Naijua songea vizuri sana.wamekwenda tu kuangalia na pia ccm wamepeleka watu wao.ukijumulisha wana ccm na watu wachache wanaomfuata.kiujumla kwa mtu mwenye akili nzima unafikiri zitto kuanzisha chama hiki ndicho kitamfanya haitoe ccm madarakani kwenye uchaguzi mwaka huu??.zitto anajua au anatambua kuwa watanzania wamechoka na utawala wa unaobebana ,wa kirafiki,husiojali kuna watoto wanakosa fee ya kwenda chuo kikuu huku watoto wao wakiwasomesha nje kwa pesa za serikali?.zitto hameshindwa kujua au kuacha kiburi kama yeye ni zaidi kwenye chama na kujikita kuunganisha nguvu kuing'oa ccm kama walivyofanya kenya??.Nini anafikiri???.Mimi mwenyewe kuna vitu sielewani na chadema na pia ukawa lakini ni naangalia nini cha muhimu kwenye kipindi hiki cha mpito.Hakuna mtu hasiojua uozo wa ccm ,sitaki poteza muda kuelezea kila kitu.wameshindwa kupelekana mahakamani ,mahakama ni yao ,wewe iba kipande cha kuku kwa mama ntilie kinacho cost sh 300.utaona nguvu kubwa inayotumia zaidi ya sh 10,000.inatamtafuta kijana aliyeiba.Naelezea hivi sio namtetea mtu yeyote anaiba hata ikiwa kitu kidogo hapana ,nimetolea mfano tu jinsi hii serikali ya ccm imefikia.kwa hiyo tuache tofauti zetu zote,tumtazame adui yetu ni ufalme wa chama cha mafisadi ccm kinaondoka madarakani iwe hisiwe.Zitto wewe ni smart lakini kwa hili umeonekana ni sio smart ,ningekupa au kukupongeza ungekaa kimya na kuomba msamaha na kujiunga kwenye vile vyama wilivyounda ukawa ili upeleke nguvu.Na kufanya kazi kwa ajili ya kuiondoa ccm ,sio unavyofanya sasa.Pole sana kwa hiyo style yako.Muda ni huu hatuna muda mwingine kuondoa ccm.piga simu kijijini kwako ,tuma msg kama 100 kwa watu tofauti ,tusiwaachie viongozi wa UKAWA tu,peleka bendera zote tatu.utakuwa umeshiriki vizuri kuing'oa ccm.Tumwache zitto aendelee kupotea