogo analazimika kutii amri ya kiongozi wake ndio maana huonekana kama wanakandamiza raia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…